Elections 2010 Alichokiomba Dr Slaa ni kusitisha kutangaza matokeo, sio Umwagaji damu

Mwanjelwa

JF-Expert Member
Jul 29, 2007
956
145
Nimefuatilia kwa makini sana uchaguzi wa mwaka huu. Nimevutiwa sana kwa jinsi shamra shamra na msisimko mkubwa sana. Hakika Tanzania tumekomaa kisiasa na tunaelekea kwema.

Tatizo langu linakuja pale mmoja wa wagombea, hapa namaanisha Dr. Slaa kuanza kwa maksudi kabisa kutaka kuanzisha fujo zisizo na maana. Kwa jinsi alivyozipanga points zake kwa kusema kura za urais zisimamishwe na si kura za ubunge nadhani kila mmoja anafahamu kuwa alikuwa anakwepa kuudhi washirika wake walioshinda ubunge. Kwa maana hii tunatambua kuwa janja yake kubwa ni kutaka serikali ya kitaifa iundwe. Mimi nakubaliana na hiyo point, ila approach aliyotumia kwa kweli inanipa wasi wasi kama kweli ana busara na ni mtu aliyekomaa kisiasa.

Kama Kiongozi mkubwa si busara kuanza kuchochea ghasia. Hicho kitendo kimenikera sana na sikutarajia kwa kiongozi niliyempa points nyingi sana kabla.

Tusimame kama Watanzania. Kama kuna shida na matokeo, tusubiri kwanza then twende mahakamani.
 
Ghasia uanzia pale sisi m wanapodhani wanatugawia haki zetu. Amini usiamini tutazidai kwa nguvu na mbele ya risasi zenu.
 
get real mwanjelwa..........are you blind or some? cant u see what otherz can see........open up your eyes and stop the bloody rubbish........
 
Nimefuatilia kwa makini sana uchaguzi wa mwaka huu. Nimevutiwa sana kwa jinsi shamra shamra na msisimko mkubwa sana. Hakika Tanzania tumekomaa kisiasa na tunaelekea kwema.

Tatizo langu linakuja pale mmoja wa wagombea, hapa namaanisha Dr. Slaa kuanza kwa maksudi kabisa kutaka kuanzisha fujo zisizo na maana. Kwa jinsi alivyozipanga points zake kwa kusema kura za urais zisimamishwe na si kura za ubunge nadhani kila mmoja anafahamu kuwa alikuwa anakwepa kuudhi washirika wake walioshinda ubunge. Kwa maana hii tunatambua kuwa janja yake kubwa ni kutaka serikali ya kitaifa iundwe. Mimi nakubaliana na hiyo point, ila approach aliyotumia kwa kweli inanipa wasi wasi kama kweli ana busara na ni mtu aliyekomaa kisiasa.

Kama Kiongozi mkubwa si busara kuanza kuchochea ghasia. Hicho kitendo kimenikera sana na sikutarajia kwa kiongozi niliyempa points nyingi sana kabla.

Tusimame kama Watanzania. Kama kuna shida na matokeo, tusubiri kwanza then twende mahakamani.

Subiria matu-si. Hauoni wizi wa kura wa CCM na NEC na jinsi wanavyobaka demokrasia. Polisi wa CCM na green guardi yao ya kuwapiga watu hauoni. Watanzania kudai kura zao ndiyo unaona wewe ovyo kabisa.
 
We ndo unaongea bila kuwa na upeo wa kutosha.kauli unazozitoa si za busara,yani unaongea chenga kabisa na bila shaka upeo wako ni wa kuhesabu vijiti tu km std 1.
Dr hajahamasisha fujo na ana haki ya kuzuia matokeo km ameona hayaendi km inavyotakiwa.
Km huna point ya msingi si lazma uandike huo ujinga wako.
 
Mwanjelwa wewe ni wa kusamehewa tu. Hujui usemalo. Pole sana ndugu.
 
Nimefuatilia kwa makini sana uchaguzi wa mwaka huu. Nimevutiwa sana kwa jinsi shamra shamra na msisimko mkubwa sana. Hakika Tanzania tumekomaa kisiasa na tunaelekea kwema.

Tatizo langu linakuja pale mmoja wa wagombea, hapa namaanisha Dr. Slaa kuanza kwa maksudi kabisa kutaka kuanzisha fujo zisizo na maana. Kwa jinsi alivyozipanga points zake kwa kusema kura za urais zisimamishwe na si kura za ubunge nadhani kila mmoja anafahamu kuwa alikuwa anakwepa kuudhi washirika wake walioshinda ubunge. Kwa maana hii tunatambua kuwa janja yake kubwa ni kutaka serikali ya kitaifa iundwe. Mimi nakubaliana na hiyo point, ila approach aliyotumia kwa kweli inanipa wasi wasi kama kweli ana busara na ni mtu aliyekomaa kisiasa.

Kama Kiongozi mkubwa si busara kuanza kuchochea ghasia. Hicho kitendo kimenikera sana na sikutarajia kwa kiongozi niliyempa points nyingi sana kabla.

Tusimame kama Watanzania. Kama kuna shida na matokeo, tusubiri kwanza then twende mahakamani.

Kama na huyu anawaza hivi, ameridhika na mfumo wa utawala uliopo ambapo Chenge, Lowassa ni wateule aimradi Mramba alikataliwa kwa nguvu ya umma, BASI bado tuna safari ndefu ya kujikomboa KIFIKRA:A S angry:
 
mwanjelwa jitambue kwanza wewe ni nani na kama wewe ni mzalendo utaitakia nchi hii mema! ila kama wewe ni tabaka fisadi na wasiwasi wangu ni kwamba unautetea ufisadi na kama ndivyo wewe ni mpuuzi wa hali ya juu kuna maana gani watanzania kupiga kura then you grap that right! mimi ninachokiona ni wajinga wachache wanaotaka kujimilikisha nchii hii na hawa sio wengine ni wale wanaongangania madaraka ili kuficha madhambi waliyowatendea watanzania kwa nusu karne!
 
Nimewapata wote hapo nitawajibu kwa pamoja.
Labda kama mtaniona sijui kama mmoja wenu alivyosema au ni namna ya kudai haki, vyovyote vile. Lakini, haikuwa busara hata kidogo kwa mtu wa kiwango chake kuongea kitu alichooongea. Hata kama unagombea roho yako isitoke, huwezi lazimisha roho za wengine pia zitoke!. Ni kiwango cha chini kabisa cha busara kwa mtu kama Dr. Slaa kuongea namna ile. Mnaonipinga hapo juu, je mmeweza elewa kwanini Slaa hajaongelea kuhusu Ubunge wakati kwenye Ubunge ndiyo kuna malalamiko zaidi kuliko Urais? NImemsikia BBC jioni akisisitizia matokeo ya Urais tu, kwanini isiwe Ubunge na Udiwani? Sikutarajia, hamna mtu alitarajia. Nilichodhani mimi, angetuambia sisi wafuasi, tusubiri matokeo kwanza na baada ya hapo twende mahakamani.

Hapa ndipo tumefika watu wanasema TOGETHER we stand, Divided it is time to GO.
 
Mwanjelwa
Ulitaka Dr. Slaa akae kimya na mwisho wa siku asaini kuwa amekubaliana na matokeo haya ya ubabaishaji?
Nionavyo mimi Dr. Slaa amefanya kile ambacho watu wengi wenye akiri timamu walikuwa wanakitarajia.
Swali lingine: Je kwa uonavyowewe matokeo haya ni sahihi? kama sio sahihi unafikiri ni tufanye? angalizo Mahakamani: Jaji ni mteuliwa na huyu unayempinga je unafikiria utapata haki huko? Hapa utaweza ona haki utaipata tu kwa nguvu ya uma na sio vinginevyo.
 
Nimewapata wote hapo nitawajibu kwa pamoja.
Labda kama mtaniona sijui kama mmoja wenu alivyosema au ni namna ya kudai haki, vyovyote vile. Lakini, haikuwa busara hata kidogo kwa mtu wa kiwango chake kuongea kitu alichooongea. Hata kama unagombea roho yako isitoke, huwezi lazimisha roho za wengine pia zitoke!. Ni kiwango cha chini kabisa cha busara kwa mtu kama Dr. Slaa kuongea namna ile. Mnaonipinga hapo juu, je mmeweza elewa kwanini Slaa hajaongelea kuhusu Ubunge wakati kwenye Ubunge ndiyo kuna malalamiko zaidi kuliko Urais? NImemsikia BBC jioni akisisitizia matokeo ya Urais tu, kwanini isiwe Ubunge na Udiwani? Sikutarajia, hamna mtu alitarajia. Nilichodhani mimi, angetuambia sisi wafuasi, tusubiri matokeo kwanza na baada ya hapo twende mahakamani.

Hapa ndipo tumefika watu wanasema TOGETHER we stand, Divided it is time to GO.

Mwanjelwa: Slaa anachofanya ni kutaka NEC ije na majibu ya maswali yake hadharani (Kitu ambacho NEC hawana), akisubiri matokeo yote yatangazwe, ujue kitakachofuatia ni kuapishwa kwa Rais mpyaa. Kwa mujibu wa sheria za nchi Rais akisha apishwa tu hakuna kesi yoyote inayoruhusiwa kufunguliwa kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyomweka madarakani Rais huyo. So huu ni wakati muafaka kudai matokeo yasitishwe kutangazwa ili tume itoe ushahidi wa madai ya Slaa.
 
So you're turning your back on Slaa because he refuses to accept the extremely suspicious results?

Coward.
 
Nimefuatilia kwa makini sana uchaguzi wa mwaka huu. Nimevutiwa sana kwa jinsi shamra shamra na msisimko mkubwa sana. Hakika Tanzania tumekomaa kisiasa na tunaelekea kwema.

Tatizo langu linakuja pale mmoja wa wagombea, hapa namaanisha Dr. Slaa kuanza kwa maksudi kabisa kutaka kuanzisha fujo zisizo na maana. Kwa jinsi alivyozipanga points zake kwa kusema kura za urais zisimamishwe na si kura za ubunge nadhani kila mmoja anafahamu kuwa alikuwa anakwepa kuudhi washirika wake walioshinda ubunge. Kwa maana hii tunatambua kuwa janja yake kubwa ni kutaka serikali ya kitaifa iundwe. Mimi nakubaliana na hiyo point, ila approach aliyotumia kwa kweli inanipa wasi wasi kama kweli ana busara na ni mtu aliyekomaa kisiasa.

Kama Kiongozi mkubwa si busara kuanza kuchochea ghasia. Hicho kitendo kimenikera sana na sikutarajia kwa kiongozi niliyempa points nyingi sana kabla.

Tusimame kama Watanzania. Kama kuna shida na matokeo, tusubiri kwanza then twende mahakamani.

Taratibu na sheria mbovu zinazotawala muundo wa uchaguzi wa Bongo ndo zinazomfanya mgombea kama Dr slaa kutamka aliyotamka. Ilivyo ni kwamba tume itakapo tangaza matokeo na Rais kutangazwa na kuapishwa hakuna namna iliyopo sheriani ya kupinga matokeo. Hivyo ni vema na bora kwa mgombea wa urais pale anapogundua kasoro za wazi zinazomkandamiza au kumnyima haki kutamka mapema ili utaratibu ufanyike na tume kutafuta ufumbuzi kabla ya kutangaza matokeo.

Mfano mzuri ni chaguzi zilizotangulia huku Unguja. Alipotangazwa Salimini, Karume, na wengine ilikuwa ndo mwisho wa kulalamikia matokeo. hivyo ni bora ukalilia utatuzi wa utata wa wizi wa kura na uchakachuaji ufanyike mapema na tume ili kupata majibu ya kuridhisha kabla ya kutangaza matokeo.
kuna kasoro kubwa zilizojionyesha wazi wazi bila kificho, hii ni pamoja na kupotea kwa kura ndani ya masanduku, kukamatwa kwa wahesab kura wakiwa na shahaa bandia, kutolingana kwa idadi ya wapiga kura za ubunge na urais, kura kuwa nyingi kuliko idadi ya waliojiandikisha.

Ni bora kurekebisha matatizo haya ambayo yamekuwa sugu ktk chaguzi za Taifa letu sasa na kuingiza madarakani viongozi waliochaguliwa kwa ridhaa ya wananchi ili kujenga demokrasia ya haki na usawa, kuliko kumwona Dr Slaa akilalamikia ubovu na kasoro na kuishia kumkosoa na kusema kuwa umefuatilia kwa makini uchaguzi unavyoendeshwa.

Siku zote demokrasia ya kweli hutawaliwa na haki na utawala wa sheria kwa ridhaa ya wavuja jasho ambao ndo wananchi.
 
Mwanjelwa, unajua kwa nini CCM wamekuwa madarakani kwa kipindi kirefu licha ya dhuluma zao dhidi ya wananchi ? Sasa nakwambia wazi bila kumung'unya maneno ni kwa sababu ya misimamo ya watu kama wewe wenye woga katika kudai haki. Inasikitisha kuwa hadi leo hii mwaka 2010 bado wako Watanzania kama Mwanjelwa wanaoamini kuwa ili kulinda amani na utulivu yabidi watu wakubali kuibiwa, kunyanyaswa, kuonewa na kufanyiwa vitendo vya dhulma. Tukifanya hivyo tunahairisha tu kwa muda kinachoitwa the inevitable kwani malipo yake yatakuwa makubwa zaidi na historia ulimwenguni kote yathibitisha hilo. Gharama ya kudai haki leo ni ndogo sana ikilinganishwa na kuidai kesho au keshokutwa.
 
Nimewapata wote hapo nitawajibu kwa pamoja.
Labda kama mtaniona sijui kama mmoja wenu alivyosema au ni namna ya kudai haki, vyovyote vile. Lakini, haikuwa busara hata kidogo kwa mtu wa kiwango chake kuongea kitu alichooongea. Hata kama unagombea roho yako isitoke, huwezi lazimisha roho za wengine pia zitoke!. Ni kiwango cha chini kabisa cha busara kwa mtu kama Dr. Slaa kuongea namna ile. Mnaonipinga hapo juu, je mmeweza elewa kwanini Slaa hajaongelea kuhusu Ubunge wakati kwenye Ubunge ndiyo kuna malalamiko zaidi kuliko Urais? NImemsikia BBC jioni akisisitizia matokeo ya Urais tu, kwanini isiwe Ubunge na Udiwani? Sikutarajia, hamna mtu alitarajia. Nilichodhani mimi, angetuambia sisi wafuasi, tusubiri matokeo kwanza na baada ya hapo twende mahakamani.

Hapa ndipo tumefika watu wanasema TOGETHER we stand, Divided it is time to GO.

Pole Mwanjelwa, ni wajibu wako kuelewa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya JMT, matokeo ya kura za urais hayapingwi mahakamani wala mamlaka yoyote.
 
Nimewapata wote hapo nitawajibu kwa pamoja.
Labda kama mtaniona sijui kama mmoja wenu alivyosema au ni namna ya kudai haki, vyovyote vile. Lakini, haikuwa busara hata kidogo kwa mtu wa kiwango chake kuongea kitu alichooongea. Hata kama unagombea roho yako isitoke, huwezi lazimisha roho za wengine pia zitoke!. Ni kiwango cha chini kabisa cha busara kwa mtu kama Dr. Slaa kuongea namna ile. Mnaonipinga hapo juu, je mmeweza elewa kwanini Slaa hajaongelea kuhusu Ubunge wakati kwenye Ubunge ndiyo kuna malalamiko zaidi kuliko Urais? NImemsikia BBC jioni akisisitizia matokeo ya Urais tu, kwanini isiwe Ubunge na Udiwani? Sikutarajia, hamna mtu alitarajia. Nilichodhani mimi, angetuambia sisi wafuasi, tusubiri matokeo kwanza na baada ya hapo twende mahakamani.

Hapa ndipo tumefika watu wanasema TOGETHER we stand, Divided it is time to GO.

Kwanza - kwa sababu kagombea uraisi
Pili - wewe si mfuasi wa Slaa bali fisadi la ccm
 
Mag3, Sophist, fishyfish wote mna haki ya kusema, aidha niwe coward, mwoga au vyovyote vile mtavyoita, hata siku moja kushindwa na kudai haki violently is never is solution. Ninachokifahamu ni kukaribisha De campo na wenzake na kuishia kutoaminiana baada ya kiongozi wetu kupelekwa pale. Kuna namna tele za kudai haki, na si kuhamasisha watu waingie mitaani. Hata hivyo, ninavyojua kwa nchi hii hakuna mtu atakuwa tayari kuwa chambo. Tuna muda na kama tumeweza kuchukua viti 51 kama wapizani, kwanini tusiweze kuchukua nchi muda ukifika?!

kwa hiyo nyie ndugu niliowataja hapo juu, mawazo ni mazuri kwa kuandika hapa hapa ili kuyajadili na si mazuri kivitendo mtaani. Bahati nzuri hayo mnayoyasema na kuchochea hamjawahi yapata ila kwa kuona kwenye TV. Ni mbaya sana.
 
kwa hiyo nyie ndugu niliowataja hapo juu, mawazo ni mazuri kwa kuandika hapa hapa ili kuyajadili na si mazuri kivitendo mtaani. Bahati nzuri hayo mnayoyasema na kuchochea hamjawahi yapata ila kwa kuona kwenye TV. Ni mbaya sana.

Acha unafiki fisadi la ccm wewe
 
Acha unafiki fisadi la ccm wewe


Majina yote weka hapa. Ukweli uko pale pale. Hakuna mtu anataka kutokuwa mwoga kwa au mnafiki kwa kuleta fujo ambazo hazina tija. Twende mbele na turudi, si njia njema.
Tujadili hoja.
 
Wote (au wengi) tumesikia alichosema.

Ameomba kura zisitishwe kutangazwa.

Mimi ningeongeza kuwa, matokeo yajumlishwe upya kwa kutumia namba za mwanzo zilizopatikana katika kila kituo na kusainiwa na mawakala wa vyama vyote.

Mafisadi wa ccm mmeanza kubadili mambo (kama kawaida yenu) na kudai kuwa Slaa anataka damu ya watanzania imwagike. Swali rahisi kwenu, kuna uhusiano gani kati ya kusitisha zoezi la kutangaza matokeo na damu kumwagika?

Kama kweli ccm mmeshinda, kwa nini msikubali kura zijumlishwe upya (sio kuhesabiwa upya)?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom