ALIYEANDAA FILAMU YA BEN ALIKOSEA KUWAPANGA WAIGIZAJI WAKE

Don san tan

JF-Expert Member
May 23, 2015
562
433
BEN alitoweka ktk kipindi ambacho alikuwa
akihoji uharali wa PhD ya Mh Magufuli.
Wajinga wachache walianzisha propaganda
mitabdaoni kujaribu kuhusisha kutoweka
kwake Ben na alichokuwa akikihoji ili
kumchafua Mh Rais na serikali yake. Lakini
mpaka sasa inaonyesha kabisa maji yako
shingoni maana wameanza kujikanyaga na
kuumbuana hadharani. Hivi leo hii hata
kama Ben atajitokeza akajaribu kupotosha
nani atakayemuamini mwanafunzi
anayesoma PhD anayejificha ili apate
umaarufu wa kisiasa?? Atatumia maneno
gani ya maigizo ili watu wamuamini?
Tujikumbushe hili suala hususani wamiliki
wa Gazeti la Mwanahalisi lililoropoka
majuzi kuhusu Ben kujificha ili apate
umaarufu.
i) Anthony Komu-Ni mmiliki mwenza wa
gazeti hili, huyu ni mbunge wa Chadema,
ni Mkurugenzi wa Fedha/Utawala wa
Chadema Makao makuu, pia ni mjumbe wa
kamati kuu ya CHADEMA, pia ni mjumbe
wa mkutano mkuu. Ben alikuwa chini ya
Kurugenzi hii ya fedha na utawala kama
sehemu ya mwajiri wake.
ii) Kubenea - Huyu ni mmiliki mwenza wa
gazeti la Mwanahalisi , ni Mbunge wa
Chadema pia ni mjumbe wa mkutano mkuu
wa Chadema
Habari ya Kubenea ktk Gazeti lao
imesema kuwa Ben yuko ktk vijiwe vya
kahawa, na kwamba amejificha ili kutafuta
umaarufu ili aweze kugombea nafasi ndani
ya chama mwakani.
iii) Mbowe - yeye alipohojiwa alisema kuwa
Ben ametekwa, na kwamba ukimya wake ni
kwasababu akiongea atahatarisha maisha
ya Ben maana watekaji wanaweza kumuua
Ben ikiwa Mbowe ataliongelea suala hilo.
Haoa inaonyesha dhahiri kuwa ulimi
ulitelwza na kusema mambo ambayo
hakutakiwa kuyasema au alisema maneno
ya muigizaji mwingine na kusahau maneno
yake aliyopaswa kuyasema.
# My_Take Inaonekana kabisa kuwa,
aliyeandaa scripts za hii movie/tamthilia
hakuwa makini sana ktk kuwagawia
uhusika wa nani aigize wapi, na aigize lini.
Yaani wamejikuta huyu anaongea maneno
ya huyu na huyu akiongea maneno ya
mwingine ktk movie moja. Sasa hivi naona
wamegeuza Gia Wanataka Ionekane Ben
Ndiye Mjinga Kwa Kujificha
Hali inavyoonekana, kuna wasiwasi
mkubwa kuwa Ben atageuzwa MBUZI wa
kafara ili boss aendelee kuonekana
Malaika. Naona Kubenea ameianza kazi
yake ipasavyo ya kusema kuwa Ben
amejificha ili kutafuta umaarufu.
Japo wanahaha kujaribu kubadili maana ya
ambacho tayari kimekwishasomwa na watu
ktk Gazeti la Mwanahalisi online. Lakini
njia pekee ya kukinusuru chama na
heshima ya Mbowe ni kumuangushia
jumba bovu kijana Ben, ili ionekane yeye
ndiye mjinga na msaka umaarufu kwa njia
za kijinga.

Magoiga SN-Mwanza
 
..labda Ben amewekwa kule wanakopaita " mahali salama." Sasa wanatafuta njia ya kumtoa.
 
hawa jamaa hawafai ata kwa mkopo make huwa wanapenda sana siasa za matukio by the way hamma mwanaufipa wa kumuhoji Dj.
 
hawa jamaa hawafai ata kwa mkopo make huwa wanapenda sana siasa za matukio by the way hamma mwanaufipa wa kumuhoji Dj.

Jaman tuje kuongea yote tuwezayo akipatikana mtanzania mwenzetu, sisi binadam hatujui kilichompata hiz zote hisia tu. Je zikiwa tofaut na uhalisia tutaweka wap sura zetu
 
Back
Top Bottom