Alichonifanyia rafiki yangu namuachia Mungu

Tajiri Tanzanite

JF-Expert Member
Oct 23, 2016
2,061
3,682
Wasaalam wadau!
Nimeona niliweke wazi hili swala ili niweze kupata mtazamo na ushauri wa wadau.

Ni hivi nilipomaliza degree yangu mwaka jana katika chuo fulani nilikutana na msichana mmoja mrembo siku mbili baada ya kumaliza mtihani wangu wa mwisho.

Mazingira ya kukutana yalikuwa hivi.
Nilikuwa na marafiki zangu watatu tunarudi zetu mageto baada yakupa mvingo kusherekea kumaliza chuo

Tulipo fika mazingira ya chuo tukakutana na mdada mzuri akatuchangamkia vizuri but alituchangamkia coz alikuwa anafahamiana na mmoja wetu,kutokana na mvingo ushapata kichwani nikamuhag nae akarespond kwa bashasha,hapo hapo nikamuomba mawasilia mtoto akatoa number.
Nikafika geto nikamtumia sms,akarespond faster akaongeza na maneno mengine,nikajisemea moyo"mtoto kashaelewa nataka nn''anyway hapo hapo nikaamua kumvutia waya akapokea then nikapiga nae story mbili tatu,nikaomba appointment ya siku inayofuata akakubali.

Siku iliyofuata nikakutanae somewhere tukawa tunakunywa vinywaji vya kawaida na tukipiga story za kawaida,baada yahapo nikamrudisha kwake alikuwa amepange na anaishi mwenyewe.Baada ya kufika kwake tukaendeleza story za kawaida tu, huku usiku ukizi kuingia nikaanza kubadisha mada taratibu nikamtupia mistari ya kiutu uzima,mara mtoto akanielewa nikala mzigo mpaka asubuhi.
Mtoto akaniambia wiki mbili nyuma alikuwa katika mfungo na maombi ya kumuomba Mungu Mume akishirikiana na Mchungaji mmoja aitwae Fred yupo Moro,akasema baada ya maombi aliambiwa na mchungaji wiki hiyo atakutana na mwanaume wake,akaniambia ndio maana amekuwa mrahisi kuniachia mzigo.

Na Mimi moyo nikasema kama nikweli Huyu lazima nimuoe,niliamua kuarisha safari ya kurudi Arusha Siku iliyofuata japo nilikata tiketi,nikaongeza wiki nikaendelea kula mzigo.

Kweli wiki hiyo hiyo mchungaji akampigia cmu,wakaanza kuongea then mchungaji akaanza kumuombea kama kawaida yao.

Then mtoto akaniambia kabla sijaenda Arusha niongee na mchungaji,nikamuambia hamna shida,kweli akampigia cmu mchungaji nikaongea nae,mchungaji akanieleza kama vile x-wangu alivyo nieleza.

Baada ya wiki moja,mm nikarudi zangu Arusha nikamuacha chuo akiandika proposal ya research na wezao na wakisha maliza proposal wataenda kufanya research na field kwa miezi 6.

But mm nikamuahidi nitamtafutia field Arusha so,akishamaliza kuandika proposal aje moja kwa moja Arusha,nilipo fika Arusha kweli nikamtafutia field.
Kutoka chuoni kuja mjini kukata tiketi yakuja Arusha niliona atapata usumbufu fulani hivi,nikaona nimpigie rafiki yangu
Cmu amsaidie huo mchakato

Huyu rafiki yangu nilikutana nae Arusha wakati nafanya field japo kichuo ni majirani yeye alikuwa anasoma Ruaha University na mm Tumaini Unversity ya Iringa
,nilijua ni mtu wa Arusha kama mm but kumbe in MTU wa Tanga

X-wangu aliweza kufika Arusha nikampokea vizuri,then baada ya siku mbili akaanza field.kutoka na maisha yakaendelea vizuri,kiukweli alikuwa nimwananke aliyejinasibu kwa Tabia yakipekee kwasababu alikuwa ni MTU was maombi kila Mara,kiasi kwamba hata tukiwa hotel,au tumekaa sehemu kama bar au pub tunakula msosi lazima ashushe maombi.

Usiku kabla ya kulala baada ya kuamka,kabla ya kula lazima maombi,jumapili lazima niburutwe kanisani,so kwa tabia take nilianza kumtamvulisha mdogo mdogo mdogo home.

Kiasi kwamba akawa na wivu kupitiliza nikilalaa usiku,anchukua CMU yangu anaanza kuwatukana wasichana ambao huwa nakuwa nao karibu katika mawasiliano,na hao wasichane nilishamueleza mapema nikamuambia hawa nimarafi zangu wa muda mrefu na nimawasiliano ya kawaida tu.

Tafauti imeanzia hapa!
Kwanza alifikia mahali akawa haoni siku zake, tukaenda kupima akakutwa ana mimba ya mwezi na wiki kazaaa,nikamuambia ongera Hanna shida nikotayari kukabiliana na majukumu..lakini akili ikaja tokea nilipo kutana nae nikadate nae mpaka ule muda wa kupima tukaesabu siku tunawiki tatu tu,so mimba kuwa na mwezi mmoja na wiki kadhaa ikatuchanganya wote wawili.

Nikamuambia asijali inaezakuwa yule mama alikadiria vibaya,so ikabidi tukapanga siku tukaenda utrasound,baada hiki kipimo ikaonyesha hivyo hivyo,means mimba imeingia wiki3 tatu nyuma kabla ya mm kusex nae.

Nikamuambia asijali asubiri mtoto akizaliwa tutampima DNA.


From there mwezangu akaanza kupoteza amani,tabia ikaanza kubadilika kiasi kwa anakuja kwangu saa mbili usiku na sio kawaida yake,na pale wanapofanyia field ofice inafungwa saa 10 jioni,nikimuuliza ananiambia alikuwa kwenye kikao.
Basi siku nyingine akachelewa mpaka saa moja na nusu nampigia ananiambia alikuwa kwenye kikao then ikabidi nikasema ngoja nikazibitishe nikaenda mpaka ofice kwao nafika pale nampigia cmu ananiambie yupo kwenye kikao wakati ofice nayona imefungwa

Nikarudi home nikaa nikamsubiri baaada ya Lisaa na nusu akaja inaelekea SAA tatu usiku,and nilikuwa nimekasirika kweli nikamuuliza mbona umenidanganya akanijibu ovyo ovyo nikamtia kelebu.

Tukagombana sana kwa maneno then tukalala usiku nikamuomba tuyasahau hayo nikambembeleza sana,lakini mwenzangu kuwa tayari kuyamaliza ilikuwa ngumu.

Anyway pakakucha nikaenda kazini of course nilipata somewhere pa kujishikiza kimtindi kipindi kile,then nilipo rudi nyumbani saa 10,nikakuta mwenzangu katimua ameacha ufunguo kwa jirani,dah!kiukwel niliumia sana anyway sijaangaika kumtafuta nikasema acha niendelee na maisha.

Sasa nikaanza kujiuliza maswali yasiyokuwa na majibu,hivi huyu x-wangu ni mgeni hapa mjini na ajamaliza field inakuaje aondoke kirahisi hivi.Nikatulia kimya sijamtafuta tena.

Nikaendelea kutafita maisha baada ya mienzi mitatu,nikaenda Iringa kufuatilia vyeti vyangu katika kuzunguka zunguka nikakutana nae anaingia class nikamsalimia nikamuahidi nitamtafuta tuongee,japo hakuwa na dalili ya mimba inavyoenekana kashaitoa.
Jioni nikampigia cmu,hakupokea
Ikabidi nimpotezee n,then baada ya kukaa wiki nikarudi zangu Arusha,japo sijafanikiwa kuchukua vyeti.

Nikaja Arusha nikaa miezi 6,baada ya hapo nikaona ngoja nirudi Iringa nikawa nawasiliana na yule rafiki yangu aliyenisaidia mchakato was huyo x-wangu kuja Arusha,nikiwa nimemuomba nifikie kwake nikae kama siku mbili nifanye yangu.
But jamaa akaniambia hatakuwepo yupo Tanga but nikifika kunamtu amemuaxhia ufunguo so nisiwaze nikifika atamuagizia tu anipatie.

Then nikasafiri nilipo fika nikamjulisha akamuagizia mtu nikapewa ifungu,nikaingia ndani nikaa kama dk10,then nikasema ngoja nikaoge,nikaenda kuogo nikarudi nikapumzika tena kidogo lakini katika angalia angalia ndani nikaona barua ya admision ya yule x-wangu wangu pale ndani dah!nikashikwa na butwaa kwanza,nijajifikiria nikasema labda walikuwa wanatembelea kawaida tu,nikaenda kula then nikarudi.

Nikarusha tena macho mara nikaona picha mbalimbali walizopiga pamoja,huku na huku nikakuta nguo za x-wangu huko ndani.dah!!nilihisi kama naota vile.
Nikajikanza kiume kunajaa mmoja jirani yake na yule mshkaji wangu lakini pia nafahamiana na kitambo so,pia nimshkaji wangu ikabidi nikamgongea nimuombe mastory.

Najamaa nikamuuliza vip kuna msichana anasifa moja mbili tatu,alisha wahi kumuona kwa msela,jamaa akaesema ndio mbona ndio mke wa jamaa na tayari kashamsilimisha na anamimba karibia ajifungue.
Sikutaka kumueleza mengi,baada ya kuagana nae nilichofanya nilirudisha ufunguo nikaenda kulala lodge.wewe hapa ungefanyaje?

And Siku angaika kumtafuta mshkaji ili kumuuliza,nimemaliza mambo yangu nikarudi Arusha,ikawa Jamaa amejua yakwamba nimejua baada ya kurudisha ufungua and akawa ananipigia simu sikuweza kupokea coz sijona umuhimu na sababu ya kendelea kuwa na urafiki na rafiki msaliti kama huyu.
Wadau vip tuendelee kuwa marafiki au nimpotezee mazima.
 
Unajipa mawazo mwenyewe kwani nafsi yako isha sita sasa kwanini ujilazimishe.......si wako huyo kaka.Wajilazimisha kwajili ya wivu ila nawe humpendi. Acha kufikiria ngono.
 
Kuna usemi wazungu huwa wanasema "Bros before hos"
Wanaume hua hatugombani kisa mwanamke, pia huyo binti anaonekana yeye ndiyo chenga kama alishasex na mtu nyuma (anaweza asiwe rafiki yako), ukaja wewe kisha rafiki yako leo ndiyo usipokee simu ya mshikaji kisa mwanamke?

Hebu acha zako bwana, pokea simu ongea na jamaa na urafiki uendelee.
 
We achana nae huyo sio rafiki mzuri anaweza kuku7bishia kifo. Maana kama ni mimi kitendo cha kuona nguo na picha2 wangenikuta maiti humo ndani
 
Kuna kamsemo haka bro " trust no body and suspect everybody" kana maana mara nying sna ingawa sio mara zote. katumie bro, hakana shida bro, NAKUOMBA SANA BRO.
 
Kwani kosa la rafiki yako liko wapi mkuu? Je alikuwa anajua kama ni girlfriend wako kipindi unamuomba amsaidie kwenye process za kuja arusha? Huyo mwanamke sio kabisa, yaani ni chenga balaa, wewe usigombane na rafiki yako endelea na maisha kama kawaida, tena ungeenda siku kuwatembelea wakiwa pamoja na usiwaulize chochote. Mshukuru Mungu maana huwezi jua amekuepushia nini mbeleni.
 
Kwani kosa la rafiki yako liko wapi mkuu? Je alikuwa anajua kama ni girlfriend wako kipindi unamuomba amsaidie kwenye process za kuja arusha? Huyo mwanamke sio kabisa, yaani ni chenga balaa, wewe usigombane na rafiki yako endelea na maisha kama kawaida, tena ungeenda siku kuwatembelea wakiwa pamoja na usiwaulize chochote. Mshukuru Mungu maana huwezi jua amekuepushia nini mbeleni.
Mbona nimuweka wazi rafiki yakwamba huyo ni shemeji take mkuu.Nimekuja kukubaliana naa kamsemo huku Arusha huwa wanasema,ukimpa msambaa,milioni kumi na mwanamke,pesa atafikisha salama kabisa lakin mke sahau.
 
Mbona nimuweka wazi rafiki yakwamba huyo ni shemeji take mkuu.Nimekuja kukubaliana naa kamsemo huku Arusha huwa wanasema,ukimpa msambaa,milioni kumi na mwanamke,pesa atafikisha salama kabisa lakin mke sahau.
Pole mkuu mie nakuomba ufanye kitu kimoja, nenda kawatembelee siku moja kama vile unamsalimia rafiki yako, ila usiwaulize chochote maana aibu itakuwa yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom