malisoka
JF-Expert Member
- Jul 8, 2012
- 1,860
- 2,638
Najua Makonda aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Najua pia kwamba Rais Magufuli aliyemteua Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, yeye mwenyewe alikatataliwa na wana Dar es Salaam. Sasa Makonda anapowataka wana Dar es Salaam wamtambue kama mungu na kwamba akisimama kuongea nao ni mungu kasimama...je mteuzi mwenyewe akisimama kuongea na wana Dar es Salaam, wamchukulie vipi?
Najua wengi hili jambo mnalichukulia kimatani lakini ukweli ni kwamba kuna aina mbili tu za watu wanaoweza kutoa kauli kama aliyoitoa Makonda. Ama ni mwathirika wa madawa ya kulevya au ni mwathirika wa ugonjwa wa akili. Mtu mwenye akili timamu hawezi kwa namna yoyote ile kutamka maneno aliyotamka Makonda. Hapa yabidi tujiulize kwa nini mpaka dakika hii mteuzi wake hajachukua hatua yoyote kutunusuru raia na kadhia hii?
Najua pia kumetokea si mara moja ama mbili tu Makonda, ameamrisha Jeshi letu la Polisi, kutii amri zake zisizo na uhalali wowote. Bila shaka haya yote yemewezekana kwa sababu Makonda akitamka, mungu katamka. Hii imewajengea wengi taswira kwamba kila anachofanya Makonda kina baraka za aliyemteua ambaye pia ndiye Jemadari Mkuu wa Taifa kikatiba. Sasa kama Makonda ni mungu, Rais Magufuli pia ni moja katika waumini wake?
=======
Kuna Mnyama mmoja anaitwa KOBE Si kila mtu anamjua yule anayetembea na jumba mgongoni. na mara nyingi anaishi kwenye maji na kando ya maji. Wanyama wengi huwa wanashindwa kumdhuru kwa sababu ana KINGA KUBWA yaani lile jumba gumu alilolibeba huwa anaingiza kichwa chake na Miguu yake na unaweza kubeba ukajua ni takataka hata anapokaribiwa na hatari hujiingiza kati lile jumba lake na adui kama nyoka, ndege nk wasiweze kumpata.
Siku moja Tai si mnamjua tai alivyo na akili? alijua kabisa huyu ni kobe na ni mzima ila kwa ujanja wake amejificha kwa kuwa Tai yule hakuna na mawindo yeyote na baada ya juhudi kubwa za kumla yule kobe kushindikana akasema janja yeke ipo. Alimshika yule kobe juu juu mpaka juu sana mawinguni akamuachia ... Weee yule kobe wangu wangu akadondoka chini juu ya jiwe akapasuka vipande vipande. Basi tai kiulaini akapata lishe yake.
Mkuu wa Mkoa Mungu yupo, tena anakuona. Usije ukafanana naye watu wakakusujudia atafanya kama Tai alivymfanyia Kobe.
Please Obey God!!
Don't be a GOD.