PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,723
Ndugu wanaJF,Ndugu wana JF,
Tunasikitika kuwataarifu kuwa mwenzetu Lunyungu ambaye ni JF member, anaugua mno, hawezi kusimama wala kukaa, anaishi kwenye wheelchair.
His lower disc has been compressed ,ana maumivu makali sana na anasubiria operation.
Anasema anawamiss sana JF members na anamiss the forum.
Kwa yoyote anaetaka kuwasiliana nae, namba yake ni 0767 554433.
Uongozi wa Jf na kwa niamba ya members wote wa JF inampa pole sana na inamtakia afya njema na apone haraka.
Mungu mbariki na msaidie Lunyungu.
Natumai mnaendelea na mapambano!
Rejeeni quotation ya hapo juu, ambapo tulipewa hiyo taarifa na member(JamiiForums).
Kimsingi, nilimpigia Bwn Lunyungu kuwa ningeenda kumtazama jana[14/9/2010], na kweli alinielekeza kwake maeneo ya Njiro, nikafika, na kwa mara ya kwanza tangu dahari tukafahamiana!.
Kwakweli huyu ndugu jamani anaumwa!...amekuwa totally incapacitated, na ni wa kupewa msaada kwa kila movement anayohitaji...sina maneno zaidi ya kusema ANASIKITISHA!
Waswahili walishasema kwamba JASIRI HAACHI ASILI, huyu bingwa wa mabandiko katika mtandao huu, pamoja na kuongea kwa tabu alinieleza kuwa anawamiss sana members wote na jukwaa kwa ujumla, na akaulizia juu ya mada-moto zinazotamba sasa hivi, nami bila kukwepesha sura nikampa full-mazaga!
Aliendelea kunisimulia jinsi ambavyo huwezi kuelezea Historia ya JF bila kumtaja yeye, maana anasema alikuwa ni mtu wa 3(overall) kujiunga na JF, miaka ya 2006!
Bingwa huyu ni mtu mweledi wa juu sana wa siasa za Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla, na pamoja na maumivu ya mwili aliyo nayo hakukosea kitu katika stories zake!
Kwa ufupi alifurahia sana kutembelewa na mimi kama member, na alikiri kuwa wana-JF ni ndugu!
Back to his health. Lunyungu alikumbana na urasimu wa hatari huko Muhimbili, pamoja na kwamba alikuwa kwenye whee-lchair akiwa hoi!...anasema kuwa moyoni mwake anayo mengi sana ya kuandika juu ya watendaji hao wa hospitali kubwa kuliko zote nchini, pindi atakapopona.
Matokeo yake ni kwamba alikata shauri kwenda kutibiwa nje ya nchi, na anasafirshwa kesho(16/9).
Hujafa hujaumbika....Wana JF nawaombeni sana tumkumbuke huyu mpiganaji katika maombi yetu.
Lakini zaidi tuanzishe namna ya kusaidiana katika shida za namna hii...Lunyungu kwa sasa anaishi kwa madawa makali sana ya kutuliza maumivu, ambapo yana bei kali, nadhani kipato chake chote kinapitilizia huko!
Hatimaye muda wa saa2.30 za usiku niliagana na mwana-mabandiko huyu, nikimtakia kila la heri katika safari ndefu, lakini pia Afya NJEMA pindi atakapofanyiwa upasuaji huko ughaibuni.
Nawasilisha, na Mungu awabariki.
UPDATE ON LUNYUNGU's Health!:
Lunyungu amenipigia simu leo(20/09/2010, saa 9.00jioni hii) toka ughaibuni, akinipa maendeleo ya Afya yake!
Kimsingi nimefurahi sana kupata call yake!
Maendeleo ni kama hivi:
(1)Alifika salama huko eneo la (tukio) matibabu!
(2)Madaktari wa huko baada ya kumchunguza walitupilia mbali dawa zote alizopewa na madaktari wa Muhimbili na kumwanzishia dawa mpya.
(3)Waliikataa kabisa diagnosis iliyoandikwa na Muhimbili, na sasa hivi wanaendelea kum'observe, na bado hawajaestablish shida yake(wakati Bongo walimchunguza kwa dakika chache tu na kuamuru afanyiwe operation!)
(4)Wamechukua samples za makohozi na wanazifanyia kazi.
(5)Ijumaa hii anakutana na 'neurosurgeon' ambaye atamchunguza kwa umakini na kutoa majibu!
(6)Anasema kwa dawa anazotumia sasa hivi tu amepata improvement kubwa sana..Anaweza hadi kupiga mswaki na kunawa mwenyewe, huku akipiga hatua mbili-tatu za kutembea!
(Anamshukuru sana MUNGU, na pia anawashukuru sana wanaJF kwa sala zenu )
HESHIMA KWENU,
MUNGU AMPE AFYA NJEMA.