Al Jazeera: Watanzania wanaishi maisha ya hofu na mashaka katika utawala wa Rais Magufuli. Je, hili lina ukweli wowote?

Dam55

JF-Expert Member
Oct 8, 2015
5,592
11,830
Nikiwa kwenye pitapita zangu huko mitandaoni nimekutana na makala fupi ya chombo cha habari maarufu Al Jazeera, katika makala hiyo wameeleza kuwa utawala wa Magufuli umeonyesha jitihada kubwa za kunyanyua Uchumi wa Tanzania lakini pia Watanzania hawako salama chini ya utawala wake.

Masoud Kipanya, ambaye ni mchora katuni maarufu hapa nchini alihojiwa akasema kuwa anaishi kwa hofu kubwa, anashindwa kufanya kazi zake yeye kama msanii anasema kuna baadhi ya kazi ameshindwa kuzi-publish kwa kuhofia usalama wake.

Zitto pia kwa upande wake amesema kuwa ni kweli Rais ana nia ya kuleta maendeleo chanya kwa Watanzania na ni mtu mwenye msimamo na uthubutu lakini ameonesha kila aina ya udikteta hiyo imekuwa sababu ya Watanzania kwasasa kuishi kwa hofu kubwa.

Swali: Je, ni kweli Watanzania hatuko salama? Ni kweli Watanzania tunaishi maisha ya hofu?

Kuna ushahidi upi kuwa Watanzania wanaishi maisha ya hofu kama tunavyoelezwa?
 
Kwani wewe unakaa nchi gani? Haulijui hili? Watu wanaogopa hata kuongea mambo yao kwenye simu, email,... Dikteta kakaba njia zote. Hata ile kuweka neno dikteta hapa moderator anatetemeka hata kama sikumtaja mtu. Ameifuta mara ya kwanza, nikairudisha. Hiyo yote ni wasiwasi.
 
Dah.. tuko wengi hapa ... wengine wanacheza draft .. wengine dhumuna ... wengine wako na vikombe vya kahawa na kashata .. kina mama pembeni pale wana kaanga mihogo yao .. mita chache mbele kuna kijiwe cha bodaboda wako wanatega abiria ..

daladala zinapishana tu route zote.. mimi hapa napita tu baada ya kutoka sokoni .. kulikuwa na lundo la watu wakitafuta mahitaji yao..kote huko sijaona sura zenye hofu .. wala viashiria vyovyote vya ukosefu wa amani ..

Vipi kwa upande wako wewe mleta mada, hali iko vipi maeneo yako?
 
Pengine wapo sahihi au hawapo sahihi

Mimi naona hofu ipo kwenye baadhi ya makundi .mfano viongozi wa serikali, au watu wenye mitazamo ya mrengo wa kulia
 
Ndio ila kuna mijitu itasema wanatumwa na mabeberu. Kuna tukio limetokea juzi tu lile la kukatwa kwa matangazo ya kipindi cha ajenda 2020 inaonyesha jinsi waendeshaji wa kipindi walivyokuwa na hofu ya kupigwa kofi na serikali kupitia chombo cha dola kwa kuruhusu pambalu kuanika madhaifu ya bunge, kiukweli kwa sasa ukiwa mtu mwenye kuweka madhaifu ya serikali kupitia nyanja yoyote ile iwe kisiasa kiuchumi, kijamii mpaka kwenye mambo ya michezo basi wewe uko na usalama mdogo
 
Waache kutuwekea maneno mdomoni hao, waangalie hata Watu walivyo huru kugombea Uraisi.

Watu wanajitokeza kugombea Uraisi kwa uhuru, kina Msigwa, Nyalandu, Mbowe, Hussein Mwinyi, Mbarawa, Ally Karume, Nahodha ...... kungekuwa na hofu nani angejitokeza kugombea?
 
Wanaoongoza kusema Magufuli dikteta na siyo mvumilivu ndiyo wanaoongoza kumsema Magufuli kwa uwazi na matusi juu, tena kumtukana Mara kwa mara na kumzushia mambo ya uongo kibao huku wakidunda mitaani.

Ndipo utakapojua baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wanacheza ngoma ya nani.
 
Dam55,
Hilo ni kweli kabisa, sasa hivi tunaongozwa kwa shuruti kwa amri zake. Kuna lile kundi la watu wasiojulikana ndio hutumika kunyamazisha kwa kuwateka, kuwaachia vilema hata kuwaua. Hili wala halina mjadala. Chaguzi za nchi hii zinanajisiwa kwa maagizo yake. Vyombo vya habari vya hapa nyumbani vimetishwa, ili visiripoti huu unyama, bali viripoti atakavyo.
 
Kama siyo mhalifu, hofu ya nini?

Watu wawili Kioanya, Zito ndiyo watanzania hao?
Utafiti was wapi huo? Au na Al Jazira wamekuwa poyoyo kama Tanzania Daima?
 
Dah.. tuko wengi hapa... wengine wanacheza draft.. wengine dhumna,...wengine wako na vikombe vya kahawa na kashata..kina mama pembeni pale wana kaanga mihogo yao.. mita chache mbele kuna kijiwe cha bodaboda wako wanatega abiria.. daladala zinapishana tu route zote.. mimi hapa napita tu baada ya kutoka sokoni.. kulikuwa na lundo la watu wakitafuta mahitaji yao..kote huko sijaona sura zenye hofu..wala viashiria vyovyote vya ukosefu wa amani..

Vipi kwa upande wako wewe mleta mada, hali iko vipi maeneo yako?

Hao wenye furaha ni wale walikubali kuishi kikondoo na kutawaliwa bila ridhaa yao.
 
Dah.. tuko wengi hapa... wengine wanacheza draft.. wengine dhumna,...wengine wako na vikombe vya kahawa na kashata..kina mama pembeni pale wana kaanga mihogo yao.. mita chache mbele kuna kijiwe cha bodaboda wako wanatega abiria.. daladala zinapishana tu route zote.. mimi hapa napita tu baada ya kutoka sokoni.. kulikuwa na lundo la watu wakitafuta mahitaji yao..kote huko sijaona sura zenye hofu..wala viashiria vyovyote vya ukosefu wa amani..

Vipi kwa upande wako wewe mleta mada, hali iko vipi maeneo yako?
Hofu inakuwa ndani huwezi iona.
 
Hilo ni kweli kabisa, sasa hivi tunaongozwa kwa shuruti kwa amri zake. Kuna lile kundi la watu wasiojulikana ndio hutumika kunyamazisha kwa kuwateka, kuwaachia vilema hata kuwaua. Hili wala halina mjadala. Chaguzi za nchi hii zinanajisiwa kwa maagizo yake. Vyombo vya habari vya hapa nyumbani vimetishwa, ili visiripoti huu unyama, bali viripoti atakavyo.
Kama ambavyo mh Mbowe alivyoshambuliwa hivi karibuni na kundi la wasio julikana na kuvunjwa mguu ama sivyo mkuu?
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom