Alfred Tibaigana na Said Mwema tutawakumbuka Daima!

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Hawa ni viongozi wastaafu wa jeshi la polisi ambao walitenda wajibu wao kwa weledi mkubwa kwa kuitumia sheria ipasavyo, kuitambua katiba ya nchi na demokrasia kwa ujumla pamoja kutumia hofu ya Mungu!

Ni viongozi ambao walitumia njia ya majadiliano kutafuta suluhu kila kunapotokea sintofahamu hasa kuhusu masuala ya kisiasa!Hawakupenda kushinikizwa kufanya kazi ispokua walizingatia sheria,kanuni na taratibu za kazi zao. Lakini pamoja hayo yote nao walikua na mapungufu makubwa tu lakini kuna tofauti kubwa kabisa ya utendaji wao na hawa wa Sasa tunaowaona, polisi wa Sasa kazi zao zinapwaya kabisa, wanafanya upendeleo wa wazi wazi bila hata kuzingatia sheria za nchi.

Kwa utendaji huu wa jeshi letu la polisi kwa muda huu wa uchaguzi watasababisha maafa makubwa kwa raia!

Binafsi sioni mantiki yeyote ya kumwacha mtu anayetukana wazi wazi na kuhangaika na yule anayetembea mtaani kusalimia wananchi wenzake kwa kisingizio cha kuhatarisha amani yake, kuna mantiki gani kuzia wanachama wa chama kimoja kuandamana kuelekea kwenye mikutano yao ya kampeni ili hali chama kiingine wanaandamana, mtu akikwambia "usipoyapata mabadiliko nyumbani kwako utayapata nyumbani kwangu" anaitwa mchochezi!Haya yote hatukuyashuhudia huko nyuma lakini leo tunayaona.

Kwahiyo kuna kuna kila sababu ya kuwakumbuka makamanda hawa wastaafu kwa maana wamaliza kazi mikono yao ikiwa misafi! Na hawa pia tunawaomba wafuate nyao ya wastaafu hawa ukizingatia siasa sasa ni tofauti na ya zamani, watu wameongezeka,mazingira yamebadilika,mbinu za kufanya siasa zimebadilika zimekua za kisasa zaidi!

Wasitumie mabavu na ubabe kuzuia vuguvugu flani badala ya kuzingatia uhalisia wa mambo na kutafuta suluhu kwa majadiliano na wahusika.
 
.....nikipata cv ya huyu jamaa wa kanda maalamu naweza kuchangia kwa facts! Cv tafadhali, maana shule nayo bwana, aah basi tu!!!!
 
Huyu Kova ni mlambaviatu.

Mangu lazima agangamale kwani ni kama MAKOFULI.....hakutaraji angepewa UAIJIPII.
 
Saidi mweema aliye uwa makamanda wetu 3 pale A town 2010 huyu tuanaenda mdogo mdogo adi na yeye 'tumrestishe ini pisi' hatuja sahau yaani ni bandika bandua alipo tupo hata afanyeje.....
 
Saidi mweema aliye uwa makamanda wetu 3 pale A town 2010 huyu tuanaenda mdogo mdogo adi na yeye 'tumrestishe ini pisi' hatuja sahau yaani ni bandika bandua alipo tupo hata afanyeje.....
Wewe unafikiri kwa uongozi wa jeshi hili la polisi ingekua enzi za Mwema hali ingekuaje? Maana sasa hivi ukiukwaji wa sheria ni mkubwa kuliko zamani.
 
Polisi hawajawahi kufanya kazi kwa weledi unaotakiwa.
Wote walikuwa na madudu yao.
 
said mwema atakumbukwa kwa mambo mengi sana, alifanya mema mengi sana,

ikiwa kuliunganisha jeshi la polisi kuwa rafiki na raia, alikua mtu wa diplomasia zaidi kuliko kutumia mabavu,

nikweli kila mwanadamu anamapungufu yake, lakini huyu bwana alijitaidi sana,
 
said mwema atakumbukwa kwa mambo mengi sana, alifanya mema mengi sana,

ikiwa kuliunganisha jeshi la polisi kuwa rafiki na raia, alikua mtu wa diplomasia zaidi kuliko kutumia mabavu,

nikweli kila mwanadamu anamapungufu yake, lakini huyu bwana alijitaidi sana,
That's a truth!
 
TIBAIGANA sawa, ila Mwema alifanya madudu mengi sana, mauaji ya MWANGOSI, mauaji ya Soweto Arusha, Bomu Olasiti yametia doa utawala wake.
 
TIBAIGANA sawa, ila Mwema alifanya madudu mengi sana, mauaji ya MWANGOSI, mauaji ya Soweto Arusha, Bomu Olasiti yametia doa utawala wake.
Unajua mkuu kwa tunaomfahamu mwema hatukurupuki kumsifia! Mwema alikua ni msomi ambaye ni mgumu sana kusikiliza shinikizo lolote kutoka juu! Haya matukio uliyoyataja yalikua hayatokei kwa maagizo yake, sometimes yalikua yakitokea yeye akiwa hana taarifa na hajui!Fuatilia hujuma zote walizokua wakililia kuhujumiwa huwezi kumsikia Mwema katajwa.
 
said mwema atakumbukwa kwa mambo mengi sana, alifanya mema mengi sana,

ikiwa kuliunganisha jeshi la polisi kuwa rafiki na raia, alikua mtu wa diplomasia zaidi kuliko kutumia mabavu,

nikweli kila mwanadamu anamapungufu yake, lakini huyu bwana alijitaidi sana,

Police Jamii and Human Rights promoter kwa hilo nampa well done. But gharama za HR ndani ya nchi changa ndio hizi polisi kuvamiwa na kupigwa kama watoto, kuna shida ya watu ku-abuse polite bhv ya askari waadilifu.
 
Polisi hawajawahi kufanya kazi kwa weledi unaotakiwa.
Wote walikuwa na madudu yao.

are you writing from the core? Au ni ushabiki wa kisiasa? Hayo madudu ya police ndo yanakufanya unasafiri bila hofu na kuikuta familia yako salama salimini. Usichangie kwa kujumuisha kila kitu na siasa.
 
yule makam aliye toa amri ya kuuwa watu pemba yuku wapi? ameisha sahaurika, hata wengine humu hamumjui
iwe ni kwa mbilinyungu, ajali, hata resasi kiama chake kitamfika tuu alipo tupo adi kieleweke....
 
Ni Dr. Saidi Mwema alipewa udaktari wa heshima mwaka jana natumaini Magufuli atampa ubalozi maana anastahili nafasi hiyo kachero huyu wa zamani wa INTERPOL
 
Back
Top Bottom