Aliyedai kuwa mtoto wa Lowassa akamatwa na Polisi. Ni baada ya kuomba radhi

Shida IPO kwa yule mama mtu.Yeye ndiyo amemkosea mwanae.Na hata huyu FATUMA hapaswi kulaumuwa muongo yeye kaambiwa na mama mtu.Zinaa kina mama acheni mtaua watu bure.
 
Mbona ninachosikia kwenye video ni kuomba radhi kwa jinsi jambo lilivyo turn out kisiasa na kudhalilisha. Yeye anasema alienda kuomba msaada maana muda mrefu alikuwa akifuatilia. Hivyo hakusema alikuwa anadanganya. Ila anaona jambo lilivyosambazwa mitandaoni na kuzagaa inamkosesha amani. Sasa atashtakiwa kwa kosa gani?
 
Si mwenyewe amesema alikuwa anatumiwa na watu kisiasa? Hilo ni kosa la jinai inabidi akasaidie polisi kueleza waliyemtuma, hamtaki kama mzee amesingiziwa asafishwe kisheria na aadhibiwe kwa usumbufu aliotoa kwa Kumasi push madai ya uongo? Namshangaa Lema badala ya kushangilia mharifu kukamatwa, anatoa lawama
 
Kwa hyo pale kaomba msamaha gani? Mbona anasema yeye alitaka tu apate msaada baada ya kuzungushwa muda mrefu na hakutaka yawe makubwa!?

Kwa nni mlimfuatilia kumtia misukosuko mpaka kumteka akaombe msamaha chini ya upinzi!? Yeye anasema mligeuza suala lake la Kisiasa badala ya lengo lake la kutaka msaada wa babake.

Pale alipoombea msamaha palikuwa wapi na ni kwa nini yule binti hakuwa huru kama alivyotoa taarifa ya awali!?

Ni wapi amekanusha kwamba hahusiani na yule mzee wetu!? Na mbona hamkumtafuta na mamake akanushe!? Muogopeni Mungu!
Dah... unatumia nguvu nyingi sana kutetea ujinga huku ukitafuta huruma ya Mungu...
 
dada wa watu ameomba msamaha kabla bashite hajakamilisha mpango wake,maana ile juma mosi alipokuwa anongea TBC alimwambia LOWASSA asijaribu kupima uwezo wake kama mkuu wa mkoa.
Sasa bushmen aliekuja town na GARI za ng'ombe ataweza pambana na born town, ambao wako kwenye game tangu wakuja anachunga mbuzi bushi.
 
Si mwenyewe amesema alikuwa anatumiwa na watu kisiasa? Hilo ni kosa la jinai inabidi akasaidie polisi kueleza waliyemtuma, hamtaki kama mzee amesingiziwa asafishwe kisheria na aadhibiwe kwa usumbufu aliotoa kwa kuwasilisha madai ya uongo?
Hajasema kwamba alitumwa Kisiasa ila amesema suala lake limechukuliwa Kisiasa na Sasa Kuna watu wanamuandama mpaka anaiona Dunia chungu.

Kama wewe ni mchunguzi japo kidogo utagundua wanaomuandama ni wale waliotajwa sio wale waliopelekewa kesi.

Lazima uwe smart, maelezo yenyewe kayatoa chini ya usimamizi maalum( body language) hakuna inajieleza, sauti na video imeungwaungwa kisanii!
 
Huezi mchezea Lowasa rafu ukabaki salama! Le Commender ajiangalie sana!

References: Nape, kuna wazee hawaguswi kirahisi; Edo ni next level.
Kafika mjini zamani! We wa juzi tu hata babako alimkuta mjini ndo mana anawapa shida sana hamli mkashiba, hamuogi mkatakata.....

Acha izo mambo
 
Huezi mchezea Lowasa rafu ukabaki salama! Le Commender ajiangalie sana!

References: Nape, kuna wazee hawaguswi kirahisi; Edo ni next level.
Kafika mjini zamani! We wa juzi tu hata babako alimkuta mjini ndo mana anawapa shida sana hamli mkashiba, hamuogi mkatakata.....

Acha izo mambo
Angalao wwe umekuwa mkweli, unajua nn kinaendelea. Wengine ni oya oya tu. Mradi Lema kasema bhaaas!
 
Sasa matusi yametokea wapi? Endelea kutumia nguvu zako kushupalia ujinga wenzako tuko bize kujenga viwanda
Tuendelee kujenga Viwanda. Naamini siku inzi akiacha ujinga atatengeneza asali. Tujifikirishe japo kidogo.
 
Tuendelee kujenga Viwanda. Naamini siku inzi akiacha ujinga atatengeneza asali. Tujifikirishe japo kidogo.
Sawa lakini sio kwa ishu hizi za kitoto. Wanasiasa wanatuchezesha shere kwa vitu vya kijinga tunasahau kuelekeza nguvu zetu kwenye ishu za maendeleo.

Ndo kama hivi sasa lidada lina miaka 31 badala ya kutulia liolewe linahangaika kumtafuta baba. Afu watu wako bize kuhangaika kufuatilia huu ujinga...
 
Sawa lakini sio kwa ishu hizi za kitoto. Wanasiasa wanatuchezesha shere kwa vitu vya kijinga tunasahau kuelekeza nguvu zetu kwenye ishu za maendeleo.

Ndo kama hivi sasa lidada lina miaka 31 badala ya kutulia liolewe linahangaika kumtafuta baba. Afu watu wako bize kuhangaika kufuatilia huu ujinga...
Hahaha, statement yako ya mwisho imetengeneza siku yangu. Umeanza kuwa na akili. Tusipoteze focus kwa hoja za hawa watu. Tuchape kazi tukitazama mbele kwa ajili ya maendeleo ya Viwanda. Usiku mwema aisee!
 
Hajasema kwamba alitumwa Kisiasa ila amesema suala lake limechukuliwa Kisiasa na Sasa Kuna watu wanamuandama mpaka anaiona Dunia chungu.

Kama wewe ni mchunguzi japo kidogo utagundua wanaomuandama ni wale waliotajwa sio wale waliopelekewa kesi.

Lazima uwe smart, maelezo yenyewe kayatoa chini ya usimamizi maalum( body language) hakuna inajieleza, sauti na video imeungwaungwa kisanii!
Na hii ndio jibu kwa nini akina Lema wanalaumu kukamatwa kwa wanaoyedai katoa ushuhuda wa uongo juu ya bosi wao badala ya kushangilia. Kuwa wanajua walichofanya hata akalazimika kuomba radhi!!!
 
Back
Top Bottom