Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,791
- 71,197
Bulembo wewe ni mbarikiwa kuweza kupata nafasi adimu sana kati ya zile 10 kuteuliwa kuwa mbunge wa Rais.
Inaaminika kwa nafasi hiyo mengi ya usemayo unawakilisha mawazo ya aliyekuteua maana hujachaguliwa. Je, wewe kutangaza Zitto auwawe huoni ni kama unatangazia dunia kuwa aliyekuteua (Rais) ndio alichotaka useme?
Je, tuamini kuwa Rais kachukia sana na ana mawazo hayo ya kumuondoa Zitto?
Ona ulivyochafua nchi na kuifanya ionekane kituko duniani! Nchi inayotaka kuua wabunge wake kwa maagizo ya bungeni.
Simama hadharani utamke haraka kuwa ulipotoka na kuomba radhi huku ukihakikishia umma kuwa aliyekuteua Rais John Magufuli hajakutuma huo ujinga.
Na jitafakari sana. Je, unaitendea haki nafasi hiyo au haikutoshi uiachie?
Sent using Jamii Forums mobile app
Inaaminika kwa nafasi hiyo mengi ya usemayo unawakilisha mawazo ya aliyekuteua maana hujachaguliwa. Je, wewe kutangaza Zitto auwawe huoni ni kama unatangazia dunia kuwa aliyekuteua (Rais) ndio alichotaka useme?
Je, tuamini kuwa Rais kachukia sana na ana mawazo hayo ya kumuondoa Zitto?
Ona ulivyochafua nchi na kuifanya ionekane kituko duniani! Nchi inayotaka kuua wabunge wake kwa maagizo ya bungeni.
Simama hadharani utamke haraka kuwa ulipotoka na kuomba radhi huku ukihakikishia umma kuwa aliyekuteua Rais John Magufuli hajakutuma huo ujinga.
Na jitafakari sana. Je, unaitendea haki nafasi hiyo au haikutoshi uiachie?
'I have no regrets': Tanzania politician branded traitor over World Bank loan
Opposition leader Zitto Kabwe received death threats after asking bank to suspend education fund over human rights concerns
www.theguardian.com
Sent using Jamii Forums mobile app