johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,616
- 141,447
Rais chagua Mkapa lakini mbunge ni chaguo lako by J K Nyerere 1995 Iringa mjiniHii kauli kama kichwa cha habari kinavyosema eti hakuna kuchagua mbunge wa upinzani hata kama anafaa.
Maneno kama haya kuzungumzwa na kiongozi mwenye dola ambaye anawania muhula mwingine wa uongozi ni kuhujumu uchaguzi mkuu.
Maneno kama haya kuzungumziwa wananchi ni kama kuwatisha kwa kuwanyima haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi bora. Kauli hii haikubaliki kamwe.
Mbaya zaidi kauli kama hizi ndizo zinaleta mzozo mkubwa siku za kutangaza matokeo. Kimsingi kauli hii ninaiona kama imetoka katika kinywa kilichokosa ustaarabu mkubwa wa kisiasa. Mbaya zaidi anayezungumza ni kiongozi wa nchi anayehubiri kuwa maendeleo hayana chama.