VIKWAZO
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 1,899
- 580
Mahakama ya Rufani, imetengua adhabu ya kifo dhidi ya Evelina Ngatala mkazi wa mji mdogo wa Makambako Wilaya ya Njombe mkoani Iringa, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia mtoto mchanga wa siku tisa.
Ngatala, alipewa adhabu hiyo Disemba 18, 2007 baada ya Jaji aliyekuwa akisikiliza shauri hilo Frederick Werema, (Sasa Mwanasheria Mkuu wa Serikali) kumtia hatiani kwa kosa la kumuua mtoto huyo, akidaiwa kumpa sumu inayotumiwa kuulia wadudu kwenye mazao ya nafaka.
Ilidaiwa mahakamani hapo kwamba mshitakiwa huyo alisababisha kifo cha mtoto huyo baada ya kwenda kumtembelea nyumbani kwao, kisha kumshauri mama yake, wakae nje kwa madai kuwa ndani kulikuwa na joto.
Mbele ya jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa linaloongozwa na Jaji Euserbia Munuo iliendelea kudaiwa kuwa baada ya kutoka nje, mama wa mtoto huyo aliingia ndani kuchukua maji ya kunywa, lakini alipotoka tena nje, alishangaa kuona mshitakiwa akiwa amempakata mtoto huku povu likimtoka mdomoni mtoto huyo.
Ilielezwa kuwa mama wa mtoto huyo, alipoona mabadiliko ya mwanae, aliamua kupiga yowe jambo liliwakusanya watu na baadaye kwenda kwenye ofisi za kijiji, lakini wakiwa huko mtoto huyo alifariki.
Hata hivyo, ilidaiwa kuwa shahidi wa kimazingira, ulitumiwa na mahakama kuu ya Tanzania kumhukumu adhabu ya kifo, Eveline Ngatala kwa kusababisha kifo cha mtoto huyo kwamba haukidhi mahitaji kiasi cha kusababisha, mteja wake ahukumiwe kunyongwa hadi kufa.
Wakili aliyekuwa akimtetea mshitakiwa huyo, Onesmo Francis, aliiomba mahakama hiyo kumwondolea mteja wake huyo adhabu iliyohukumiwa kutokana na ushahidi wa kimazingira uliokuwepo kutokidhi mahitaji.
Wakili mwandamizi wa serikali, Andikalo Msabila, alikubaliana na upande wa utetezi, na kuiomba mahakama hiyo kutengua adhabu iliyotolewa kwa mrufani huyo.
CHANZO: NIPASHE
Ngatala, alipewa adhabu hiyo Disemba 18, 2007 baada ya Jaji aliyekuwa akisikiliza shauri hilo Frederick Werema, (Sasa Mwanasheria Mkuu wa Serikali) kumtia hatiani kwa kosa la kumuua mtoto huyo, akidaiwa kumpa sumu inayotumiwa kuulia wadudu kwenye mazao ya nafaka.
Ilidaiwa mahakamani hapo kwamba mshitakiwa huyo alisababisha kifo cha mtoto huyo baada ya kwenda kumtembelea nyumbani kwao, kisha kumshauri mama yake, wakae nje kwa madai kuwa ndani kulikuwa na joto.
Mbele ya jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa linaloongozwa na Jaji Euserbia Munuo iliendelea kudaiwa kuwa baada ya kutoka nje, mama wa mtoto huyo aliingia ndani kuchukua maji ya kunywa, lakini alipotoka tena nje, alishangaa kuona mshitakiwa akiwa amempakata mtoto huku povu likimtoka mdomoni mtoto huyo.
Ilielezwa kuwa mama wa mtoto huyo, alipoona mabadiliko ya mwanae, aliamua kupiga yowe jambo liliwakusanya watu na baadaye kwenda kwenye ofisi za kijiji, lakini wakiwa huko mtoto huyo alifariki.
Hata hivyo, ilidaiwa kuwa shahidi wa kimazingira, ulitumiwa na mahakama kuu ya Tanzania kumhukumu adhabu ya kifo, Eveline Ngatala kwa kusababisha kifo cha mtoto huyo kwamba haukidhi mahitaji kiasi cha kusababisha, mteja wake ahukumiwe kunyongwa hadi kufa.
Wakili aliyekuwa akimtetea mshitakiwa huyo, Onesmo Francis, aliiomba mahakama hiyo kumwondolea mteja wake huyo adhabu iliyohukumiwa kutokana na ushahidi wa kimazingira uliokuwepo kutokidhi mahitaji.
Wakili mwandamizi wa serikali, Andikalo Msabila, alikubaliana na upande wa utetezi, na kuiomba mahakama hiyo kutengua adhabu iliyotolewa kwa mrufani huyo.
CHANZO: NIPASHE