Alianza Mkapa.... hawa wanafuata tu..

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
Madiwani ruksa kushindania zabuni

2007-12-17 08:32:28
Na Bigambo Jeje, PST Musoma


Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kutowanyima zabuni madiwani kwa kusingizia kuwa hawastahili kufanya biashara na halmashauri zao.

Aidha, hakuna sheria inayowazuia madiwani kufanya biashara na halmashauri yoyote ile.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Ofisa Ugavi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Athuman Ngwalo.

Aliyasema hayo mjini Musoma, wakati akiwasilisha mada ya ununuzi wa vifaa vya umma katika semina ya siku mbili ya Mradi wa Uwekezaji katika Kilimo Vijijini (DASIP).

Semina hiyo ilihudhuriwa na maofisa wa mradi huo kutoka Wilaya sita za Mikoa ya Mara, Mwanza na Shinyanga.

Bw. Ngwalo alisema kwa mujibu wa Sheria ya ununuzi wa vifaa vya umma ya mwaka 2004, kifungu cha tatu kimewataja watumishi wote wa serikali wasiotakiwa kufanya biashara yoyote na halmashauri au serikali kuu zikiwemo na zabuni mbalimbali.

Alisema sheria hiyo haijawataja madiwani kwamba ni watumishi wa umma hivyo wanaruhusiwa kufanya biashara hiyo.

Alisema amesikitishwa kusikia kwamba baadhi ya halmashauri zimekuwa zikiwanyima zabuni madiwani wanapoomba kazi katika halmashauri kupitia kampuni zao.

Alisema uamuzi huo ni wa uonevu na unawanyima haki zao za msingi.


Alisema awali, madiwani walikataliwa kupewa zabuni kisheria kulingana na Sheria ya ununuzi ya vifaa vya umma ya mwaka 2001 kwa kuwa walikuwa ni wajumbe wa bodi za zabuni katika halmashauri zao.

Alisema baada ya Sheria hiyo kufanyiwa marekebisho na kuwaondoa madiwani kwa kuwavua ujumbe wa bodi hizo mwaka 2004, sasa kushindania zabuni kwao si dhambi tena.

Alisisitiza kuwa kama kampuni ya diwani ina vigezo vyote vinavyotakiwa kwa mujibu wa zabuni iliyotangazwa na kuonekana imeshinda zabuni hiyo halmashauri husika inatakiwa kuitangaza kama mshindi kampuni hiyo.

Ofisa huyo alizishauri halmashauri kuzitumia taasisi za serikali kama vile vikosi vya Jeshi, Magereza na Ujenzi kufanya kazi za maendeleo katika halmashauri badala ya kutegemea wazabuni.

SOURCE: Nipashe


My Take:

Finally a Licence to ufisadi has been given!
 
Kwa hali ya sasa hivi Tanzania chochote chaweza kutokea maana mkuu wa kaya yeye anakimbilia kupiga picha na boyz 2 men kiwanja na Lowasa yuko bize kutafuta richmonduli nyingine!

Kazi ipo bongo hiyo!
 
Sasa kama hatuwezi kuelewa conflict of interest in such as simple scenario, bado tutasema sisi tuna uongozi kweli?
 
Kama kweli wewe ni kiongozi na unaona unaweza kufanya biashara vizuri zaidi kwa nini uendelee kukaa madarakani? Achia ngazi na ukomalie kwenye biashara ambayo itakuingizia pesa kuliko kukaa kwenye halmashauri ambazo zinakunyima uhuru wako wa kufanya biashara. Je, msemaji wa Ikulu anasemaje kuhusu swala hili?

Kwa mwendo huu hata 2010 hatuwezi kufika.
 
Wakati umefika tuwe na utaratibu wa kusimamia conflict of interest kwa viongozi wetu. Watu wanatafuta uongozi kusidi wautumie kujipatia mali badala ya kutekeleza majukumu ya uongozi. Kama madiwani wakiruhusiwa kugombea tenda za serikali za mitaa wanzoongoza, halafu wao hao hao ndio waamue nani wa kupewa tenda hizo je ni kweli rai wengine watazipata?
 
Watasubiri kusikiliza malalamiko ya wananchi kuhusu uamuzi huu. Wakiona kumekuwa na kimya baada ya muda mfupi basi tusishangae kusikia wizara zisiwanyime zabuni mawaziri na makatibu wakuu wa wizara mbali mbali. Hapo ndio usanii utaongezeka kwa kasi sana maana hakuna waziri au katibu mkuu atakayekaa ofisini kufanya kazi za siri kali, wote watakuwa busy kufukuzia zabuni za mawizara mbali mbali! Vichwani mwao hawa viongozi uchwara maadili ya viongozi hayana maana yoyote!
 
Kiini cha haya yote ni Azimio la Zanzibar. Hawa jamaa waliua miiko ya uongozi bila kuweka sheria ambayo ingelinda conflict of interest. Leo hii huwezi kushangaa kusikia waziri wa nishati na madini ana miliki mgodi au waziri wa mawasiliano na uchukuzi anamiliki kampuni ya uchukuzi au mawasiliano.

Wakati Msekwa akiwa Spika wa Bunge, alipewa ulaji Vodacom na watu walipokuja juu na kumtaka achague kimoja alikuwa bold na kusema hakuna mgongano wa kimaslahi na wale wanaotaka aachie ngazi moja ni kwamba wanamuonea wivu tu. Hawa ndiyo viongozi wetu na baada ya kutoka nje ya Bunge akawa mtu wa kwanza kusema Katiba ya Tanzania inatakiwa kufanyiwa marekebisho. Leo hii baada ya kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM ukimwambia hayo maneno ya kurekebisha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakuambia katiba ni safi na wala hakuna haja ya kuibadilisha bali ni kuweka viraka vya hapa na pale ambavyo havigusi maslahi yao bali vinazidi kuwaumiza wananchi wa kawaida na kuwanyima haki yao.
 
Have you ever get to the point and said it's over, i better search for other country citizenship. I believe i am on that point, i can't believe every time i opened the newspaper i found some stupid nonsenses.

Who ever support this need to know conflict of interest, will the common man be able to win zabuni if mayors and many other governmental leaders join the race? What are this people thinking? Does this people understand that Tanzania is the country, and not a porker club?

Mr JK is busy doing non sense, just showing his cute face on unknown medias. For God sake we need our country back, we need the leadership we always desires. Where is strong upinzani? Where is our roots and humble leaderships? Where are we going? We look like youngs and dumbs with full of something. God help us, because that is the only power that we relied on.
 
Azimio la Zanzibar liliua Azimio la Arusha..hasa katika miiko ya uongozi.Swali: Mwalimu Nyerere ambaye ndiye kinara wa Azimio la Arusha alikuwa wapi wakati Azimio la zenji linapitishwa.Aliwahi kukemea?Au naye aliona alama za nyakati akaamua kukaa kimya.
Kwa kuwa viongozi nao ni wanadamu na wana desires za kuwa watu wa maana,watu wenye fedha na umaarufu wana haki ya kujitafutia bila kuvunja sheria.Kumwekea mwanadamu vikwazo ili asiweze kufanikiwa katika maisha si jambo la akili bali ni hulka ya wivu.Linatakiwa ni kuwa uwazi uwepo katika kila jambo.Kama mtu anaweza kumiliki mali kwa njia za halali hakuna ubaya.Na kama kuna hila katika kuipata ie mali,aidha kwa ufisadi au rushwa sheria zifuate mkondo.Kinachotakiwa ni kwa viongozi kuwa waadilifu.
 
Hapa bado kuna Conflict of Interest wazeee....kama wajumbe wa Bodi ya zabuni watafuata sheria/kanuni za manunuzi..inatakiwa wafanze declaration ya conflict of interest kwa mtu yeyote aliyeomba zabuni, eg kama ni ndugu,mme,mke,mtoto, au kama ni muajiri wake kwa namna yeyote ile etc etc..na wakisha declare interest wanatakiwa wasishiriki ktk kuijadili hiyo zabuni..Hivyo basi,kufuatana na kwamba Halmashauri ipi chini ya Madiwani kwa hiyo wajumbe wote wa bodi ya zabuni ni waajiriwa wa madiwani na hivyo wote wanatakiwa ku-declare conflict of interest wakati wa kujadili zabuni toka kwa diwani yeyote!

Kisheria,diwani anaweza kutender ktk Halmashauri zingine zote isipokuwa anayoiongoza yeye!!!

Huyo Afisa ugavi alitoa tafsiri rahisi pasipo kufikiri matokeo yake..ama kwa makusudi au pasipokujua!
 
Hapa bado kuna Conflict of Interest wazeee....kama wajumbe wa Bodi ya zabuni watafuata sheria/kanuni za manunuzi..inatakiwa wafanze declaration ya conflict of interest kwa mtu yeyote aliyeomba zabuni, eg kama ni ndugu,mme,mke,mtoto, au kama ni muajiri wake kwa namna yeyote ile etc etc..na wakisha declare interest wanatakiwa wasishiriki ktk kuijadili hiyo zabuni..Hivyo basi,kufuatana na kwamba Halmashauri ipi chini ya Madiwani kwa hiyo wajumbe wote wa bodi ya zabuni ni waajiriwa wa madiwani na hivyo wote wanatakiwa ku-declare conflict of interest wakati wa kujadili zabuni toka kwa diwani yeyote!

Kisheria,diwani anaweza kutender ktk Halmashauri zingine zote isipokuwa anayoiongoza yeye!!!

Huyo Afisa ugavi alitoa tafsiri rahisi pasipo kufikiri matokeo yake..ama kwa makusudi au pasipokujua!
 
Azimio la Zanzibar liliua Azimio la Arusha..hasa katika miiko ya uongozi.Swali: Mwalimu Nyerere ambaye ndiye kinara wa Azimio la Arusha alikuwa wapi wakati Azimio la zenji linapitishwa.Aliwahi kukemea?Au naye aliona alama za nyakati akaamua kukaa kimya.
Kwa kuwa viongozi nao ni wanadamu na wana desires za kuwa watu wa maana,watu wenye fedha na umaarufu wana haki ya kujitafutia bila kuvunja sheria.Kumwekea mwanadamu vikwazo ili asiweze kufanikiwa katika maisha si jambo la akili bali ni hulka ya wivu.Linatakiwa ni kuwa uwazi uwepo katika kila jambo.Kama mtu anaweza kumiliki mali kwa njia za halali hakuna ubaya.Na kama kuna hila katika kuipata ie mali,aidha kwa ufisadi au rushwa sheria zifuate mkondo.Kinachotakiwa ni kwa viongozi kuwa waadilifu.


Hoja zako nzuri sana Mkuu,
Lakini mimi na taka niulize hivi ,hivi kweli kabisa unahisi Vionzozi wetu hawa wana UADILIFU ulio usema?
Ili tuweze kukubariana katika hayo uliyo yasema ili tusionekane ni wenye kuwaonea wivu.
Wewe mwenewe umesema,"viongozi nao ni wanadamu na wana desires za kuwa watu wa maana,watu wenye fedha na umaarufu wana haki ya kujitafutia bila kuvunja sheria"
Kwa maneno mengine wao pia ni wadhaifu,nawanaweza kutumia udhaifu huo kufanya linalo wezekana ili waweze kupata uo UMAARUFU na PESA kwa kutumia vyeo vyao na Ushawishi walionao katika bodi hizo za zabuni ukilinganisha na wafanyabiashara wa kawaida wanao omba zabuni kiharali.

Kuhusu Azimio la Zanzibar,Nyerere alisha protest na kusema "wameliacha azimio la Arusha baharini" na kuja na azimio la Zanzibar.
Msekwa alipo ulizwa kuhusu hilo kwenye kipindi kimoja cha TV baada ya kupewa Umakamu mwenyekiti,alichoseama ni "tulipokaa zanzibar ilikua ni kulekebisha vipengele vichache ktk lile la Arusha ila sio kuribadilisha na hasa kwenye miko ya viongozi"
 
Hapa bado kuna Conflict of Interest wazeee....kama wajumbe wa Bodi ya zabuni watafuata sheria/kanuni za manunuzi..inatakiwa wafanze declaration ya conflict of interest kwa mtu yeyote aliyeomba zabuni, eg kama ni ndugu,mme,mke,mtoto, au kama ni muajiri wake kwa namna yeyote ile etc etc..na wakisha declare interest wanatakiwa wasishiriki ktk kuijadili hiyo zabuni..Hivyo basi,kufuatana na kwamba Halmashauri ipi chini ya Madiwani kwa hiyo wajumbe wote wa bodi ya zabuni ni waajiriwa wa madiwani na hivyo wote wanatakiwa ku-declare conflict of interest wakati wa kujadili zabuni toka kwa diwani yeyote!

Kisheria,diwani anaweza kutender ktk Halmashauri zingine zote isipokuwa anayoiongoza yeye!!!

Huyo Afisa ugavi alitoa tafsiri rahisi pasipo kufikiri matokeo yake..ama kwa makusudi au pasipokujua!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom