KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,154
- 56,705
Huyu si yule ninaemzungumzia la hasha!! ila kipindi ana gimba jeupe kichwani mwake na maji yatembeayo ktk viunga vyake alionekana mahili,jasiri na mwenye fadhili.
kila alipopita alipigiwa makofi na vigelegele,utashi wa kazi zake ulikuwa wa haki ndivyo wasemavyo lkn nini sasa..?
wakati uliopita si wa sasa,wasasa unaenda na wasasa huku ngoma ikipigwa kwa milindimo tofautitofauti wachezaji nao wanaenda tofauti!!
hata hivyo akicheka anamwanya hajui hilo ila gimba lake jeupe lilihisi hivyo!. waekaji wa historia walimuweka ktk mitindo tofautitofauti lkn mpiga ngoma sijui hajaielewa mitindo hiyo!,basi ngoma ipigwe,ichezwe,turuke ila tusimsahau akicheka anamwanya.