Albert Msando apotoka tena

Molemo, nitajie matusi yangu kwa Chama na Kamati Kuu. Nitaona aibu.

Ulinzi wa nini nahitaji? Unawapa sifa CCM wasizostahili hata kidogo. Katika maisha yangu CCM wangekuwa wameongea na mimi au wamenitumia kwa hata jambo moja wangejisifu sana. Hilo halitakaa litokee na wanajua hivyo.

Inawezekana kabisa wewe ni mwanaCCM unajidai Chadema kwa kusema uongo na uzushi ili ionekane kuna tatizo. Tunawashtukia na tutawakomesha. Ujanja wenu wa kuchonganisha kwa kutumia kivuli cha kutojulikana kimefika mwisho.

Hatuendekezi upuuzi. Na kama ni mwanachadema na unaamini unachosema nipigie simu unieleweshe na mimi nitakuelewesha. Hakuna sababu ya kujificha. Nitumie PM na nitajadiliana na wewe vizuri tu.

Ha..Ha..Haaa!!

Nijibu maswali yafuatayo..

Ni sahihi kwenda Serena Hotel kuzungumzia uliyoyazungumzia huku ukijua waandishi wa habari siyo walioshtaki hao waasi unaowatetea?

Pili Ukiwa kama Diwani wa Chadema ni sawa kabisa kufanya unachokufanya??

Kwanini nikupigie simu huku ukiwa wewe unatangaza mambo ya Chadema Serena Hotel??

Unapinga vijana wa UVCCM hawakuwa wanaratibu watu waliokuwa wanaingia mkutanoni Serena??

Huoni wanachadema makini wamekosa Imani na wewe??

Kwa hiyo ulivyoandika unakomesha tabia unayoisema ndani ya Chadema unamaanisha unakomesha tabia ya Mbowe,Dr Slaa na Kamati Kuu??.

Tuanzie hapo Mkuu..
 
ni kwel uliyoyasema..yule si mwanasheria...kwanza ni mwanachama wa ccm..jambo lingine inakuaje kwenye kikao zito na wenzake wakubali kuwa wamekosea halafu et huku nje anakana?? Kwan sis watoto??? Na iweje badala ya kujibu tuhuma anatafuta mwanasheria na kukata rufaa? Kwan alifukuzwa uanachama??? Yaan we upewe barua kazin ya kujieleza kufanya makosa,badala ya kujib tuhuma et unakata rufaa? Utakataje rufaa wakat hujahukumiwa?? Kusimamishwa uongoz si kufukuzwa uanachama..kuna tofaut ya kusimamishwa kazi au uongoz ili kupisha uchunguzi au kujitetea na kufukuzwa kazi au uanachama...zito na wenzake wamesimamishwa na kupewa barua wajibu tuhuma na wafike mbele ya kamat kuu kujieleza,badala yake wamekata rufaa huku mwingine (mwigamba) akikimbilia kwa msajili akilia asaidiwe,hiv si kuchochea kufukuzwa uanachama??? Wanang'ang'ania nn chadema?????


Unapotibua mzinga wa nyuki huwapangii pa kuruka na pa kutua!!!!
 
na wewe uwe unasoma ukaelewa sentensi ama nikurudishie quotations??
huyo mdau alizodoa kwamba kuvuviwa limekosewa na si kwamba hajui maana yake
tena alisema kana kwamba he was sure kwa kudai "" ETI NA WEWE UWE UNAANDIKA VIZURI SASA KUVUVIWA NDO KISWAHILI GANI"" wewe hapo ungeelewaje??

kimsingi bado mnachemka sana
Alizodoa nalo lipo kwenye kamusi ya Kiswahili...
Wanafunzi wako wanapata tabu sana.
 
hahahhahhaah!!!!!!!!!ukiona neno nimelitumia jua najua sio tu maana bali hata historia yake kwamba lilitoholewa wapi na msingi wake ni upi.
mie ni malkia nwa kiswahili fasaha uliza uambiwe dogo usikurupuke..........
nwa nalo ni kiswahili kazi kweli kweli...
 
Msando Albert,

Ikithibitika kuwa taratibu hazikufuatwa, je hiyo itafuta tuhuma walizopewa Zitto na wenzake? Na hivyo kufuta nia (intention) ya Kamati Kuu kuwaadhibu Zitto na wenzake? Hata wakimrejeshea Zitto nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu, atafanyaje kazi na timu ambayo inaamini kuwa Zitto ni msaliti? How will he fit in? Katika hali hiyo, chama kitaimarika vipi?

Na ukiacha taratibu, hizo tuhuma 11 ni zipi na majibu yake ni yapi? Sina hakika kama kwenye taarifa yako ya jana ulijibu tuhuma 11. Did you? If not, I am inclined to believe it was strategic. Kwa nini hizi tuhuma 11 zisiwekwe wazi ili wote tupime uzito wake? Mwenye kuzifahamu hizi tuhuma, tafadhali.

Tuhuma dhidi ya Zitto ni kutokana na Waraka wa Mwigamba ambao unasemekana ni Mkakati wa Ushindi wa Uchaguzi wa ndani ambao uliandaliwa kwa siri.

Mkakati huo kutokana na maudhui yake unasemekana kukashifu viongozi, kutoa tuhuma za uongo, kujenga makundi, kuchonganisha wanachama na viongozi na kutaka nafasi za uongozi bila kufuata utaratibu.

Lengo langu ni kuhakikisha taratibu tulizojiwekea zinafuatwa. Endapo ukiukaji wake unasababisha haki isitendeke na isionekana imetendeka hatuna budi kukubali kwamba tumekosea na kuchukua hatua stahiki kurekebisha.

Lazima tuaminiwe kwamba tunafuata Katiba na Kanuni zetu kama chama. Tunapokosea turekebishe. Sio dhambi kujirekebisha ukikosea. Ni ukomavu.
 
Mwaikenda,

1. Kutetea utawala wa Sheria na tafsiri sahihi ya Katiba yetu ni kubomoa chama? Ndio mimi ni Diwani lakini itakuwa ajabu sana kusema kwamba kumtetea Zitto lazima nijiuzulu kwanza. Mimi sio mjumbe wa Kamati Kuu, Baraza Kuu wala Mkutano Mkuu. Mgongano wa maslahi unatoka wapi? Naweza vipi kuathiri maamuzi ya vikao hivyo?

2. Je marekebisho ya Kanuni ya 2013 yalijumuisha kwamba kukiwa na dharura utaratibu uliotajwa kwenye kipengele (a) usifuatwe? Kwa nini kipengele kilichoongezwa cha (d) kilitaja utaratibu ambao hautafuatwa ni ule wa (b) na (c) peke yake? Hilo unalielezeaje?

3. Kikao cha Kamati Kuu kilikuwa kikao cha dharura? Waraka husika ulikamatwa siku hiyo hiyo ya kikao au jana yake kwa hiyo ikabidi maamuzi ya dharura yafanyike?

Kama ilikuwa ghafla hivyo kwa nini asingesimamishwa uongozi, apewe mashtaka kama Kanuni inavyosema halafu asikilizwe kwa dharura na adhabu itolewe ya kumvua uongozi? Dharura sio haraka kaka.

4. Kupewa taarifa rasmi kwa maandishi na mwenendo kupelekwa Baraza Kuu ni taratibu ambazo lazima zikamilike ili muadhibiwa aweze kukata Rufaa. Ndio maana taarifa ya nia imetolewa ili taratibu hizo zikamilike. Hakuna niliposema nataka mwenendo wa shauri. Tunachotaka ni taarifa rasmi ya maamuzi.

5. Mwenendo unatakiwa umefika Baraza Kuu ndani ya siku 14 toka tarehe 22/11/2013. Je umefikishwa?

Tusijadili kwa jazba na hasira. Mimi kueleweshwa kwa hoja ni mwepesi sana. Fanya hivyo na kama uko sahihi nitaconcede. Lakini sitaconcede kisa tu utasema akili au uelewa wangu mdogo.

Ahsante.
dharura sio haraka.......... naomba kunukuu
 
Naona CHADEMA FAMILY mkiongozwa na babu wa kulike mnavyomshambulia Msando, Hivi nyie na akili zenu kweli mlitaka Msando asimtete Zitto kisa eti yeye ni mwanachadema?! Kama hamjui Msando hapo yupo kazini hiyo ni taaluma yake. CHADEMA FAMILY hebu jitahidini kufanya walau kidogo tu kile mnachowaambia CCM (kutenganisha taaluma na siasa) Uwakili ni taaluma ya Msando jamani na hacheki upumbavu (Stupidity= lack of knowledge) wenu wa kumtishia kumfukuza.
Alafu eti mnapiga makelele eti kwanini alienda kusemea kwenye press conference kwa hiyo yeye hana haki ya kutumia press conference ila Mnyika na Lissu wana haki!
Zitto ni public figure na CHADEMA imegawanyika mara mbili CHADEMA FAMILY na CHADEMA HALISI nyie mambo yenu ya kifamilia yafanyieni huko huko kwenye familia yenu mkiwa mmejifungia chumbani/sebuleni but CHADEMA HALISI mambo yake ni ya wazi kwa jamii, na hii isssue iende hivi hivi ili mwisho wa siku public tujue mchele ni upi na pumba ni zipi!
 
Ben, nakubaliana na hoja ya vichaka vitatu. Kwanza haujui kama huyo aliyesema hayo maneno sio mwanachadema brother. Sio kila anayekosoa sio mwenzetu.

Pili, hoja yangu ni nyepesi sana. Ingeweza kujibiwa kwa NDIO au HAPANA.

Kwamba, je Kanuni zimefuatwa au la. Badala yake hoja inahama na kufanywa ni tatizo kati ya Albert na wanachadema wenzake au Albert na Chadema.

Na kuhamishwa huko kunafanywa makusudi na wale ambao ndio adui zetu. Wanajenga chuki kati yetu wanatuacha tuparuane.

We need to take a step back and think. And after all it's not as bad as its made to look. But only if we both wake up and stop it. My cent.

Albert,

Aya ya kwanza,Sijui huu upotoshaji una malengo gani.Hakuna mahali popote nilikosema anayetukosoa ni mwenzetu au si mwenzetu.

Hujajibu swali langu kuwa je,wewe kama mwanachadema halisi unayejua kanuni,maadili,itifaki na katiba ya CHADEMA unakubaliana na hizo rhetorics za vichaka vitatu?To me that's just another rhetorical hogwash.Wewe umekwepa kujibu

Pili,Utamtenganishaje Albert na wale wanaokidhalilisha chama kwenye media badala ya kufuata kanuni na taratibu?Yaani ushiriki mchezo huu moja kwa moja halafu unalaumu watu kufanya mjadala kuwa Albert na CHADEMA?

Albert,Wewe ni Msomi na unajua impact ya unachofanya katika Jamii na kama mwanasiasa unajua madhara ya unachofanya.Hao maadui zetu unawalaumu kama njia ya ku-blind watu na kutaka ku-divert attention na attitude za watu towards reality ya kile unachofanya/mnachofanya.

Hao maadui zetu wewe na wateja wako ndio mnawapa platform hii na hata hapa wanakupa sapoti na kuandika maaneno unayokubaliana nayo.Watu hao siku zote wapo huku wakiitukana CHADEMA,Pia nenda kasome magazeti ya maadui zetu uone jinsi walivyoshikilia bango haya mliyoyafanya jana pale Serena Hotel.Leo kweli unawalaumu maadui zetu?

Hebu tufikie hatua tuache unafiki.

By the way,Kulikua na haja gani ya wewe kwenda kufanya Press Conference badala ya ku-address hili ndani ya vikao?Kama wewe ni Mwanasheria wao tena kwa bahati nzuri ni Diwani,ni kiongozi na Mwanachama hai Wa CHADEMA,kwanini usifuate taratibu na hata kama ni utetezi ukaupeleka kwenye vikao?

Leo unalaumu wanaokushambulia?Hebu tuache unafiki Brother na tuweke maslahi ya taasisi juu ya urafiki.

Hebu Tuwe principled sasa!
 
Tuhuma dhidi ya Zitto ni kutokana na Waraka wa Mwigamba ambao unasemekana ni Mkakati wa Ushindi wa Uchaguzi wa ndani ambao uliandaliwa kwa siri.

Mkakati huo kutokana na maudhui yake unasemekana kukashifu viongozi, kutoa tuhuma za uongo, kujenga makundi, kuchonganisha wanachama na viongozi na kutaka nafasi za uongozi bila kufuata utaratibu.

Lengo langu ni kuhakikisha taratibu tulizojiwekea zinafuatwa. Endapo ukiukaji wake unasababisha haki isitendeke na isionekana imetendeka hatuna budi kukubali kwamba tumekosea na kuchukua hatua stahiki kurekebisha.

Lazima tuaminiwe kwamba tunafuata Katiba na Kanuni zetu kama chama. Tunapokosea turekebishe. Sio dhambi kujirekebisha ukikosea. Ni ukomavu.


Patriotism!!!!!!

Be blessed
 
Ha..Ha..Haaa!!

Nijibu maswali yafuatayo..

Ni sahihi kwenda Serena Hotel kuzungumzia uliyoyazungumzia huku ukijua waandishi wa habari siyo walioshtaki hao waasi unaowatetea?

TAARIFA YANGU KWA UMMA KUPITIA WAANDISHI HAIKUWA UTETEZI. ILIKUWA KUELEZA HATUA AMBAZO ZIMECHUKULIWA NA ZITTO NA KWANINI.

NI BAADA YA ZITTO KUWA AMEWASILISHA UTETEZI WAKE WA MAANDISHI KAMATI KUU.

Pili Ukiwa kama Diwani wa Chadema ni sawa kabisa kufanya unachokufanya??

NAAMINI KWAMBA MWANACHADEMA LAZIMA ATETEWE NA MWANACHADEMA KWA MASUALA YA CHAMA. SASA KAMA KUMTETEA MWANACHADEMA LAZIMA NIJIUZULU UANACHAMA KWANZA ITAKUWA AJABU SANA. AU KWAMBA NIJIUZULU UDIWANI NDIO NITETEE UKIUKWAJI WA KANUNI ITAKUWA NI CHAMA CHA AJABU SANA.

HATA VIONGOZI WANGU WANALIJUA HILO.

MBONA SIKUAMBIWA NIJIUZULU UANACHAMA NDIO NIWATETEE MH MWENYEKITI, MH Ndesamburo nk KWENYE KESI ZA UCHAGUZI AMBAZO ZOTE TULISHINDA?

AU HAKUKUWA NA CONFLICT OF INTEREST KUMTETEA MGOMBEA WA CHADEMA WAKATI MIMI NI DIWANI WA CHADEMA?

Kwanini nikupigie simu huku ukiwa wewe unatangaza mambo ya Chadema Serena Hotel??

NIPIGIE SIMU KAMA LENGO LA DHATI NI KUREKEBISHANA NA KUTATUA MATATIZO YETU YA CHAMA. TUJIBIZANE HAPA NA KUTUKANANA KAMA LENGO NI TOFAUTI. UMESHUHUDIA MATUSI NA KASHFA ZINAZOTOLEWA DHIDI YANGU. SIJUI ZINASAIDIA NINI HATA KAMA INGEKUWA KWELI NIMEKOSEA AU SINA HOJA.

Unapinga vijana wa UVCCM hawakuwa wanaratibu watu waliokuwa wanaingia mkutanoni Serena??

HAKUNA KIJANA WA UVCCM ALIRATIBU MKUTANO WANGU JANA. SIMJUI KIJANA YEYOTE WA UVCCM ALIYEFANYA HIVYO. SINA SABABU YA KURATIBIWA MKUTANO NA UVCCM KAKA.

Huoni wanachadema makini wamekosa Imani na wewe??

HAPANA. NAONGEA NA WANACHADEMA WENGI TU NA WANAELEWA KIPINDI TUNACHOPITIA. WANAONIFAHAMU KWA KARIBU WANAJUA NASIMAMIA NINI. KWA WALE AMBAO WANACHANGIA KWA USHABIKI WANAKOSA IMANI KWA KUTOKUFAHAMU.

Kwa hiyo ulivyoandika unakomesha tabia unayoisema ndani ya Chadema unamaanisha unakomesha tabia ya Mbowe,Dr Slaa na Kamati Kuu??.

NIMESEMA TUNAKOMESHA TABIA YA WATU HUMU KUJIDAI NI WANACHADEMA ILHALI NI CCM NA LENGO LAO NI KUTUCHONGANISHA ILI TUGOMBANE WENYEWE KWA WENYEWE.

MBOWE NA SLAA NI VIONGOZI WA KITAIFA NA JANA UMESIKIA NIMETOA RAI KWAMBA WANACHAMA WAWAHESHIMU NA WAWE WATULIVU KWA SABABU TAYARI HATUA ZIMECHUKULIWA KUKATA RUFAA NA KUTOA UTETEZI.

Ni vigumu kiasi gani kuona nini najaribu kufanya?

Tuanzie hapo Mkuu..

Tumeanzia hapo kiongozi. Nasubiri maelekezo
 
Nadhani wewe ndio unatakiwa kutiliwa mashaka uwezo wako wa kuelewa sheria maana unaonegea mambo ya kusikia pasipo kuwa na facts. Kwenye huo waraka kuna mahali popote jina la Zitto Kabwe limetajwa? Hata kama lingekuwa limetajwa kuna ushahidi kuwa alihusika kuuandaa? Leo mimi nikiandaa waraka nikaweka jina la Mbowe utalazimisha kuwa Mbowe anaufahamu? Mbona CDM wanataka watu waamini kuwa Video ya Lwakatare ni ya kutunga lakini haohao hawataki kukuli kuwa ZZK hausiki na kuandaa waraka Leta ushahidi kuwa alihusika kuandaa nasi tutakuamini.

Jaribu kuwa great thinker acha kusukumwa na chuki binafsi, mhukumu mtu basing on facts beyond reasonable doubts siyo kwa kusikia story za kwenye vijiwe vya kahawa.

Capito, lakini si walikiri kuuandaa huo waraka, je unataka kutushawishi kwamba waraka ule uliandaliwa na wakasingiziwa? Halafu si anasema ZZK hakupewa mashitaka yake kabla aliyakuta kwenye kikao, kwani alikuwepo kikaoni?
 
Back
Top Bottom