Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,056
- 22,755
Najua Makonda aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Najua pia kwamba Rais Magufuli aliyemteua Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, yeye mwenyewe alikatataliwa na wana Dar es Salaam. Sasa Makonda anapowataka wana Dar es Salaam wamtambue kama mungu na kwamba akisimama kuongea nao ni mungu kasimama...je mteuzi mwenyewe akisimama kuongea na wana Dar es Salaam, wamchukulie vipi?
Najua wengi hili jambo mnalichukulia kimatani lakini ukweli ni kwamba kuna aina mbili tu za watu wanaoweza kutoa kauli kama aliyoitoa Makonda. Ama ni mwathirika wa madawa ya kulevya au ni mwathirika wa ugonjwa wa akili. Mtu mwenye akili timamu hawezi kwa namna yoyote ile kutamka maneno aliyotamka Makonda. Hapa yabidi tujiulize kwa nini mpaka dakika hii mteuzi wake hajachukua hatua yoyote kutunusuru raia na kadhia hii?
Najua pia kumetokea si mara moja ama mbili tu Makonda, ameamrisha Jeshi letu la Polisi, kutii amri zake zisizo na uhalali wowote. Bila shaka haya yote yemewezekana kwa sababu Makonda akitamka, mungu katamka. Hii imewajengea wengi taswira kwamba kila anachofanya Makonda kina baraka za aliyemteua ambaye pia ndiye Jemadari Mkuu wa Taifa kikatiba. Sasa kama Makonda ni mungu, Rais Magufuli pia ni moja katika waumini wake?
=======
Najua pia kumetokea si mara moja ama mbili tu Makonda, ameamrisha Jeshi letu la Polisi, kutii amri zake zisizo na uhalali wowote. Bila shaka haya yote yemewezekana kwa sababu Makonda akitamka, mungu katamka. Hii imewajengea wengi taswira kwamba kila anachofanya Makonda kina baraka za aliyemteua ambaye pia ndiye Jemadari Mkuu wa Taifa kikatiba. Sasa kama Makonda ni mungu, Rais Magufuli pia ni moja katika waumini wake?
=======
Wana JF, Nimejaribu kuifanyia analysis/ kuichambua kwa MAKINI kauli ya RC Makonda akimjibu yule afisa wa Ardhi na kupata yafuatayo.
1. Mkuu wa Mkoa alikuwa tayari na FACTS/Ukweli kuhusu maafisa wa ardhi kusuasua katika utendaji wao wa kazi na kuumiza wananchi!
2.ALIINUA sauti yake KIDOGO akitaka apate MAELEZO SAHIHI kutoka kwa yule mama afisa wa Ardhi.
Lakini naye akajibu kwa KUZUNGUKA ZUNGUKA jambo lililomuudhi Mkuu wa Mkoa.
Maana kama afisa wa Ardhi ni LAZIMA AJUE matatizo SUGU ya ardhi hasa YALIYOKAA miaka mingi bila KUSHUGHULIKIWA!
Hivyo alihitaji jibu lililojaa maadili na UKWELI!
3.TATIZO la mama MJANE kuzungushwa zungushwa na mafisa wa Ardhi kwa MIAKA mingi akitaka HAKI yake ndo kulimfanya makonda atumie neno
"Nikisimama nasimamia MUNGU"
ukii analyze hiyo sentensi ina maana "Nikisimama NASIMAMIA KWELI ya Mungu"
Tukumbuke jamani kuwa Mungu ni Mungu wa WAJANE