Ali Kiba Fans' Special Thread...

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
55,791
90,556
Mashabiki wa Ally Kiba wajumuike hapa kumpa ushauri what is next baada ya mashabiki kuonesha mapenzi yao ya dhati kwa Kiba kwenye Fiesta na kuandika historia mpya Tanzania.

Mimi kama Matola nitatumia effort zangu binafsi kuhakikisha nakutana na Kiba na manegement yake ili kuwapa mikakati ya mfalme huyu aweze kuutunza huu ufalme wake.

La kwanza niko tayari kutoa Tshirt za Kiba zenye kiwango ambapo shughuri ya kuziandaa kuna kampuni iko South Africa inaweza kuleta Tshirt katika viwango vya USA.

warumi nifah geniveros

Nisaidieni kuwaita wadau ili tumtengeneze Ally Kiba sasa na nitahakikisha anafunguwa ID hapa kwa jina lake ili kujibu maswali ya wadau pale patakapokuwa na ulazima wa yeye kufanya hivyo. Yeye siyo wa level ya Instagram.


-------------

Ufafanuzi juu ya zawadi



Kwa hisani ya Mkuu Matola, nathibitisha kuwa amefikisha habari kwetu kutoa zawadi ya thamani ya shilingi elfu ishirini (20,000/-) kwa ajili ya mshindi atakaye bahatika post yake kuwa ya kwanza kuingia ukurasa wa 100 katika uzi huu.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na Mkuu Matola ambaye ni mwandalizi wa zawadi hii. Zawadi hiyo itatolewa na Moderator wa JF.

Wasalaam!

Taarifa ya Mshindi

Mshindi wa shindano hili ni Mkuu @geniveros ndiye aliweza kubahatika bandiko lake kuingia na kufungua ukurasa wa 100 wa mada hii hivyo kujipatia kifurushi cha thamani ya shilingi alfu ishirini (20,000/-) na amekiri kuwasiliana na Mkuu @Matola juu ya zawadi hiyo.

Pongezi kwa washiriki wote.

JF Team inashukuru kwa uwepo wenu.

Wasalaam!
 
Kuanzia kesho nitatafuta mawasilano ya Kiba nitaonana naye ana kwa ana kuzungumza naye hii program na nijuwe yeye na Manegement yake wamejipangaje na mimi sifanyi mambo kienyeji kama wako tayari niandae mzigo nitasaini nao mikataba halali ya kibiashara na tutasambaza AK gear. na kama kuna Fans wenye namba ya AK wanitupie inbox ili kunirahisishia kazi.

Ningeshauri huyu Mfalme aitwe AK 47.
 
Wazo Zuri sana. Tutashirikiana kumleta Kiba JF naye awe Akitoa taarifa na kujibu maswali humu. Safi sana, yeye sio levo za Instagram huku ndiko kunakomfaa.
Ova
 
Huyu jamaa namkubali sana sema nyie ndiyo mtamwangusha mapema sababu mnamwingiza kwenye bifu zisizo na kichwa hivi vitu vina wakati na majira kama wakati wake wa kuwaa juu umefika hakuna wa kuzuia ila kama muda bado mtalazimisha lakini atabaki hapo hapo tu. muacheni afanye kazi zake msimwingize kwenye mashindano , wewe ukitoa t.shert ni vzr coz upo unachangamkia fursa .
 
Tishert hizo yani ni bonge la idea will be cool naunga mkono hoja nami ntazipigia kampeni tuzinunue
nyie upande wa pili fanyeni yenu
 
Mwacheni aliyetoa hivyo vipaji ahukumu kwa haki yake na kwa wakati wake, kama wakati haujafika wa alikiba kuwa juu tena hata mumpe promo kiasi gani hatapanda chati, na kama wakati wa diamond kushuka chati haujafika hata azomewe na wamdiss kwa aina na kiasi gani haitasaidia kumshusha sana sana mnampaisha juu zaidi.
 
Mhhhhhhhh sasa huyu King alikua wapi siku zote????????
Kasubiri wenzake wamekaa kwenye game eti "The king is back...

Ali Kiba tunajua una sauti nzuri ila you were having all the time hukuweza kutumia
usilazimishe kurudi kwa nguvu just let the nature do its course.. ni sawa na sa hizi
Afande Sele arudi aanze kusema "Mfalme wa Rhymes" nimerudi" Ni kitu hakiwezekani
Kila mfalme na wakati wake..
 
44 Reactions
Reply
Back
Top Bottom