Alama hizi za speed limit highway ya Ubungo hadi Kibamba zipo sahihi?

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
Highway ya kuanzia Ubungo mataa hadi Kibaha ipo katika hatua za mwisho kukamilika. Ni barabara nzuri sana yenye upana na nafasi ya kutosha kupitisha idadi kubwa ya magari bila kusababisha usumbufu miongoni mwa watumiaji wa barabara hiyo

Hata hivyo kuna hii kero ya alama za speed limit za 50kph kila baada ya hatua kadhaa! Pamoja na kuwepo vibao vingi kuonyesha 50kph hakuna vibao vya kuonyesha ukomo wa katazo hilo au viko kwenye maeneo machache sana!

Bahati mbaya, askari wa usalama barabarani wanatumia vibao husika kutoza faini madereva wanaokiuka speed limit au kuchukua ya "ku brash viatu"

Swali langu ni kwamba kwenye highway kama ile ni sahihi kuwa na vibao kama vile kila baada ya kilometer moja au pengine chini ya hapo?

Dereva anapoona kibao ya 50kph atajuaje kwamba ameshafika mwisho wa katazo? Tena unaeza kuta unamaliza kibao kimoja cha 50 unakutana kingine cha 50kph!!!

Inawezekana barabara haijakabidhiwa kwa serikali kwa maana bado ipo kwenye matengenezo, sasa ni sawa kwa askari kukusanya "tozo"?

Kama ni sawa kwanini kwenye zile rush hours huwa wanahimiza madereva wakimbize magari bila kujali alama hizo ili kuepeusha foleni?

Mambo haya ndio yanafanya wananchi waamini maneno ya uvumi wa SIRI ILIYO WAZI kwamba askari wa usalama barabarani wanageuza madereva kua mtaji wao
 
Hivi unapitaje sehem yenye msongamano kama ubungo mataa kwa speed zaidi ya 50

Au Mtoa mada unazungumzia ubungo ya NJOMBE?
Mkuu, kuna kipande cha kuanzia Kimara Stop Over hadi Kibamba. Hapo hakuna msongamano na barabara inaruhusu hata 120kph

Hapo ndio traffic police wanakaa na tochi yao. Hawakai sehemu yenye msongamono kama unavyosema
 
Hapana atakuwa anazungumzia ile ya moshi kule kwenye kiwanda cha miwa
Kuna baadhi ya maeneo machache yenye msongamano kama pale Korogwe, Kimara mwisho na Mbezi mwisho ni sahihi kabisa kuweka speed limit maana hata kwa common sense tu dereva hawezi kwenda kasi maeneo hayo

Lakini sehemu hizo askari hawakai na tochi wala hawakamati waendao kasi! Askari wa tochi utawakuta kwenye kipande kuanzia Mbezi mwisho baada ya daraja, kuja Mbezi kwa Yusufu, Luguruni, Kibamba, Kikuvya hadi Kibaha Maili Moja. Maeneo hayo hakuna movement kubwa za watu
 
Kuna baadhi ya maeneo machache yenye msongamano kama pale Korogwe, Kimara mwisho na Mbezi mwisho ni sahihi kabisa kuweka speed limit maana hata kwa common sense tu dereva hawezi kwenda kasi maeneo hayo

Lakini sehemu hizo askari hawakai na tochi wala hawakamati waendao kasi! Askari wa tochi utawakuta kwenye kipande kuanzia Mbezi mwisho baada ya daraja, kuja Mbezi kwa Yusufu, Luguruni, Kibamba, Kikuvya hadi Kibaha Maili Moja. Maeneo hayo hakuna movement kubwa za watu
Mkuu askari wa kibongo achana nao, watakuumiza kichwa. Naomba niishie hapa tu mana naweza kujikuta nje ya mada na kukwaza watu.
 
Umaskini ni jambo baya sana. Unaweza kupewa kitanda na godoro lake zuri kabisa lakini ukasema linakuumiza na hivyo kuamua kulala sakafuni. Kuna watu nchi hii wana akili za kimaskini na roho mbaya hadi shetani anashangaa. Ndicho kinachotokea hicho kipande na barabarani kwa ujumla. Uzuri wa barabara umekosa maana kabisa.
 
Highway ya kuanzia Ubungo mataa hadi Kibaha ipo katika hatua za mwisho kukamilika. Ni barabara nzuri sana yenye upana na nafasi ya kutosha kupitisha idadi kubwa ya magari bila kusababisha usumbufu miongoni mwa watumiaji wa barabara hiyo

Hata hivyo kuna hii kero ya alama za speed limit za 50kph kila baada ya hatua kadhaa! Pamoja na kuwepo vibao vingi kuonyesha 50kph hakuna vibao vya kuonyesha ukomo wa katazo hilo au viko kwenye maeneo machache sana!

Bahati mbaya, askari wa usalama barabarani wanatumia vibao husika kutoza faini madereva wanaokiuka speed limit au kuchukua ya "ku brash viatu"

Swali langu ni kwamba kwenye highway kama ile ni sahihi kuwa na vibao kama vile kila baada ya kilometer moja au pengine chini ya hapo?

Dereva anapoona kibao ya 50kph atajuaje kwamba ameshafika mwisho wa katazo? Tena unaeza kuta unamaliza kibao kimoja cha 50 unakutana kingine cha 50kph!!!

Inawezekana barabara haijakabidhiwa kwa serikali kwa maana bado ipo kwenye matengenezo, sasa ni sawa kwa askari kukusanya "tozo"?

Kama ni sawa kwanini kwenye zile rush hours huwa wanahimiza madereva wakimbize magari bila kujali alama hizo ili kuepeusha foleni?

Mambo haya ndio yanafanya wananchi waamini maneno ya uvumi wa SIRI ILIYO WAZI kwamba askari wa usalama barabarani wanageuza madereva kua mtaji wao
Hiyo barabara imejaa taksima yana haina 90%,na ukiwa dreva sio mzoefu ajali ni fasta
 
Back
Top Bottom