decomm
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 726
- 655
Amani iwe kwenu.
Katika uzi huu tutakuwa tunajifunza / kukumbushana alama na michoro ya barabarani za SADC.
Alama na michoro hii ipo takribani 178.
Leo nitaanza na mchoro namba 173 na 174.
Hii ni mistari inayokaribia kufanana lakini ina maana tofauti kabisa ambapo medereva wengi huichukulia kama yote ni kama namba 174 (kwa maana ya kwamba mstari #173 madereva wengi hawaujui na pia hao wachoraji barabarani hukosea kuichora ipasavyo)
#173 ni mstari wa ONYO / TAHADHARI, unaelekea UKANDA WA HATARI (hivyo usiovateki)
#174 ni mstari unaotenganisha njia ya kuendeshea katika barabara (unaruhusiwa kuovateki kama ni salama)
Pia madereva wengi wamekaririshana kwamba mistari ya dash dash unaruhusiwa kuovateki ambapo si muda wote ni sahihi.
Sehemu kama IYOVI (Mikumi - Ruaha Mbuyuni) mistari hii ilitakiwa ionekane waziwazi, lakini ni sehemu chache sana imechorwa kwa usahihi.
Leo wewe umepata bahati ya elimu hii basi ifuatilie, kisha uelimishe na madereva na watumia barabara wengine.
Nimeambatanisha picha ya mistari hivyo kama inavyooneshwa kwenye 'high way codes' ama kwenye vitabu vya mafunzo ya udereva.
___
#Usalama barabarani ni jukumu letu sote.
__
D.
Katika uzi huu tutakuwa tunajifunza / kukumbushana alama na michoro ya barabarani za SADC.
Alama na michoro hii ipo takribani 178.
Leo nitaanza na mchoro namba 173 na 174.
Hii ni mistari inayokaribia kufanana lakini ina maana tofauti kabisa ambapo medereva wengi huichukulia kama yote ni kama namba 174 (kwa maana ya kwamba mstari #173 madereva wengi hawaujui na pia hao wachoraji barabarani hukosea kuichora ipasavyo)
#173 ni mstari wa ONYO / TAHADHARI, unaelekea UKANDA WA HATARI (hivyo usiovateki)
#174 ni mstari unaotenganisha njia ya kuendeshea katika barabara (unaruhusiwa kuovateki kama ni salama)
Pia madereva wengi wamekaririshana kwamba mistari ya dash dash unaruhusiwa kuovateki ambapo si muda wote ni sahihi.
Sehemu kama IYOVI (Mikumi - Ruaha Mbuyuni) mistari hii ilitakiwa ionekane waziwazi, lakini ni sehemu chache sana imechorwa kwa usahihi.
Leo wewe umepata bahati ya elimu hii basi ifuatilie, kisha uelimishe na madereva na watumia barabara wengine.
Nimeambatanisha picha ya mistari hivyo kama inavyooneshwa kwenye 'high way codes' ama kwenye vitabu vya mafunzo ya udereva.
___
#Usalama barabarani ni jukumu letu sote.
__
D.