Alifumaniwa, akavuliwa nguo

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,315
33,109

Na Mwandishi Wetu

Sakata la mchekeshaji mwenye uwezo mkubwa nchini kulawitiwa, sasa linaweza kuchambuliwa na Risasi Jumamosi baada ya kupata ÔdataÕ za uhakika kutoka kwa vyanzo vyake...
Hata hivyo, busara imechukua nafasi yake kuendelea kuhifadhi jina la msanii huyo ambaye ishu yake ya kufanyiwa mchezo wa Mombasa ipo dhahiri mitaani na inanongÕonwa na wengi.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, msanii huyo anayefunika zaidi anapovaa uhusika wa kike kazini, alifanyiwa tendo hilo la kikatili, baada ya kutegwa na baadaye kufumaniwa akila ÔurojoÕ na mke wa mtu feki.

Habari zinasema kuwa ÔdogoÕ huyo anayehesabiwa kama nyota kwenye kundi lake kutokana na uwezo wake wa kuchekesha, ÔalidakwaÕ kisha kufanyiwa mchezo huo mbaya, Mburahati, Dar es Salaam.

Ilielezwa kuwa, mchekeshaji huyo ambaye ni mfupi, mwembamba kwa wajihi, alitendwa ÔumombasaÕ na watu ambao wana kisasi naye .

Risasi lina majina ya wabaya wa mchekeshaji huyo, ingawa linayaweka ÔpendingÕ kwa sasa mpaka hapo baadaye litakapoamua vinginevyo.

Watu ambao wametajwa kumfanyia unyama dogo huyo ni wawili, mmoja ni nyota wa zamani wa soka, wakati mwenzake ni mwanamuziki wa dansi mwenye jina kubwa nchini.

Ilielezwa na vyanzo vyetu kuwa, watu hao wawili walikutana na kupanga ÔoparesheniÕ ya kumfanyia kitu kibaya dogo huyo kama njia yao ya kumshikisha adabu.

ÒWalikutana na kupanga mbinu zao, kwahiyo wakaona adhabu ambayo inamfaa ni kumpeleka Mombasa, kwahiyo walikodi watu ambao walitekeleza oparesheni hiyo ya kinyama.

ÒWatu ambao walikodiwa, walimuandaa mwanamke ambaye alianza kumtega Ôbwa mdogoÕ kimapenzi mpaka alipoingilika, wakakubaliana kuingia chumbani ambako maharamia waliokodiwa walivamia.

ÒBahati nzuri walimkuta amevaa, lakini wale maharamia walianza kumpiga na kumhoji ni kwanini anachukua wake za watu, baadaye walimvua nguo na kumtendea unyama huo,Ó alisema mtoa habari wetu.
Chanzo chetu kiliendelea: ÒWalimfanyia unyama huo na kumuumiza vibaya, baadaye wakamuonya aache kufuatilia mambo ya watu na kujiepusha na wake za watu.

Habari zaidi zinasema kuwa baada ya kufanyiwa unyama huo na ÔrumazÕ kutawala kila pembe ya nchi, uongozi wa televisheni inayorusha kipindi cha kundi lake, ulimwita na kumuuliza lakini alikanusha na kudai kwamba anazushiwa na wasanii wenzake.

ÒUongozi ulimuuliza akakanusha, wasanii wenzake wakimuuliza anakuwa mbogo, lakini ukweli ni kuwa ndugu yetu amefanyiwa kitu kibaya,Ó alisema mtoa habari wetu.
Global Publishers - Tanzania Newspapers
 
Angalia live yaliyokuwa yakitabiriwa. Mara nyingi wasanii hutabiri matukiao mabaya yote yatakayowakuta. Kwani hawajui kinywa huumba. Watch it [ame=http://www.youtube.com/watch?v=H4ujP_3pcK8&feature=related]YouTube - Ze Comedy - Mzee Wa Sumbawanga.[/ame]
 
Back
Top Bottom