dedam
JF-Expert Member
- Jan 5, 2011
- 845
- 165
Kumbe kuna tofauti ya bakwata na bakwacha nazo ni 1. Bakwata ni baraza kuu la waislamu tanzania wakati bakwacha ni baraza kuu la waislamu wa chama cha mapinduzi. 2. Bakwata wanashughulika na dini na hawanunuliki na mambo ya kidunia wakati bakwacha wanajishughulisha na siasa na walisafiri mpaka igunga na kutoa kauli nzito kupinga wasiotaka na kuunga mkono mgombea wa ccm. 3. Bakwata wanasema hijabu ni vazi linalofunika mzima wa mwanamke kasoro viganja vya mkono na uso wakati bakwacha wanasema mtandio wa kitambaa chepesi kinachofanana na net ya mbu kikifunika kichwa nacho hijabu na yeyote atakayefunua kitambaa cha mwanamke huyo basi na adui wa uislamu na hastahili kupigiwa kura kwa mujibu wa bakwacha mtu alivaa mtandio ambao kwao ni hijabu hata kama kifua kiko wazi na kuacha wazi miguu yake ili wapita njia waamue kama anao usafiri au hana hastahi kukorofishwa na yeyote. Hizi tofauti ambazo nilikuwa sizijui. Source soma mwanahalisi.