Alipokuwa hana kazi aliniheshimu, saivi kapata kazi haniheshimu

Wazabanga kuku

JF-Expert Member
Dec 13, 2016
264
378
Nipo kwenye mahusiano na mwanamke ambae wakati nadate nae hakuwa na kazi na alikua na heshima sana, simu anapiga meseji anatuma na tuna mtoto mmoja lakini kapata kazi basi suala la kupiga simu kwangu ni gumu.

Mimi ndo nahangaika daily kumtafuta mbaya zaidi nikipiga simu kwa ndugu zake nisipoanza kuwasalimia wanamwambia dada yao na anakuja na maneno kibao ya kejeli, sasa bado sijafunga nae ndoa lakini keshaanza nongwa NIFANYAJE JAMANI?
 
Piga chini, kuanza upya sio ujinga. Ukimwoa atakufanyia makubwa zaid ya hayo.
 
ACHA MASIHARA MKUU! moyo unapenda! ila haufungwi kwa kuwa fikra zinafanya kazi "Huwezi Kuuona Umuhimu Wa Mtu, Hadi Atakapokosekana Katika Jambo Flani Linalokuhusu" achana na neno NAMPENDA SANA NASHINDWA KUMUACHA, hizo ni fikra za walianza kubalehe, Selemani Msindi anasema "Aliwazalo Mjinga, Ndo Linalomtokea"
 
Sasa we unataka jibu gani hapo tabia ya MTU apate Pesa, umeenda sokoni unakuta nyanya kibao bado unahangaika na iliyooza,pana njia Mbili piga chini,au kuwa na hela zaid yake zaidi ya hapo kubali kuteseka km vile ulikuja duniani kuteswa na mapenzi,kuwa neutral sababu binadamu ni dynamic wanabadilika badilika Leo mzuri kesho mbaya na kinyume chake.
 
Nipo kwenye mahusiano na mwanamke ambae wakati nadate nae hakuwa na kazi na alikua na heshima sana, simu anapiga meseji anatuma na tuna mtoto mmoja lakini kapata kazi basi suala la kupiga simu kwangu ni gumu.

Mimi ndo nahangaika daily kumtafuta mbaya zaidi nikipiga simu kwa ndugu zake nisipoanza kuwasalimia wanamwambia dada yao na anakuja na maneno kibao ya kejeli, sasa bado sijafunga nae ndoa lakini keshaanza nongwa NIFANYAJE JAMANI?
JF kuna mambo, tatizo la weza kuwa wewe huelewi, kazi unayo long, kilichokufanya husioe nini?
 
Kuna mada humu inatembea kuhusu wanaume kuogopa wanawake waliowazidi kipato nadhani huu ni ushahidi wa wazi,sasa huyo kapata kazi kashakua mbogo,je ukimkuta mwenye kazi yake na anapesa itakuaje?
Mkuu piga chini tafuta mwingine anza upya ukichekacheka atakuja kukunyorosha ww
 
Yani umeshamzalisha unahangaika nae upate kipi tena? Mkuu ebu amka usingizini na piga chini chini kabisa Ingekuwa mimi mtu nimemzalisha azingue kwanza ntaenda bar na kuzungusha bia kujipongeza , Watoto wa bichi wote hao wake up, au ww ndo wale mlioanza kula K mwaka wa tatu chuoni?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom