Aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa na Mwanasheria Mkuu (Werema) ashinda rufani

VIKWAZO

JF-Expert Member
Apr 9, 2011
1,899
580
Mahakama ya Rufani, imetengua adhabu ya kifo dhidi ya Evelina Ngatala mkazi wa mji mdogo wa Makambako Wilaya ya Njombe mkoani Iringa, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia mtoto mchanga wa siku tisa.

Ngatala, alipewa adhabu hiyo Disemba 18, 2007 baada ya Jaji aliyekuwa akisikiliza shauri hilo Frederick Werema, (Sasa Mwanasheria Mkuu wa Serikali) kumtia hatiani kwa kosa la kumuua mtoto huyo, akidaiwa kumpa sumu inayotumiwa kuulia wadudu kwenye mazao ya nafaka.

Ilidaiwa mahakamani hapo kwamba mshitakiwa huyo alisababisha kifo cha mtoto huyo baada ya kwenda kumtembelea nyumbani kwao, kisha kumshauri mama yake, wakae nje kwa madai kuwa ndani kulikuwa na joto.

Mbele ya jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa linaloongozwa na Jaji Euserbia Munuo iliendelea kudaiwa kuwa baada ya kutoka nje, mama wa mtoto huyo aliingia ndani kuchukua maji ya kunywa, lakini alipotoka tena nje, alishangaa kuona mshitakiwa akiwa amempakata mtoto huku povu likimtoka mdomoni mtoto huyo.

Ilielezwa kuwa mama wa mtoto huyo, alipoona mabadiliko ya mwanae, aliamua kupiga yowe jambo liliwakusanya watu na baadaye kwenda kwenye ofisi za kijiji, lakini wakiwa huko mtoto huyo alifariki.

Hata hivyo, ilidaiwa kuwa shahidi wa kimazingira, ulitumiwa na mahakama kuu ya Tanzania kumhukumu adhabu ya kifo, Eveline Ngatala kwa kusababisha kifo cha mtoto huyo kwamba haukidhi mahitaji kiasi cha kusababisha, mteja wake ahukumiwe kunyongwa hadi kufa.

Wakili aliyekuwa akimtetea mshitakiwa huyo, Onesmo Francis, aliiomba mahakama hiyo kumwondolea mteja wake huyo adhabu iliyohukumiwa kutokana na ushahidi wa kimazingira uliokuwepo kutokidhi mahitaji.

Wakili mwandamizi wa serikali, Andikalo Msabila, alikubaliana na upande wa utetezi, na kuiomba mahakama hiyo kutengua adhabu iliyotolewa kwa mrufani huyo.



CHANZO: NIPASHE
 
hicho ndicho kipimo tosha na ushahidi kuwa huyu bwana ndiyo maana alisema "KATIBA MPYA HAPANA"
 
mambo hayo......mara ya mwisho sheria ya kunyongwa ilitekelezwa lini?

wewe sawa hpja yako mkuu, unataka kusema nini? kwamba hii issue ya uongo au ilikuwa sawa huyo mtu kuhukumiwa kunyongwa maana hiyo sheria haitekelezwi?
kama unauliza mara ya mwisho ni lini jibu ni kwamba hiyo sheria ipo so uwezi kusema mara ya mwisho kutekelezwa sheria hipo
 
hicho ndicho kipimo tosha na ushahidi kuwa huyu bwana ndiyo maana alisema "KATIBA MPYA HAPANA"

wakichunguza kuna wengi aliwakatili kutoka na upeo wake wa kisheria
siju kwenye mikataba ya serikali inakuwaje huko
 
Tuliwahi kujiuliza huko nyuma kuwa jamaa huyu werema anaweza kuwa ametoa hukumu za utata kutokana na ufinyu wa akili zake
 
Tuliwahi kujiuliza huko nyuma kuwa jamaa huyu werema anaweza kuwa ametoa hukumu za utata kutokana na ufinyu wa akili zake

nadhani huyu jamaa hana huruma kesi zake zote alizosimamia zichunguzwa upya
 
Mahakama ya Rufani, imetengua adhabu ya kifo dhidi ya Evelina Ngatala mkazi wa mji mdogo wa Makambako Wilaya ya Njombe mkoani Iringa, ambaye alihukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia mtoto mchanga wa siku tisa.

Ngatala, alipewa adhabu hiyo Disemba 18, 2007 baada ya Jaji aliyekuwa akisikiliza shauri hilo Frederick Werema, (Sasa Mwanasheria Mkuu wa Serikali) kumtia hatiani kwa kosa la kumuua mtoto huyo, akidaiwa kumpa sumu inayotumiwa kuulia wadudu kwenye mazao ya nafaka.

Ilidaiwa mahakamani hapo kwamba mshitakiwa huyo alisababisha kifo cha mtoto huyo baada ya kwenda kumtembelea nyumbani kwao, kisha kumshauri mama yake, wakae nje kwa madai kuwa ndani kulikuwa na joto.

Mbele ya jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa linaloongozwa na Jaji Euserbia Munuo iliendelea kudaiwa kuwa baada ya kutoka nje, mama wa mtoto huyo aliingia ndani kuchukua maji ya kunywa, lakini alipotoka tena nje, alishangaa kuona mshitakiwa akiwa amempakata mtoto huku povu likimtoka mdomoni mtoto huyo.

Ilielezwa kuwa mama wa mtoto huyo, alipoona mabadiliko ya mwanae, aliamua kupiga yowe jambo liliwakusanya watu na baadaye kwenda kwenye ofisi za kijiji, lakini wakiwa huko mtoto huyo alifariki.

Hata hivyo, ilidaiwa kuwa shahidi wa kimazingira, ulitumiwa na mahakama kuu ya Tanzania kumhukumu adhabu ya kifo, Eveline Ngatala kwa kusababisha kifo cha mtoto huyo kwamba haukidhi mahitaji kiasi cha kusababisha, mteja wake ahukumiwe kunyongwa hadi kufa.

Wakili aliyekuwa akimtetea mshitakiwa huyo, Onesmo Francis, aliiomba mahakama hiyo kumwondolea mteja wake huyo adhabu iliyohukumiwa kutokana na ushahidi wa kimazingira uliokuwepo kutokidhi mahitaji.

Wakili mwandamizi wa serikali, Andikalo Msabila, alikubaliana na upande wa utetezi, na kuiomba mahakama hiyo kutengua adhabu iliyotolewa kwa mrufani huyo.



CHANZO: NIPASHE

Najaribu ku-imagine kama High court ingekuwa mahakama ya mwisho, huyu mama angelinyongwa bure!!!!!!!!!!!!!!!. Mwanasheria Mkuu sasa anatoa hukumu inatenguliwa, sijui, mimi sio mwanasheria lakini inatia shaka na weledi kwa ngazi aliyopewa sasa.
 
Najaribu ku-imagine kama High court ingekuwa mahakama ya mwisho, huyu mama angelinyongwa bure!!!!!!!!!!!!!!!. Mwanasheria Mkuu sasa anatoa hukumu inatenguliwa, sijui, mimi sio mwanasheria lakini inatia shaka na weledi kwa ngazi aliyopewa sasa.

mbona hii alisha prove kwenye shwala la KATIBA watu wanamuuliza maswali muhimu yeye anajibu wanaotaka katiba mpya ni wanaongea kama mabata

kwenye kulipa RICHMOND alisema fasta tu walipwe
juzi hapa bunge kabanwa na LISU nasema lisu ana tafuta umaarufu kuonekana kwenye TV matokeo yaka wakambana afute kauli na spika anakasema ndio ifute

kwa kifupi ni PROF KILAZA
 
Back
Top Bottom