Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,391
- 39,484
Madiwani ruksa kushindania zabuni
2007-12-17 08:32:28
Na Bigambo Jeje, PST Musoma
Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kutowanyima zabuni madiwani kwa kusingizia kuwa hawastahili kufanya biashara na halmashauri zao.
Aidha, hakuna sheria inayowazuia madiwani kufanya biashara na halmashauri yoyote ile.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Ofisa Ugavi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Athuman Ngwalo.
Aliyasema hayo mjini Musoma, wakati akiwasilisha mada ya ununuzi wa vifaa vya umma katika semina ya siku mbili ya Mradi wa Uwekezaji katika Kilimo Vijijini (DASIP).
Semina hiyo ilihudhuriwa na maofisa wa mradi huo kutoka Wilaya sita za Mikoa ya Mara, Mwanza na Shinyanga.
Bw. Ngwalo alisema kwa mujibu wa Sheria ya ununuzi wa vifaa vya umma ya mwaka 2004, kifungu cha tatu kimewataja watumishi wote wa serikali wasiotakiwa kufanya biashara yoyote na halmashauri au serikali kuu zikiwemo na zabuni mbalimbali.
Alisema sheria hiyo haijawataja madiwani kwamba ni watumishi wa umma hivyo wanaruhusiwa kufanya biashara hiyo.
Alisema amesikitishwa kusikia kwamba baadhi ya halmashauri zimekuwa zikiwanyima zabuni madiwani wanapoomba kazi katika halmashauri kupitia kampuni zao.
Alisema uamuzi huo ni wa uonevu na unawanyima haki zao za msingi.
Alisema awali, madiwani walikataliwa kupewa zabuni kisheria kulingana na Sheria ya ununuzi ya vifaa vya umma ya mwaka 2001 kwa kuwa walikuwa ni wajumbe wa bodi za zabuni katika halmashauri zao.
Alisema baada ya Sheria hiyo kufanyiwa marekebisho na kuwaondoa madiwani kwa kuwavua ujumbe wa bodi hizo mwaka 2004, sasa kushindania zabuni kwao si dhambi tena.
Alisisitiza kuwa kama kampuni ya diwani ina vigezo vyote vinavyotakiwa kwa mujibu wa zabuni iliyotangazwa na kuonekana imeshinda zabuni hiyo halmashauri husika inatakiwa kuitangaza kama mshindi kampuni hiyo.
Ofisa huyo alizishauri halmashauri kuzitumia taasisi za serikali kama vile vikosi vya Jeshi, Magereza na Ujenzi kufanya kazi za maendeleo katika halmashauri badala ya kutegemea wazabuni.
SOURCE: Nipashe
My Take:
Finally a Licence to ufisadi has been given!
2007-12-17 08:32:28
Na Bigambo Jeje, PST Musoma
Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kutowanyima zabuni madiwani kwa kusingizia kuwa hawastahili kufanya biashara na halmashauri zao.
Aidha, hakuna sheria inayowazuia madiwani kufanya biashara na halmashauri yoyote ile.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Ofisa Ugavi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Athuman Ngwalo.
Aliyasema hayo mjini Musoma, wakati akiwasilisha mada ya ununuzi wa vifaa vya umma katika semina ya siku mbili ya Mradi wa Uwekezaji katika Kilimo Vijijini (DASIP).
Semina hiyo ilihudhuriwa na maofisa wa mradi huo kutoka Wilaya sita za Mikoa ya Mara, Mwanza na Shinyanga.
Bw. Ngwalo alisema kwa mujibu wa Sheria ya ununuzi wa vifaa vya umma ya mwaka 2004, kifungu cha tatu kimewataja watumishi wote wa serikali wasiotakiwa kufanya biashara yoyote na halmashauri au serikali kuu zikiwemo na zabuni mbalimbali.
Alisema sheria hiyo haijawataja madiwani kwamba ni watumishi wa umma hivyo wanaruhusiwa kufanya biashara hiyo.
Alisema amesikitishwa kusikia kwamba baadhi ya halmashauri zimekuwa zikiwanyima zabuni madiwani wanapoomba kazi katika halmashauri kupitia kampuni zao.
Alisema uamuzi huo ni wa uonevu na unawanyima haki zao za msingi.
Alisema awali, madiwani walikataliwa kupewa zabuni kisheria kulingana na Sheria ya ununuzi ya vifaa vya umma ya mwaka 2001 kwa kuwa walikuwa ni wajumbe wa bodi za zabuni katika halmashauri zao.
Alisema baada ya Sheria hiyo kufanyiwa marekebisho na kuwaondoa madiwani kwa kuwavua ujumbe wa bodi hizo mwaka 2004, sasa kushindania zabuni kwao si dhambi tena.
Alisisitiza kuwa kama kampuni ya diwani ina vigezo vyote vinavyotakiwa kwa mujibu wa zabuni iliyotangazwa na kuonekana imeshinda zabuni hiyo halmashauri husika inatakiwa kuitangaza kama mshindi kampuni hiyo.
Ofisa huyo alizishauri halmashauri kuzitumia taasisi za serikali kama vile vikosi vya Jeshi, Magereza na Ujenzi kufanya kazi za maendeleo katika halmashauri badala ya kutegemea wazabuni.
SOURCE: Nipashe
My Take:
Finally a Licence to ufisadi has been given!