kindikinyer leborosier
JF-Expert Member
- Jan 6, 2018
- 430
- 780
Habari wanajamii?
Poleni na majukumu ya week nzima!
Niende moja kwa moja kwenye uzi husika, mwaka 2013 nilianza mahusiano na binti mmoja ambae familia yao ilikua karibu sana na familia yetu.
Tulidumu kwenye mahusiano kwa muda kidogo mpaka 2017 ambapo tuliamua kuachana, sababu kubwa ikiwa yeye alikua akiwa na mahusiano mengine chuoni kwao, kwa siri. nilivyokuja kusikia nilichukua maamuzi hayo japo kweli nilikua nikimpenda sana.
Kwenye mihangaiko ya maisha nilikuja kuishi Mwanza, siku moja aliniambia anarudi kwao Musoma anataka kunipitia, nilimkaribisha, japo sikumleta kwangu, tuliishia kwa hotel.
Alikua na mambo mengi sana ya pride mara hiki mara kile, mara ampigie simu mwanaume alienae hivyo, nilikausha tuu, mwisho nilimwaga kama saa 2 usiku!
Juzi aliniandikia txt anaolewa, sikujali nikamjibu nitampa mchango wangu, nikatulia, jana amenitafuta ananiomba anatoka Dsm kwa mchumba wake, anataka afikie kwangu napoishi afanye manunuzi kabla ya kurudi Musoma.
Mwanzo nilikubali ila baadae niliwaza nikaona si busara, kwa sababu hizi:
1. Mahusiano yetu yalikua yakifahamika mpaka nyumbani kwetu.
2. Tabia zake za awali za majivuno na pride
Alikuja kugundua namwepuka kwani nilimwambia na ziara ya kikazi nje ya mkoa.
Alilalamika sana, na kusema kila mtu anajua yeye anaenda kuolewa hata kwetu, hivyo mimi kumkatalia nilifanya vibaya kwani hata wadogo zangu wanaweza kupata hifadhi siku moja kutoka kwake.
Asanteni wadau, Je nilikosea kumkatalia.
Natanguliza samahani endapo uandishi wangu haujakaa sawa!
Poleni na majukumu ya week nzima!
Niende moja kwa moja kwenye uzi husika, mwaka 2013 nilianza mahusiano na binti mmoja ambae familia yao ilikua karibu sana na familia yetu.
Tulidumu kwenye mahusiano kwa muda kidogo mpaka 2017 ambapo tuliamua kuachana, sababu kubwa ikiwa yeye alikua akiwa na mahusiano mengine chuoni kwao, kwa siri. nilivyokuja kusikia nilichukua maamuzi hayo japo kweli nilikua nikimpenda sana.
Kwenye mihangaiko ya maisha nilikuja kuishi Mwanza, siku moja aliniambia anarudi kwao Musoma anataka kunipitia, nilimkaribisha, japo sikumleta kwangu, tuliishia kwa hotel.
Alikua na mambo mengi sana ya pride mara hiki mara kile, mara ampigie simu mwanaume alienae hivyo, nilikausha tuu, mwisho nilimwaga kama saa 2 usiku!
Juzi aliniandikia txt anaolewa, sikujali nikamjibu nitampa mchango wangu, nikatulia, jana amenitafuta ananiomba anatoka Dsm kwa mchumba wake, anataka afikie kwangu napoishi afanye manunuzi kabla ya kurudi Musoma.
Mwanzo nilikubali ila baadae niliwaza nikaona si busara, kwa sababu hizi:
1. Mahusiano yetu yalikua yakifahamika mpaka nyumbani kwetu.
2. Tabia zake za awali za majivuno na pride
Alikuja kugundua namwepuka kwani nilimwambia na ziara ya kikazi nje ya mkoa.
Alilalamika sana, na kusema kila mtu anajua yeye anaenda kuolewa hata kwetu, hivyo mimi kumkatalia nilifanya vibaya kwani hata wadogo zangu wanaweza kupata hifadhi siku moja kutoka kwake.
Asanteni wadau, Je nilikosea kumkatalia.
Natanguliza samahani endapo uandishi wangu haujakaa sawa!