Alabuliwa Risasi Ya Makalio Akizini Ndani Ya Gari

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,809
Alabuliwa Risasi Ya Makalio Akizini Ndani Ya Gari



Jeshi la polisi limekumbwa na kashfa nyingine baada ya askari wake kudaiwa kumpiga risasi msichana wa miaka 16 baada ya kumkuta akivunja amri ya sita ndani ya gari.

Msichana huyo alikumbana na mkasa huo Jumatano usiku eneo la Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam, aalipopigwa risasi sehemu ya makalio wakati akijaribu kuwakimbia polisi kwa kutumia gari la mpenzi wake.

Mpenzi huyo alikamatwa na kuwekwa mahabusu na kufunguliwa kesi ya ubakaji.

Akizungumza na NIPASHE Jumapili jana katika wodi ya Hospitali ya Temeke alikolazwa, msichana huyo alisema siku ya tukio alikutana na kijana huyo majira ya saa 8:00 usiku katika baa moja inayoitwa Kindau na kukubaliana kwenda kushiriki tendo la ndoa kwa malipo ya Shilingi 20,000.

Alisema kutokana na muda huo kuwa usiku sana hawakuweza kwenda katika nyumba ya kulala wageni na badala yake walikwenda eneo la Zakhem na kisha walipaki gari kwenye uchochoro na baadae walianza kubanjua amri ya sita.

Wakiwa kwenye kilele cha mapenzi yao, ghafla walishtukia gari la polisi likiwajia kwa kasi kwa nia ya kuwakamata, “Tuliagana anilipe elfu ishirini wala hakunibaka kama anavyodai, wao polisi walitukuta tayari tunamaliza lakini kutokana na woga tulikimbia ili tusikamatwe,” alisema msichana huyo.

Alisema wakati wanakimbia kwa kutumia gari la mpenzi wake askari mmoja alifyatua risasi iliyopenya kwenye taa ya gari na kwenda kumjeruhi sehemu ya makalio yake, “Nilisikia mlio mkubwa wa bunduki, ghafla nilihisi kitu kimeingia mwilini mwangu na kuishiwa nguvu,” alisema kwa uchungu.

Alisema kwa kuona hali hiyo, mpenzi wake alisimamisha gari kwa kujisalimisha na polisi walipowafikia walimtaka mpenzi wake huyo atoe pesa kama malipo ya kitendo chao cha kukutwa wakifanya mapenzi ama sivyo watampeleka kituoni.

Alieleza kuwa mpenzi wake hakuweza kutoa pesa hizo ndipo walipoamua kumpiga na kumpeleka kituo cha polisi cha Mbagala na yeye alifikishwa hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, ndugu na jamaa wa mpenzi wake wanapinga hatua ya polisi hao kutumia nguvu kubwa kama watu hao walikuwa watuhumiwa wa ujambazi.

Wakizungumza wakiwa kwenye kituo cha Polisi cha Mbagala kufuatilia hatma ya ndugu yao, ndugu hao ambao hawakutaka majina yao yatajwe gazetini walisema hatua ya polisi kupiga risasi huku wakitambua watu hao sio majambazi ni kitendo cha kinyama, “Tunachoshangaa ni kwa nini polisi wapige risasi wakati wakijua hawakuwa majambazi ila walikuwa wakifanya mapenzi, hata hilo jalada la kesi walilofungua wanataka kuficha maovu yao na sio vinginevyo,” alisema ndugu mmoja ambaye alijitambulisha kuwa shemeji yake.

Alisema kimsingi tukio hilo lilikwenda katika makubaliano yao na sio ubakaji kama wanavyodai, ila kinachofanyika kwa sasa ni kutaka kumlinda Askari mwenzao aliyejeruhi kwa risasi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, David Misime, alipopigiwa simu kuelezea tukio hilo, alisema kwa sasa hawezi kulizungumza kwa kuwa yupo nje ya Mkoa kikazi.

Source :- Nipashe Jumapili
 
It clearly looks like was a consensus among the two, so how did police get into and opened fire to the girl? There is apparently covering up of some of the information which could otherwise reveal the police weaknesses.
 
How kud it be possible to shoot the girl who was being raped instead of shooting a man? This is rediculous
 
How kud it be possible to shoot the girl who was being raped instead of shooting a man? This is rediculous
Did u read the story..!?

Wakiwa kwenye kilele cha mapenzi yao, ghafla walishtukia gari la polisi likiwajia kwa kasi kwa nia ya kuwakamata, "Tuliagana anilipe elfu ishirini wala hakunibaka kama anavyodai, wao polisi walitukuta tayari tunamaliza lakini kutokana na woga tulikimbia ili tusikamatwe," alisema msichana huyo.
 
How kud it be possible to shoot the girl who was being raped instead of shooting a man? This is rediculous

Hakuwa anabakwa kulingana na habari yenyewe inavyosema, hata hivyo ni upuuzi tu hata kama angepigwa risasi mwanamke ama mwanamme katika hali kama ile.
 
Wawache zinaa na kujiuza.

Halafu wasingekimbia, kilichowakimbiza ni nini? inaonesha polisi walikuwa wakiipiga risasi gari ili isimame na bahati mbaya risasi ikapenya na kumtandika makalio huyo kijana.

Wanaume kutembea na msichana wa miaka kumi na sita ni kosa Tanzania? au akiwa anasoma tu? kwani najuwa kuwa si kosa kuolewa wa miaka kumi na sita na hata wa miaka kumi na nne, labda sheria za ndoa ziwe zimebadilishwa.
 
Sheria ya ndoa inasema msichana wa miaka 15 ana weza funga ndoa na wakati sheria ya ubakaji Tanzania inasema ukimtafuna msichana mwenye umri chini ya miaka 18 unakuwa umebaka. Kwenye sheria kuna tatizo na magamba wanayaona haya na hawataki kubadilisha sijui kwanini ndio upuuzi wao huu sijui kipi hawakioni hapo. Ila kutumia nguvu kwenye kupiga risasi huku wakiwa hawana ushahidi nalo ni tatizo kubwa sana.
 
Wawache zinaa na kujiuza.

Halafu wasingekimbia, kilichowakimbiza ni nini? inaonesha polisi walikuwa wakiipiga risasi gari ili isimame na bahati mbaya risasi ikapenya na kumtandika makalio huyo kijana.

Wanaume kutembea na msichana wa miaka kumi na sita ni kosa Tanzania? au akiwa anasoma tu? kwani najuwa kuwa si kosa kuolewa wa miaka kumi na sita na hata wa miaka kumi na nne, labda sheria za ndoa ziwe zimebadilishwa.
huyo mwanamke alikuwa bar...wazazi wake wako wapi? huu ni mfumo duni wa ccm ..mtoto han la kufanya anajiuza..who to blame? CCM and no one else....offcourse kutembea na underage ni kosa kisheria, mteja kaenda bar kakuta malaya kamnunua..au siku hivi wanawake (machangudoa) wanaandikwa miaka yao vifuani?..ccm mnatupeleka wapi? i cant wait hili li CCM kufa
 
huyo mwanamke alikuwa bar...wazazi wake wako wapi? huu ni mfumo duni wa ccm ..mtoto han la kufanya anajiuza..who to blame? CCM and no one else....offcourse kutembea na underage ni kosa kisheria, mteja kaenda bar kakuta malaya kamnunua..au siku hivi wanawake (machangudoa) wanaandikwa miaka yao vifuani?..ccm mnatupeleka wapi? i cant wait hili li CCM kufa
Hata ili nalo mnalaumu CCM...! Dah! Kazi kweli kweli.
 
Kufanya malovedove na mtoto under 18 ,ubakaji though pia nadhani polisi hawakuwa na nia ya kumlabua huyo bint risasi it seems that walitaka watoboe tyre then wawadai kitu kidogo !!!!!!!!!! mi mwenyewe nshawahi kukoswa risasi bar walitukuta nyt kali af wakadai kitu, kidogo wakabeba viti tulivyokomaa nao wakawakaanza fyatua risasi!!! Wanadai ati timevnja sheria weee tulivyozidisha jeuri wakasema et tulitaka kuwapora silaha!!! Waroho sana ndo mana wkt mngne wanavka mipaka
 
huyo mwanamke alikuwa bar...wazazi wake wako wapi? huu ni mfumo duni wa ccm ..mtoto han la kufanya anajiuza..who to blame? CCM and no one else....offcourse kutembea na underage ni kosa kisheria, mteja kaenda bar kakuta malaya kamnunua..au siku hivi wanawake (machangudoa) wanaandikwa miaka yao vifuani?..ccm mnatupeleka wapi? i cant wait hili li CCM kufa

Ndio maana Serikali ya CCM imeamuwa kutengezesha vitambulisho vya uraia ambapo bar wataweza kuthibitisha umri wa anaeingia hapo bar kama wanavyofanya nchi zingine. Kwa sasa tumlaumu Nyerere aliyekuwa hataki tuwe na vitambulisho vya uraia.
 
It clearly looks like was a consensus among the two, so how did police get into and opened fire to the girl? There is apparently covering up of some of the information which could otherwise reveal the police weaknesses.

How kud it be possible to shoot the girl who was being raped instead of shooting a man? This is rediculous
Hoja ya kiswahili inajibiwa kwa kiswahili someni tena mtaelewa ndipo muulize kwa mshangao tena... Kha!

wao polisi walitukuta tayari tunamaliza lakini kutokana na woga tulikimbia ili tusikamatwe,” alisema msichana huyo.(Msichana alijua kosa lake) Kipolisi ni kosa na Sheria inamtaka atumia arm kumsimamisha kwa ishara kwanza then risasi chini ya kiuno,

Alisema kwa kuona hali hiyo, mpenzi wake alisimamisha gari kwa kujisalimisha na polisi walipowafikia.

Huelewi na Majibu yote yapo hapo hapo au mleta habari aandike kwa English?

Wawache zinaa na kujiuza.

Halafu wasingekimbia, kilichowakimbiza ni nini? inaonesha polisi walikuwa wakiipiga risasi gari ili isimame na bahati mbaya risasi ikapenya na kumtandika makalio huyo kijana.

Wanaume kutembea na msichana wa miaka kumi na sita ni kosa Tanzania? au akiwa anasoma tu? kwani najuwa kuwa si kosa kuolewa wa miaka kumi na sita na hata wa miaka kumi na nne, labda sheria za ndoa ziwe zimebadilishwa.
Zinaa hawawezi acha hadi goverment irekebishe uchumi wa ukweli sio wa vitabuni na hii ni urithi wa Dunia Zinaa alianza Hawa

Bahati mbaya! hiyo ni kawaida ya Polisi wetu kusingizia hilo Tuliona kwa Zombe walipiga Juu kwa bahati mbaya zikampata nadhani risasi zao huwa zinaenda juu na kutua kwenye target.

Wanaume kutembea na msichana chini ya miaka 18 ni kosa la ubakaji hat kama amemuoa hii sheria ilishadadiwa nchi nzima ilifahamu na ubakaji ulipungua pengine jk ndio hakujua hilo akidai ni kiherehere chao.

Hao Jamaa ni uzembe wao kutowapoza hao polisi sheria itawashika wote.

Chenge pekee ndio anaweza fanya kosa kisha akaishinda sheria akawa huru Bisha
 
Tuache mambo ya ushabiki na kuweka kila kwenye mambo ya kisiasa hivi ni kweli hao wazinzi waliambiwa wafanye hivyo na ccm? au hao polisi walipewa amri ya kufyatua risasi na ccm? Malaya ni malaya tu hata wakiwa ulaya na hawawezi kuacha hata kama wakipewa kazi ikulu wataendeleza umalaya hata na walinzi au wafagiaji ni tabia chafu na malezo mabaya ya wazazi wao.
 
Ndio maana Serikali ya CCM imeamuwa kutengezesha vitambulisho vya uraia ambapo bar wataweza kuthibitisha umri wa anaeingia hapo bar kama wanavyofanya nchi zingine. Kwa sasa tumlaumu Nyerere aliyekuwa hataki tuwe na vitambulisho vya uraia.
FF hayo ni mawazo mgando...kwa hiyo tumlaumu nyerere kwa vie kulikuwa hakuna internet kipindi chake?
 
Tuache mambo ya ushabiki na kuweka kila kwenye mambo ya kisiasa hivi ni kweli hao wazinzi waliambiwa wafanye hivyo na ccm? au hao polisi walipewa amri ya kufyatua risasi na ccm? Malaya ni malaya tu hata wakiwa ulaya na hawawezi kuacha hata kama wakipewa kazi ikulu wataendeleza umalaya hata na walinzi au wafagiaji ni tabia chafu na malezo mabaya ya wazazi wao.
pigia mstari hapo....na ina maana hujui sababu ni nini?
 
FF hayo ni mawazo mgando...kwa hiyo tumlaumu nyerere kwa vie kulikuwa hakuna internet kipindi chake?

Mie naongelea vitambulisho wewe unaongelea internet, kwa nini usimlaumu ilikuwa hakuna TV station wakati wake, hata Karume aliweka ZTV?
 
pigia mstari hapo....na ina maana hujui sababu ni nini?
<br />
<br />
Ndiyo maana nikasema hiyo ni tabia ya mtu hata akiwa anakaa wapi na anapata nini atakuwa malaya tu unataka kuniambia kuwa wale wote malaya unaowaona wana shida kuliko wanawake wengine na hawawezi kufanya kitu kingine cha kujipatia kipato?
 
Ndio maana Serikali ya CCM imeamuwa kutengezesha vitambulisho vya uraia ambapo bar wataweza kuthibitisha umri wa anaeingia hapo bar kama wanavyofanya nchi zingine. Kwa sasa tumlaumu Nyerere aliyekuwa hataki tuwe na vitambulisho vya uraia.
<br />
<br />
"Tumlaumu Nyerere" inaonekana kuna harufu ya udini hapa.
 
Tuache mambo ya ushabiki na kuweka kila kwenye mambo ya kisiasa hivi ni kweli hao wazinzi waliambiwa wafanye hivyo na ccm? au hao polisi walipewa amri ya kufyatua risasi na ccm? Malaya ni malaya tu hata wakiwa ulaya na hawawezi kuacha hata kama wakipewa kazi ikulu wataendeleza umalaya hata na walinzi au wafagiaji ni tabia chafu na malezo mabaya ya wazazi wao.

CCM inahusika kwa 100% kwa sababu haiingii akilini mtoto wa miaka 16 anakuwa hayupo kwene uangalizi wa wazazi au walezi usiku wa manane..Serikali inatakiwa kushape mustakabali wa jamii kuanzia ngazi ya familia mpaka taifa..badala kufanya yanayowahusu raia wao wako bize kuuza nchi.
 
Back
Top Bottom