DG,
Ninapenda kukujulisha kwamba katika ufuatiliaji wa vitendo vya rushwa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020, leo TAKUKURU(M) Kigoma katika jimbo la uchaguzi la Buhigwe tumekamata Tsh. 210,000/= zilizokuwa zimeshagawiwa Tsh. 10,000/= kwa kila mjumbe kwa wajumbe 21 kutoka kata ya Mnanila jimboni humo katika kikao kilichokuwa kimeitishwa na Mbunge wa jimbo hilo aliyemaliza muda wake Mhe. ALBERT NTABALIBA OBAMA.
Aidha mbunge huyo amesalimisha kwa maafisa wa TAKUKURU kiasi cha Tsh. 2,000,000/= alizokutwa nazo wakati akiendelea na kikao hicho. Fedha Tsh. 210,000/= zilizokamatwa kutoka kwa wajumbe 21 zilikuwa zimegawiwa na Mwenyekiti wa UWT(W) Buhigwe ambaye katika maelezo yake amethibitisha kukabidhiwa fedha hizo na Mhe. Mbunge ALBERT NTABALIBA OBAMA.
Uchunguzi wa tukio hili unaendelea, tutawasilisha taarifa ya matokeo ya uchunguzi mapema iwezekanavyo.
Naomba kuwasilisha tafadhali.
Stay tuned.
=======
Tukio hilo lilitokea Tarehe 07/07/2020 saa nane Mchana. Mbunge aliyemaliza muda wake Obama, alikuwa na kikao halali cha CCM.
Pamoja na kwamba hajatangaza nia ya kugombea Popote, TAKUKURU waliweza kujipenyeza kwenye kikao chake na Walimkuta anagawa elfu 10 kwa kila Mjumbe aliyehudhuria. (alikuwa hagawi yeye, alimpa mtu awagawie Wajumbe hapo Mkutanoni).
Walipomkagua wakakuta ana laki mbili na elfu kumi. Alikua kashagawa elfu kumi kumi kwa Wajumbe 21.
Obama alijitetea kwamba aliwachelewesha wajumbe kuondoka hivyo ilikua ni hela ya chakula cha Mchana kwa Wajumbe waliokuwa wapo mkutanoni tangu saa tatu asubuhi.
TAKUKURU wakawataka waliopokea hela warudishe na wakashikilia laki mbili na Elfu kumi zilizokuwa zinagawiwa kwa Uchunguzi.
Pia wakamtaka Obama kama ana hela yoyote aisalimishe, akasalimisha Milioni Mbili.
Baada ya hapo wakamruhusu aendelee na Vikao vyake kwenye vijiji mbalimbali kama ratiba yake inavyoonesha. Akimaliza atahojiwa..
Hata hivyo Kesho Tarehe kumi saa tatu asubuhi, TAKUKURU Kigoma, itatolea ufafanuzi wa kina swala hili.
Ninapenda kukujulisha kwamba katika ufuatiliaji wa vitendo vya rushwa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020, leo TAKUKURU(M) Kigoma katika jimbo la uchaguzi la Buhigwe tumekamata Tsh. 210,000/= zilizokuwa zimeshagawiwa Tsh. 10,000/= kwa kila mjumbe kwa wajumbe 21 kutoka kata ya Mnanila jimboni humo katika kikao kilichokuwa kimeitishwa na Mbunge wa jimbo hilo aliyemaliza muda wake Mhe. ALBERT NTABALIBA OBAMA.
Aidha mbunge huyo amesalimisha kwa maafisa wa TAKUKURU kiasi cha Tsh. 2,000,000/= alizokutwa nazo wakati akiendelea na kikao hicho. Fedha Tsh. 210,000/= zilizokamatwa kutoka kwa wajumbe 21 zilikuwa zimegawiwa na Mwenyekiti wa UWT(W) Buhigwe ambaye katika maelezo yake amethibitisha kukabidhiwa fedha hizo na Mhe. Mbunge ALBERT NTABALIBA OBAMA.
Uchunguzi wa tukio hili unaendelea, tutawasilisha taarifa ya matokeo ya uchunguzi mapema iwezekanavyo.
Naomba kuwasilisha tafadhali.
Stay tuned.
=======
Tukio hilo lilitokea Tarehe 07/07/2020 saa nane Mchana. Mbunge aliyemaliza muda wake Obama, alikuwa na kikao halali cha CCM.
Pamoja na kwamba hajatangaza nia ya kugombea Popote, TAKUKURU waliweza kujipenyeza kwenye kikao chake na Walimkuta anagawa elfu 10 kwa kila Mjumbe aliyehudhuria. (alikuwa hagawi yeye, alimpa mtu awagawie Wajumbe hapo Mkutanoni).
Walipomkagua wakakuta ana laki mbili na elfu kumi. Alikua kashagawa elfu kumi kumi kwa Wajumbe 21.
Obama alijitetea kwamba aliwachelewesha wajumbe kuondoka hivyo ilikua ni hela ya chakula cha Mchana kwa Wajumbe waliokuwa wapo mkutanoni tangu saa tatu asubuhi.
TAKUKURU wakawataka waliopokea hela warudishe na wakashikilia laki mbili na Elfu kumi zilizokuwa zinagawiwa kwa Uchunguzi.
Pia wakamtaka Obama kama ana hela yoyote aisalimishe, akasalimisha Milioni Mbili.
Baada ya hapo wakamruhusu aendelee na Vikao vyake kwenye vijiji mbalimbali kama ratiba yake inavyoonesha. Akimaliza atahojiwa..
Hata hivyo Kesho Tarehe kumi saa tatu asubuhi, TAKUKURU Kigoma, itatolea ufafanuzi wa kina swala hili.