Kuna Mnamibia tulikuwa nae kwenye kozi ya miezi 6 America ya kusini baada ya kurudi nyumbani kanipigia simu mkewe ana mimba ya mtu mwingine ya miezi 5.Jamaa kachanganyikiwa anadai mkewe alitoka na rafiki zake wa kike wakaenda disco kitu ambacho alikuwa anafanya mara moja moja hata mumewe akiwepo[ladies nightout].Siku hiyo wenzake walikuwa wakicheza akaja mwanaume aliyeonekana msaarabu na kuomba kukaa naye,baada ya maongezi ya kawaida jamaa akaamka kufata kinywaji na kuomba kumletea na yeye.Baada ya kunywa kinywaji hakumbuki kilichotokea akajikuta kwenye chumba cha hoteli akiwa uchi asubuhi ya pili huku akiwa peke yake.Aliporudi nyumbani na kuwapigia simu rafiki zake wakamwambia hata wao walishangaa alivyoondoka gafla wakadhani hakujisikia vizuri na kurudi nyumbani.Alipima ukimwi na kujikuta salama lakini kuhusu mimba alitaka mumewe arudi waamue la kufanya.Hajaripoti polisi kwakuwa hamjui jamaa aliyembaka.
Rafiki yangu anadai anampenda sana mkewe na angeweza kutoa mimba bila ya yeye kujua na muda pia ungeruhusu.Yuko njia panda kuhusu kulea mtoto wa mtu huko wenyewe hawana mtoto.Nimshaurije?
Rafiki yangu anadai anampenda sana mkewe na angeweza kutoa mimba bila ya yeye kujua na muda pia ungeruhusu.Yuko njia panda kuhusu kulea mtoto wa mtu huko wenyewe hawana mtoto.Nimshaurije?