Al Jadawi yuko Tanzania?

Duu nimejiona sijui historia ya tz na hata zbar....najiona mtupu kabisa nahitaji sana kujua zaidi hist ya nchi hz 2 kwa makini tangu harakati na woote walioshiriki na waliotusaliti na walipo .....hadi haatma yetu...maana mmm
 
Ukiwa Mzanzibari moja kwa moja wewe ni Mtanzania. Lakini unaweza kuwa Mtanzania pasipo kuwa wewe ni Mzanzibari. Uraia una ncha nyingi , na ya muhimu ni nile ya kuwa raia wa kuzaliwa, na kutoukana uraiawako wa kuzaliwa.

Uzanzibari siyo uraia.. hakuna raia wa Zanzibar.. wapo wakazi wa Zanzibar. Kuna uraia mmoja tu nao ni ule Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.... Hivyo, kuwa Mzanzibari hakukufanyi kuwa Mtanzania unless kama ulikuwa raia wa Zanzibar kabla ya Muungano..
 
duh haya yote tumeshayasema mkuu.. anaitwa Brig. Gen. Suleiman Yahya Mohammed Al-Adawi.. alizaliwa miaka ya hamsini na kuondoka Zanzibar miaka michache kabla ya mapinduzi ya Zanzibar.. familia yake ina nyumba Dar na Zanzibar (ana ndugu zake wengi tu na wana biashara kadhaa). Ana ukaribu wa mahusiano na Rostam na watawala wa Zanzibar.. pia vyanzo vya intelligencia vinadokeza kuwa ana mahusiano ya karibu na watu wa CUF hususan mmoja wa viongozi wakuu wa CUF..

Ahaaaaaa! Kumbe ndo maana Lipumba alikuwa anatetea ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans kwa visingizio kadhaa! Duh! Hii TZ taaaabu kweli kweli. Kwa maana nyingine tukimpa kura Limpunda ufisadi bado utakuwa ni kwa kwenda mbele.
 
Ni kweli alikuwapo Zanzibar kiasi cha wiki tatu zilizopita kwa hakika. Rostam alikwenda huko kuonana naye kama kawaida yao. Al Adawi ambaye alikuwa ADC wa Mfalme wa Oman, ni mtu muhimu sana kwa siasa za TAnzania. Ana majumba mawili ya kifahari katika beach za East eneo la Bwejuu na West Coast eneo la MAzizini. Mazizini aliuziwa kwa bei ya bure na Dk; Salmin Amour nyumba ya serikali na aliibomoa na kujenga kasri. Ahsante Gembe kutuzindua, tunamrafuta.

ADC kirefu chake ni nini?
 
Hi thread ni katika threads nzuri za JF kwa muda mrefu maana inafundisha, ina mambo mengi ambayo wengi hatuyajui na tunaweza kujifunza. Binafsi nimeipenda!
 
Back
Top Bottom