Akili mukichwa: Wengine wakimbia nchi wengine wakimbilia Bungeni Dodoma

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Sep 11, 2017
244
312
Mara baada tu ya matokeo ya uchaguzi viongozi wakuu wa CHADEMA walidai hawawezi kubariki uchafuzi na kwamba hakuna mbunge wao atakubali kuapishwa. Sasa wameapishwa!

Nimesikia Lissu akihojiwa leo na TV kuhusu kuapishwa wabunge wa CHADEMA naye akadai kwamba anajisikia kama Yesu aliyesalitiwa. Hapo hapo akaongeza kwamba mapambano lazima yafanyike nje na ndani! Hakutaka kujibu swali lililomtaka aeleze kama chama chake sasa kinayatambua matokeo au la!

Maswali yangu kwa Mbowe

1. Je, sasa CHADEMA kinatambua matokeo ya uchaguzi? Haoni kuwa dunia inaona hawana msimamo na ni kweli walishindwa kwenye sanduku la kura?

2. Je, yule wa Mpanda aliyekaidi agizo lake ataadhibiwa ikiwa hawa wamefanya alichofanya?

3. Ule mpango wa wabunge wa jimbo kuchangia 500000 na wa viti maalum 1M utaendelea ukitilia maanani sasa wachangiaji watakuwa wachache mno? Wa Mpanda akigoma mtamfanya nini?

4. Je, kitendo cha kukubali kushiriki bunge sio sawa na kuwasaliti wenzao wanaodai wanakimbia kwa kuhofia maisha yao? Iweje wanaodaiwa kuhatarisha maisha ya wenzenu ndio wanawaapisha? Hivi Halima na Bulaya wanatofauti gani na Lema hadi Lema akimbie hadi kupeleka mke na watoto jela Kenya?

5. Je, Mbowe mmepima faida na hasara ya kushiriki? Au wamama wametoa shinikizo ili waendelee kufaidi posho? Au ni ili walau ruzuku japo kiduchu ipatikane? Hivi ACT mtawaeleza nini ikiwa wao wamealikwa na wameshikilia msimamo ninyi mmeachia? Au na ACT ni suala la njaa na muda tu wataachia?

Kweli adui mwombee njaa. Wengine wakimbia nchi wengine wakimbilia Dodoma!
 
Tutavumilia tofauti zetu na hili litapita na msitegemee kutusambaratisha kwa kutugawa!
ALUTA CONTINUA!
😅
👊 ✌️✌️✌️
 
Inatakiwa mtu achague chama au nchi. Akina Halima wamechagua nchi, kwani ni kwa mujibu wa sheria za nchi.
 
Mara baada tu ya matokeo ya uchaguzi viongozi wakuu wa CHADEMA walidai hawawezi kubariki uchafuzi na kwamba hakuna mbunge wao atakubali kuapishwa. Sasa wameapishwa!...
Mimi naona kwamba demokrasia imechukua sura mpya sasa.

Tunaanzia kujidemokratisi ndani ili nje tuwe imara..... hili la Mdee na wenzake kuapa jana ni tija kibwa sana kwa Taifa na ukuaji wa demokrasia.

Kutegemea kupambania ideologies nje ya utaratibu rasmi kunapelekea kujibananisha na uvunjaji taratibu ulio sugu.

Wale waliokimbia naamini serikali yetu inawaona bado ni watoto wake na warudi watapokelewa kama ambavyo imetolewa tamko rasmi hapo juzi.

Kuna wakati wanasiasa tujifunze kuyaacha yapite hata kama yanauma kiasi gani.

Sisi wananchi na mashabiki wa siasa tunapaswa kuwa na kiasi kwamba unaweza ukawa unatumika kwa manufaa ya huyo anayekushawishi ufanye baya lakini akishapata lake baas shughuli imekwisha na hakujali.

Naipongeza CHADEMA in advance iwapo watawaimarisha wabunge wake walioapishwa ili kushirki ujenzi wa nchi. Jambo kubwa wanalopaswa kufanya sasa ni kukubali matokeo
 
Ndo mana siasa ukiifanya kama nguo hutakaa kwa amani liroho litakuuma tu,nawapongeza wenye misimamo ya wastani ,wacha wakapate pesa ya maisha hao wengine siku zao tunazihesabu tu tunajua waturudi tu muda bado
 
Mara baada tu ya matokeo ya uchaguzi viongozi wakuu wa CHADEMA walidai hawawezi kubariki uchafuzi na kwamba hakuna mbunge wao atakubali kuapishwa. Sasa wameapishwa!..
Huko CCM hakuna hata mwanachama mmoja mwenye akili akawa anatoa mawazo mazuri ya kueleweka na kukubalika na wote humu JF maana chochote cha kijinga kama hiki mleta mada au uzi atatambulika tu kuwa ni wa CCM kwa ujinga uliomo. CHADEMA, vyama vya Upinzani na wapiga kura wote walioibiwa kura zao, hawatambui matokeo ya Uchafuzi ule lakini haina maana Sheria, taratibu na kanuni zilizopo nazo zinapingwa.

Askari yeyote vitani anakuwa na manufaa kwa Jeshi lake, nchi yake na kwake mwenyewe kama atabaki hai kuendelea kupigana ndani na nje mpaka ushindi upatikane kama Mh Lissu alivyosema. Lissu alitishiwa maisha akatoa taarifa kwa wahusika wakapuuza, akapugwa risasi 16 mbele yao lakini mpaka leo IGP Sirro hajasema neno wala kufanya lolote kuwakamata wahusika.

Baada ya Kampeni mlinzi aliyepewa na Serikali aliondolewa na Mh Lissu alitangaza kutishiwa maisha na badala ya kupewa ulinzi alikamatwa ili amalizwe kwa madai ya kutaka kuandamana bahati nzuri diplomasia iliingilia kati akaachiwa kwa muda ndo akaamua ahame nchi ili aweze kuendelea kupigana akiwa hai.

Angekuwa mjinga kama mleta mada kama angebaki nchini Dodoma ambako alipigwa risasi 16 zingine zikiwa bado ziko mwilini eti ili aendelee kupambana na maadui zake walioko mita chache tu ambao wameua watu wengi kuliko Awamu zote nne za nyuma. Mh Lissu, Godbless Lema na wengine walioamua kuhama nchi ili kunusuru maisha yao wapigane tena siku nyingine, huo ukiwa ni uamuzi wa busara na pigo kwa CCM, Serikali na wauaji wasiyojulikana waliondaliwa.

Wabunge wa CHADEMA wa viti maalumu hawaingii Bungeni kwa ushindi wa Uchafuzi uliowaingiza wale wote batili wa CCM bali wanaingia kisheria na taratibu na Chama chao kimetumia busara ya kutii Sheria kuruhusu waapishwe. Yule wa Nkasi, Katavi wa kuchaguliwa na wananchi aachwe awakilishe wapiga kura wake, kitakachompata Msimamizi kutotii agizo toka juu la kutotangaza Mpinzani, hakimhusu yeye aungane na wenzake wa viti maalumu watuwakilishe badala ya wenzao wengi tuliowapigia kura lakini kura za kwenye mabegi meusi ndo zilitosha.

Ni kweli kwa uchache wao na tabia chafu iliyojengeka na iliyozoeleka ya Wabunge wa CCM walio wengi, mchango wao utamezwa na kelele za wazungusha makalio na wapiga makofi meza lakini hata mtu mmoja anaweza akaleta mabadiliko.
 
Back
Top Bottom