Alikuwa rafiki, tukagombania bwana, sasa kaka yake anataka kunioa!

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,587
215,181
Mimi na huyu dada tulisoma wote primary, baada ya hapo secondary kila mtu akatimkia kivyake, tulikutana chuoni tukiwa in early 20's. Yeye alikuwa na bwana lakini sikuwahi kumfahamu, ilitokea siku moja nilikwenda kukata ticket nisafiri, yule kijana kumbe aliniona akamuomba mkata ticket kwa gharama yeyote nipe kiti pembeni ya yule dada, sikujua muuza ticket alifika dau au la, lakini nilikaa kiti kimoja na yule kaka. Wakati ule barabara zilikuwa mbovu sana, ile safari ilichukua massa 8. Tulifika usiku, wakati ule hakukuwa na mobile phones, so yule kaka alichukua taxi akahakikisha inanifikisha mimi kwanza ndiyo yeye aendelee na safari.

Kwa kifupi muda wote ule nilishamwambia ninasoma chuo gani ninafanya nin. Basi kaka akaanza trip za kuja chuoni na vijizawadi. Yule dada akagundua lo, urafiki ulikwisha, inilijaribu kumueleza kuwa sikufahamu uhusiano wao. Yule jamaa alinionyesha barua aliyoiandika yule dada kwake, 'unaniacha mimi cheupe dawa kwaajili ya yule gorilla', any way, ninajua hakutakiwa kunionyesha ile barua.

Miaka mingi imepita sasa, nimekutana na kaka yake ambae wakati tuko primary yeyey alikuwa mbele yetu sana, tumeanza ku date, na inaonyesha is heading to a serious relationship, kaka amenifahamisha dada yake amekuja kumsalimia niende, nimefika dada ananibenulia midomo, jamaa amenotice hiyo, alichoniambia amesema I've to make an effort to talk to his sister because I mean so much to him. Ninaomba ushauri.
 
HAHAHAAAAAAAAAAAAAAA!!!!!!!!!!!! @ Gorilla! Mambo ya G U NOT!!!!!!!! You made my evening CHEUPE V GORILLA!!!!!!!!!

Back to topic!

Usijipe stress wewe! Wifi bongoooo!!!!!!!!!!! Wifi ilikua zamani sio sasa! Kama ana uchungu sanaa aolewe yeye basi na huyo kaka yake!

Wewe hapo ndo umeshika hatamu na bank account zote ukijitahidi kwenye uwanja wa fundi seremala, There is nothing between you and the wife title! JST IGNORE HER!!!!!!! Toka lini tembo akawaza barabarani kuna visisimizi? Ukimuignore ata learn to accept the reality kuwa wewe ndo maza house originale!!!!!!!!

Mwenyewe viwifi uchumba hivi huwaga navinyali nyali, sio kwa kuwa navionea wivu au kijiba ila navihurumia kujikukurusha na kujikomba komba wakati yeye wifi wa 20 labda mimi kutambulishwa! Sasa inakuwa i spare myself the sentiments!!!!!!!!!
 
Kama umemwambia story yote huyo mchumba wako then ni jukumu la huyo bwana kuwapatanisha! sasa kati yenu wawili - wewe na dada yake (kama nyie mmeshindwa kupatana), yule ambaye hatofunguka kuongea na mwenzake basi ahesabiwe kama mtu wa mataifa!
 
Dah! This is like a movie. Kweli dunia mzunguko. Aisee hapo kikubwa ni uimara wa uhusiano wako wewe na huyo kaka yake. Kama uhusiano wenu ni imara kiasi cha kutosha, huyo dada yake hawezi kuwatenganisha. Jaribu kuongea nae uone atakujibu nini! Lakini, yote kwa youte, huyo mchumba wako mtarajiwa na wewe ndio wenye maamuzi ya mwisho!

By the way, yaliyopita si ndwele ila ningependa kujua. Je mkiwa huko chuo, yule kaka aliyefanya mpaka mkagombana, ulimkubalia kuwa na uhusiano nae wa kimapenzi?
 
Saafi hii muvi Tami, Paloma njoo utupe uzoefu Wako juu ya like zali lako. Maybe itasaidia kuokoa huu uchumba maana huyu Mpwa wangu kaombewa makanisa tote ili ampate Mume.....halafu vizingiti ndio vinaanza mchana hivi
 
Last edited by a moderator:
kijana si unampenda ya nini kujipa pressure.
you cant please everybody in this world.....
no turning back,move forwaad my dear,you just cant loose the chance cos of some people!!!!!!!
 
Dah! This is like a movie. Kweli dunia mzunguko. Aisee hapo kikubwa ni uimara wa uhusiano wako wewe na huyo kaka yake. Kama uhusiano wenu ni imara kiasi cha kutosha, huyo dada yake hawezi kuwatenganisha. Jaribu kuongea nae uone atakujibu nini! Lakini, yote kwa youte, huyo mchumba wako mtarajiwa na wewe ndio wenye maamuzi ya mwisho!

By the way, yaliyopita si ndwele ila ningependa kujua. Je mkiwa huko chuo, yule kaka aliyefanya mpaka mkagombana, ulimkubalia kuwa na uhusiano nae wa kimapenzi?

Zile zilikuwa za utoto hata ku do na mwanaume unaogopa, sana sana kakutoa movie, Avalon, unapata denda alafu unarudi choni.
 
Umenikumbusha story fulani. Kuna dada mmoja alikua family friend,
Na kulikua na kaka mmoja alikua ananitongoza. Nilimkataa, akadate huyo family friend
vyao vikaisha after a few month, but mimi na yule kaka tukaendelea kua marafiki
hivi leo ni almost 7 years later mi na yule kaka still tupo marafiki, yule dada kaolewa
Hapa majuzi nilikua somewhere na huyo kaka tunapunga hewa, mara dada akapita
You won't believe it, kanitangaza eti nimemwibia mpenzi wake. :shock:
Yeye kaolewa, mimi na huyo kaka hatujawahi kua (na hatuwezi tena)
Nashangaa vitu vya zamani, seven years ago, anataka kuvileta leo
The guy wasn't man enough for me then, leo nimekua ndio nimpende?
Na hata nikimpenda yeye yanamuhusu nini maana she is married tayari?

Haya turudi kwenye mada: Kama kweli huyo kaka ana-insist mwambie
akae na dada yake na amshahurie: she should appologize to you. basi!
 
Bonge la movie, ukizingatia mama yao alikuwa mwalimu wetu primary, kila nikumuona ninamsalimia 'shikamoo mwalimu' sasa inaelekea atakuwa 'mama mkwe'.
 
Zile zilikuwa za utoto hata ku do na mwanaume unaogopa, sana sana kakutoa movie, Avalon, unapata denda alafu unarudi choni.

Okay! Cha msingi ni msimamo wenu, yaani wewe na huyo kaka yake na 'shosti wako wa zamani'.

Halafu lazima mtakuwa watu wazima sana, maana mlikuwa chuo enzi za ''hakuna mobile phones, na outing ilikuwa kwenda Avalon Cinema''. Busara zenu na zitawale swala hili ili nifikie mwisho wenye mafanikia mnayoyatarajia!
 
acha na huyo dada c lolote si chochote, ww cha msingi focus on hw to strengthern ua reletionship mpaka ndoa, acha na hao mawifi ushuz
Watu wengine bhanaaaaaaaaaaa arrrrrrggggghhhhhh
 
Okay! Cha msingi ni msimamo wenu, yaani wewe na huyo kaka yake na 'shosti wako wa zamani'.

Halafu lazima mtakuwa watu wazima sana, maana mlikuwa chuo enzi za ''hakuna mobile phones, na outing ilikuwa kwenda Avalon Cinema''. Busara zenu na zitawale swala hili ili nifikie mwisho wenye mafanikia mnayoyatarajia!

Time flies my dea, yaap, hakukuwa na mobile phones lakini chuoni tulikuwa na chumba cha kupokelea simu, ilikuwa karibu na office ya mkuu wa chuo, ukipigiwa unaitwa. Kupata barua ilikuwa dili.
 
huyo nae wifi yako inakuwaje hadi leo anatunza hasira za utotoni?
 
Mimi na huyu dada tulisoma wote primary, baada ya hapo secondary kila mtu akatimkia kivyake, tulikutana chuoni tukiwa in early 20's. Yeye alikuwa na bwana lakini sikuwahi kumfahamu, ilitokea siku moja nilikwenda kukata ticket nisafiri, yule kijana kumbe aliniona akamuomba mkata ticket kwa gharama yeyote nipe kiti pembeni ya yule dada, sikujua muuza ticket alifika dau au la, lakini nilikaa kiti kimoja na yule kaka. Wakati ule barabara zilikuwa mbovu sana, ile safari ilichukua massa 8. Tulifika usiku, wakati ule hakukuwa na mobile phones, so yule kaka alichukua taxi akahakikisha inanifikisha mimi kwanza ndiyo yeye aendelee na safari.

Kwa kifupi muda wote ule nilishamwambia ninasoma chuo gani ninafanya nin. Basi kaka akaanza trip za kuja chuoni na vijizawadi. Yule dada akagundua lo, urafiki ulikwisha, inilijaribu kumueleza kuwa sikufahamu uhusiano wao. Yule jamaa alinionyesha barua aliyoiandika yule dada kwake, 'unaniacha mimi cheupe dawa kwaajili ya yule gorilla', any way, ninajua hakutakiwa kunionyesha ile barua.

Miaka mingi imepita sasa, nimekutana na kaka yake ambae wakati tuko primary yeyey alikuwa mbele yetu sana, tumeanza ku date, na inaonyesha is heading to a serious relationship, kaka amenifahamisha dada yake amekuja kumsalimia niende, nimefika dada ananibenulia midomo, jamaa amenotice hiyo, alichoniambia amesema I've to make an effort to talk to his sister because I mean so much to him. Ninaomba ushauri.
Hiyo 'K'imeshakua used kishenzi lol!!
 
Love conquers all my dear kama kweli una penzi la dhati na zito kwa huyo kaka mtu, tafuta suluhu na wifi yako. Mwambie ilikuwa utoto tu muyamalize. Kama vipi jilipue kwa mpenzio mweleze ukweli asipokuelewa it wasn't meant to be. Ni bora ukaachika kwa kusema ukweli kuliko kuuficha ukaja julikana baadae.
 
HAHAHAAAAAAAAAAAAAAA!!!!!!!!!!!! @ Gorilla! Mambo ya G U NOT!!!!!!!! You made my evening CHEUPE V GORILLA!!!!!!!!!

Back to topic!

Usijipe stress wewe! Wifi bongoooo!!!!!!!!!!! Wifi ilikua zamani sio sasa! Kama ana uchungu sanaa aolewe yeye basi na huyo kaka yake!

Wewe hapo ndo umeshika hatamu na bank account zote ukijitahidi kwenye uwanja wa fundi seremala, There is nothing between you and the wife title! JST IGNORE HER!!!!!!! Toka lini tembo akawaza barabarani kuna visisimizi? Ukimuignore ata learn to accept the reality kuwa wewe ndo maza house originale!!!!!!!!

Mwenyewe viwifi uchumba hivi huwaga navinyali nyali, sio kwa kuwa navionea wivu au kijiba ila navihurumia kujikukurusha na kujikomba komba wakati yeye wifi wa 20 labda mimi kutambulishwa! Sasa inakuwa i spare myself the sentiments!!!!!!!!!

Duuu! Hayo maneno simchezo mtu anaweza kujpiga ktanz akiyaona
 
Love conquers all my dear kama kweli una penzi la dhati na zito kwa huyo kaka mtu, tafuta suluhu na wifi yako. Mwambie ilikuwa utoto tu muyamalize. Kama vipi jilipue kwa mpenzio mweleze ukweli asipokuelewa it wasn't meant to be. Ni bora ukaachika kwa kusema ukweli kuliko kuuficha ukaja julikana baadae.

Asante sana. Unajua mahusiano ya sasa hivi ni kuwa tu unahitaji company, si ile ya kuwa akiniacha nitafanya nini jamaini. Yeye ana career na mimi vile vile.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom