Yeyote anayejiuliza maswali kadhaa kuhusu uongozi katika nchi yetu, haya ni moja ya maswali yatakayomtatiza:1. Je kulikuwa na haja ya Rais kuanza mchakato mpya na vyama vya siasa kuhusu muundo au mchakazo wa kuunda kwa Katiba mpya akiwa Ikulu??2. Je ni sahihi kwa Bunge kama mhimili mwingine wa uongozi wa nchi kuwa na tofauti za wazi kuhusu maswala mihumu wa kiushirikiano? Hapa swala la posho za wabunge na danadana katika ofisi ya Bunge yenyewe na sasa na taasisi ya Urais. Majibu:1. JK amekosa ushawishi kwa mihimili mingine na sasa kila kiongozi anafanya analotaka na analoamua bila ushirikiano na wengine. Rais hawezi kuweka sahihi muswada ili uwe sheria halafu akarudi nyuma kutaka mabadiliko ya sheria hiyo kabla hata haijaanza kufanya kazi. Angejua hilo angeweka ushawishi wake kwa Spika ili mawazo ya wengine yasikilizwe na watu sahihi.2. Bunge na taasisi ya Urais lazima vifanya kazi pamoja. Rais ananukuliwa hata na Waziri Mkuu na Spika, lakini taasisi yake inajitokeza na kusema hizo nukuu si sahihi. Hivi kweli yote mawili yanaweza kuwa ni kweli?? Hapana, ni moja ndio sahihi au yote sio sahihi. Kinachotokea sasa kuhusu posho kinaacha maswali mengi na nyeti kuliko majibu wala hizo fedha!!Ombwe la Uongozi ndio janga la Taifa Tanganyika. Sio maradhi, njaa, magonjwa na umasikini!!!