Alex Msama Vp Tena Na Rose Mhando??

Heloo

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
4,391
3,402
Habari zenu wanajanvi.
Katika Gazeti.la Kiu toleo no.1472 la Tarehe 9-11,2016.Alex Msama anamtuhumu Rose Mhando kama ni Mtumiaji mkubwa wa Madawa ya Kulevya ,kamtoa Mara nyingi police pia kamlipia madeni Na pia Rose Mhando keshawatapeli wachungaji Na Eti hiyo ni Laana.Na Tena anadai keshamkombolea nyumba yake isipigwe Mnada kwa madeni pia keshamlipia madeni yapatayo Milioni 100,Lakini mwandishi walipomuuliza mbona.Madai yako hayafanani Na Ukweli??kwa Maana kwamba Rose akiwa analalamika kwamba yeye.kwa Sasa analala njaa Na wao wanaendesha Magari ya kifahari.Na majumba ya kifahari wakati wanakutana walikuwa masikini wa kutupwa ila Leo hawapokei simu yake.Mwaandishi.anadai.Sauti ya Rose au muonekano sio ya mtumiaji wa Madawa kama inavyodaiwa.Yeye Msama Anasisitiza Anajidunga.kila siku.Milioni 1 Na ni tapeli ndo maana kamkimbia hataki Tena kujihusisha naye.Na Pia kadai Kuwa Rose Hana Jeuri ya kujaza uwanja wa Taifa ndo mana katika Albalm yake Mpya aliyozindulia Diamond Jubilee hakujaza .Sawa tumuamini Nani.Hakuna hata Picha ya ushahidi kwamba anatolewa.kila Mara Police.Picha anayojidunga au aliyechooka kama akina Nice,chid,Ray C.Sisi wapenzi wa Rose Mhando tutakikisha VIP.Au Je Kuna Kitu zaidi ya hicho??Hivi Wewe Msama Dereva Tax wa Zamani unaweza mlipia Rose Mhando Milioni 80 ya madeni yake unavyopenda sifa si tungejua??
Kuna siku Uwanja wa Taifa nilikuwepo uwanjani.Ilikuwa siku ile mama Salma kikwete anaaga Na kuombea Amani kabla ya uchaguzi wa mwaka jana.Rose Mhando aliwekwa wa mwisho kuimba Na mwisho wa siku Mtangazaji akasema Rose Hataimba Tena.Karibia uwanja.mzima ulilipuka kwa Hasira why???walipoona Nguvu ya Rose Ni kubwa wakamleta.Aliimba vizuriii mno Tena zaidi ya zamani.Tena wimbo wake ulikuwa.kama una maneno 'Mungu kama Kaniweka juu Shetani huwezi nishusha.Watu walisikikaa wakiimba naye.Niseme Ukweli.. Rose Hata kama Kateleza kama Binadamu wa kawaida bado anayo Nguvu Tena kuubwa.Na kama kuna malalamiko dhidi yake Basi itumike Busara.Kupotea kwa Rose Mhando kwenye Anga la Muziki wa Injili Ni kama Kanumba kwa Bongo Movies kwa Sasa.Na pia Rose alisema Jamani nazushiwa navuta unga hivi Mvuta unga aliyekubuhu kama madai yao Anawez kuimba Na kukumbuka mashairi Na Stepu kama hivi???Promota mwingine anayesoma hapa tafadhari nakuomba ukamuokoe Rose.Kuna Ukweli unafichwa!!!Huwezi kazana Sema Fulani hivi Bila Hata ushahidi.
Wito wangu kwa Rose pambana.Tafuta Promota mwingine.Nguvu unayo kubwa kwenye Soko la injili Tanzania Na Africa.Hizo zingine Ni Changamoto tu na uzifanyie Kazi kama zipo.Mungu anakupenda.Na naamini Watanzania Wengi tunapenda sana Kazi zako.Umejaaliwa Sauti Tamu Na nzuri.Maadui zako hawawezi kutokukubaliana kwamba Wewe Ni Mgodi unaotembea!!!!
 
aisee,mungu atamsaidia huwa namkubali anafanya mziki mzuri sana ngoja mapromota waje najua watauelewa uzi wako mkuu .
 
Aisee yaan leo hii kuna watu nilipanda kwenye daladala wakawa wanaongelea Rose alivo kuwa amekamata muziki, huyo jamaa kipindi hiko alienda Zambia huko, mpakani na Zimbabwe anakwambia alikuta Rose nyimbo zake zinapendwa kweli, na zilikuwa zikipigwa karibu kila sehemu, hadi kwenye ma bar, sema tukawa tunajiuliza Rose kapoteaje!? Hatukuoata jibu.

Kupotea si mbaya ila kama hakujiwekeza ki uchumi hapo ndio lazima ajute, sidhani kama Rose yule wa kipindi kile atarudi tena
 
Vyote umeongea hapo ila nami napenda kuwaambia Waafrika wenzangu Mungu hachezewi .Huyo bibie Mhando mpaka dalali Msama , mmeyaona ya Lusekelo ya kuumbuliwa asubuhi mapema.
 
Dahh, Rose yasije kumkuta kama yaliyomkuta Saida Karoli. Ukikutana na Mapromota wabaya lazima mwisho uwe mbaya. Hapa wameshaacha kumtukuza Muumba ameingia shetani. Bila aibu Promota anajaribu kumshusha chini Rose!!!
 
Huyu msama kazidi sasa ok hata kama anafanya inamhusu nini amwache dada wa watu kila siku kwenye magazeti! Kha!
 
Lakini ulivyoandika ujapangilia kwenye mtiririko mzuri mkuu
Wewe ndo Alex Msama nini.What matters is A message. Umekuwa mwana linguistic... Ebu rudisha Pesa za Rose Mhando.
 
hivi rose mhando ni mwanamuziki mpaka sasa au ameacha?
Anaimbaa Sema Msama kwa kutumia Pesa Zake anafanya asifanyiwe Hata Promo. Unaambia Rose Sasa analala njaa.Can you believe this tio such an incredible singer!!
 
Aisee yaan leo hii kuna watu nilipanda kwenye daladala wakawa wanaongelea Rose alivo kuwa amekamata muziki, huyo jamaa kipindi hiko alienda Zambia huko, mpakani na Zimbabwe anakwambia alikuta Rose nyimbo zake zinapendwa kweli, na zilikuwa zikipigwa karibu kila sehemu, hadi kwenye ma bar, sema tukawa tunajiuliza Rose kapoteaje!? Hatukuoata jibu.

Kupotea si mbaya ila kama hakujiwekeza ki uchumi hapo ndio lazima ajute, sidhani kama Rose yule wa kipindi kile atarudi tena
Sijui kama wananchi tumsaidieje.Kipaji anacho ila figisu nyiiingi
 
aisee,mungu atamsaidia huwa namkubali anafanya mziki mzuri sana ngoja mapromota waje najua watauelewa uzi wako mkuu .
Tuombe Mungu.Promota mzuri apatikane.Sio huyo Msama.Eti Rose Hana ubavu wa kujaza Diamond Jubilee. Hivi Anamjua Rose au anamsikia.Yule inatumia Pesa kushawishi atengwe..baada ya kumdhurumu
 
Daaah!! kwa kweli acheni Mwenyezi Mungu aitwe Mungu Mwenyezi....na mwenye haki ataipata tu....
 
Daaah!! kwa kweli acheni Mwenyezi Mungu aitwe Mungu Mwenyezi....na mwenye haki ataipata tu....
 
Kumbe ndo maana Rose aliimba wimbo unasema "Adui yangu aloo..."
sikujui kama nyuma ya wimbo huo yupo ndugu aliyetoka
mkoani kwa miguu na kudandia maloli mpaka Daresalama.
Kaosha masufuria ya mama ntilie kule feri ili apate msosi.

Nikuulize mtani wangu,hao waliokupa lifti kwenye malori yao
au hao mama ntilie nao wakijitokeza na kuanza kukunanga
kwenye vyombo vya habari utajisikiaje?

Kama kweli wewe ni mtu wa Mungu
lazima ukumbuke kila mtu ni mfano wa Yona
amewekewa samaki wake ili amfikishe ninawi.
Na kila mtu amewekewa Musa wake ili amtoe misri.
Hakuna mahali kwenye maandiko tunamuona samaki
akimtambia Yona kusema "kama si mimi ungekufa maji"
TAFAKARI CHUKUA HATUA.
 
Mtoa mada unaandika kama ngumbaru, anyway ni kweli Rose alishika sana enzi za 'Nibebe', hiyo ishu ya madawa na utapeli nimeisikia mara nyingi sijui ina ukweli kiasi gani
 
Sitaki kuaamini wala kukubali eti rose mwando anatumia madawa ya kulevya na nitakuwa wa mwisho kuamini, hapa Kuna kitu kimejificha.
 
Back
Top Bottom