Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,556
- 29,642
Kwa taarifa yakoKwa jinsi Dereva ' Bodaboda ' alivyokuwa kaumia vibaya Kichwani na Kuburuzwa nilishindwa Kujizuia na Kusikitika sana tu na kujikuta nakimbia (natoka Baru) eneo la Tukio kwa Kiwewe na kwenda 'Kuisikilizia' Ajali kwa mbali.
Najua (Huenda) Tukio lile lilishuhudiwa na mwana JamiiForums mwingine hivyo naomba asimulie hali nzima ilivyokuwa. Ni Ajali iliyotokea Goba Saa 1 Usiku wa leo Jumanne.
Jamani Wadogo zetu na Kaka zetu mnaoendesha hizi ' Bodaboda 'hasa' Kibiashara ' jioneeni Huruma jinsi mnavyokufa na kulemazwa hovyo kwa Ajali za Barabarani kwa Kuendesha kwa Nidhamu, kuwa Makini na kufuata sana Sheria. Taifa linawahitaji mno tu.
Bodaboda anapoondoka geto kwake ahsubuhi, huwa anaikunja roho yake vizuuri na kuiweka sandukuni kisha anatoka akiwa kiwiliwili kitupu.. Ndo maana wanatatarika barabarani kama kuku mwenye kideri aliyepakwa pilipili kunako makalio