Taswira
JF-Expert Member
- Sep 23, 2012
- 1,198
- 447
MTAALAM wa kutegemewa katika mifumo ya benki barani Afrika, Oran Njeza, ameteuliwa kuwa kamanda wa Jumuiya ya vijana wa CCM(UVCCM), wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani hapa.
Akizungumzia uteuzi huo, Njeza alisema kuwa ameupokea kwa furaha baada ya kurudi nyumbani nchini Tanzania na kujishughulisha na kilimo mkoani Mbeya.
Nimefanya kazi nchini nikianzia ofisi ya Waziri Mkuu, nikawa Mhadhili wa chuo cha SAUTI, nikaenda nchini Marekani katika masuala ya benki, Afrika kusini, Uingereza na nikaja kuifufua benki ya NMB ilipokuwa ikitakiwa kufufuliwa au kuuawa huku vitu vyote vizuri wakiwemo wafanyakazi wakipelekwa NBC alisema Njeza.
Alisema kazi yake kubwa kwa sasa ni kusaidiana na jamii katika maendeleo na alitakiwa awe kiongozi wa benki nchini Kenya lakini kwasababu yeye anapenda zaidi kilimo ameamua kujikita katika kazi hiyo.
Mwenyekiti wa UVCCM wilayani humo, Msafiri Mwashambwa, alimshukuru kamanda huyo kuupokea uteuzi huo ambao umepitia ngazi mbalimbali kuanzia ngazi ya wilaya, Mkoa mpaka Taifa.
Katibu wa jumuiya hiyo, Christina Hussein, alimwambia Njeza kuwa, ajiandae kuapishwa baada ya taratibu za mkoa kukamilika na baada ya hapo atafanyiwa sherehe kisha naye kuwaapisha makamanda wa UVCCM, wa kata za chama hicho.
Naye katibu msaidizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo, Kumotola Kumotola, alimwambia kamanda huyo kuwa, vijana wanategemea busara zake ili kusonga mbele.