Akaunti za mafisadi BoT zagundulika

Jembajemba

JF-Expert Member
Feb 3, 2007
257
32
WAKATI moto wa sakata la utata wa kampuni ya kitapeli ya Richmond ukiendelea kuwaka, huku Bunge likisubiri kwa hamu hatua zitakazochukuliwa dhidi ya watuhumiwa, bomu jingine la ufisadi mkubwa uliofanyika kwenye akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) limelipuka kufuatia vigogo kadhaa Serikalini wakiwemo wastaafu kubainika walinufaika kwenye ufisadi huo.

Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu ndani ya Serikali viliambia Majira Jumapili kwamba tayari Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi kwa kushirikiana na mataifa mbalimbali imegundua nyumba na hoteli za kifahari zinazomilikiwa na viongozi wa Serikalini, wafanyabiashara maarufu na viongozi mashahuri wastaafu walionufaika kwa namna moja au nyingine na ubadhirifu wa sh, bilioni 133 za akaunti ya EPA.

Miongoni mwa mambo yaliyosaidia kubainika kwa mali hizo ni baada ya baadhi ya mataifa ya nje kuihoji Serikali ya Tanzania juu ya uwezo wa viongozi hao kuzimiliki.


Uchunguzi wa kina na uliopata uthibitisho kutoka kwa maofisa wa ngazi muhimu wanaojua mchakato wa chini kwa chini unaofanywa kufuatilia zilikopelekwa fedha hizo, pia umeeleza kuwa kuna mabilioni ya fedha za mafisadi hao zimenaswa kwenye akaunti mbalimbali za nje.

Katika Uchunguzi huo nchi zilizogundulika kuwa watuhmiwa wamewekeza miradi mbali na fedha ni pamoja na Uswidi, Marekani, Ubeligiji, Dubai, Afrika Kusini na nchi kadhaa zenye ushirikiano wa kibiashara na Tanzania.

“Mimi nawashangaa watu wanaohofia taarifa ya uchunguzi wa Richmond, wangejua kilichomo ndani ya taarifa ya EPA wasingezungumza, ninaamini wananchi wakijua majina yaliyomo kwenye taarifa ya EPA wangetaka wawekwe kizuizini moja kwa moja wakati uchunguzi ukiendelea.

“Unajua wakati Rais alipozungumza kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi hakutaja majina ya vigogo waliohusishwa, ni majina yanayotisha, wamo viongozi waandamizi wakiwemo Makatibu Wakuu wa Wizara kadhaa walioko Serikalini na waliostaafu," kilisema chanzo chetu.

Habari hizo zilieleza kwamba licha ya vigogo wa Serikali pia wapo wafanyabiashara maarufu nchini huku baadhi yao wakiwa tayari wametajwa kwenye ripoti ya Richmond.

“Uchunguzi wa Serikali umefanyika kwa siri kubwa, ndio maana hata Bunge ilipoomba ripoti hiyo Serikali haikutaka kutoa maelezo zaidi kwani kufanya hivyo kwa sasa kungevuruga uchunguzi unaoendelea, Serikali imeomba nchi kadhaa kutoa ushirikiano na tayari nchi husika zimeitikia kwa sharti kwamba iwe siri kubwa,” kiliongeza chanzo chetu na kuthibitisha kuwa tayari baadhi ya akaunti hizo zimefungwa.

Pamoja na taratibu zingine Serikali inafanya uchunguzi kujua namna watuhumiwa hao walivyopata fedha zilizoko kwenye akaunti zao za nje pamoja na uwezo wa kujenga nyumba na hoteli za kifahari ambazo hata nchi husika zinashangaa uwezo wa Watanzania hao.

source:
http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=5704
 
Hii inaonyesha wazi kuwa Tanzania sio nchi maskini bali kuna watu wachache ambao wanafaidika na utajiri mkubwa ambo nchii hii unao. Mbali na wageni ambao kila leo wanavuna utajiri wa nchi hii lakini pia kuna Watanzania wenzetu ambao hawana chembe ya huruma kwa watanzania wenzeo ambao hata mlo wa siku moja haujui??? kwa kweli inasikitisha na kuhuzunisha kuona watu wa sample hii.

Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Africa

Mungu wanakamishe Mafisadi wote - ameen
 
WAKATI moto wa sakata la utata wa kampuni ya kitapeli ya Richmond ukiendelea kuwaka, huku Bunge likisubiri kwa hamu hatua zitakazochukuliwa dhidi ya watuhumiwa, bomu jingine la ufisadi mkubwa uliofanyika kwenye akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) limelipuka kufuatia vigogo kadhaa Serikalini wakiwemo wastaafu kubainika walinufaika kwenye ufisadi huo.

Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu ndani ya Serikali viliambia Majira Jumapili kwamba tayari Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi kwa kushirikiana na mataifa mbalimbali imegundua nyumba na hoteli za kifahari zinazomilikiwa na viongozi wa Serikalini, wafanyabiashara maarufu na viongozi mashahuri wastaafu walionufaika kwa namna moja au nyingine na ubadhirifu wa sh, bilioni 133 za akaunti ya EPA.

Miongoni mwa mambo yaliyosaidia kubainika kwa mali hizo ni baada ya baadhi ya mataifa ya nje kuihoji Serikali ya Tanzania juu ya uwezo wa viongozi hao kuzimiliki.


Uchunguzi wa kina na uliopata uthibitisho kutoka kwa maofisa wa ngazi muhimu wanaojua mchakato wa chini kwa chini unaofanywa kufuatilia zilikopelekwa fedha hizo, pia umeeleza kuwa kuna mabilioni ya fedha za mafisadi hao zimenaswa kwenye akaunti mbalimbali za nje.

Katika Uchunguzi huo nchi zilizogundulika kuwa watuhmiwa wamewekeza miradi mbali na fedha ni pamoja na Uswidi, Marekani, Ubeligiji, Dubai, Afrika Kusini na nchi kadhaa zenye ushirikiano wa kibiashara na Tanzania.

“Mimi nawashangaa watu wanaohofia taarifa ya uchunguzi wa Richmond, wangejua kilichomo ndani ya taarifa ya EPA wasingezungumza, ninaamini wananchi wakijua majina yaliyomo kwenye taarifa ya EPA wangetaka wawekwe kizuizini moja kwa moja wakati uchunguzi ukiendelea.

“Unajua wakati Rais alipozungumza kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi hakutaja majina ya vigogo waliohusishwa, ni majina yanayotisha, wamo viongozi waandamizi wakiwemo Makatibu Wakuu wa Wizara kadhaa walioko Serikalini na waliostaafu," kilisema chanzo chetu.

Habari hizo zilieleza kwamba licha ya vigogo wa Serikali pia wapo wafanyabiashara maarufu nchini huku baadhi yao wakiwa tayari wametajwa kwenye ripoti ya Richmond.

“Uchunguzi wa Serikali umefanyika kwa siri kubwa, ndio maana hata Bunge ilipoomba ripoti hiyo Serikali haikutaka kutoa maelezo zaidi kwani kufanya hivyo kwa sasa kungevuruga uchunguzi unaoendelea, Serikali imeomba nchi kadhaa kutoa ushirikiano na tayari nchi husika zimeitikia kwa sharti kwamba iwe siri kubwa,” kiliongeza chanzo chetu na kuthibitisha kuwa tayari baadhi ya akaunti hizo zimefungwa.

Pamoja na taratibu zingine Serikali inafanya uchunguzi kujua namna watuhumiwa hao walivyopata fedha zilizoko kwenye akaunti zao za nje pamoja na uwezo wa kujenga nyumba na hoteli za kifahari ambazo hata nchi husika zinashangaa uwezo wa Watanzania hao.

source:
http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=5704

Duh! Ndio maana hawataki kabisa kuitoa hiyo ripoti ya ukaguzi wa EPA maana sirikali yote itaonekana IMEOZA kwa ufisadi! Hawa wabunge nao bado ni mabaradhuli! watakubali vipi bunge liahirishwe hadi mwishoni mwa April wakati kuna tuhuma nzito za ufisadi ndani ya BoT!
 
Hii Serikali yote ni kitu kimoja usanii mtupu kwa nini wanawaficha hawa mafisadi??? kwa nini wasiwaweke hadharani jamii ikawaona??? and then sheria kachukua mkondo wake
 
Ndugu yamgu Jemba jemba hali ya Mtanzania inasikitisha na kibaya zaidi ni kwamba wanaosababisha madhila haya ni wenzetu tena waliotujia na hoja tamu za namna wanavyofikiria kumuondoa mtanzania hapo alipokuwepo na kumpeleka sehemu nyingine na kweli wamefanya hvyo kwa kumpeleka kwenye dimbwi zaid la umaskini. Leo hii Kandoro analia lia tumchangie fedha za madawati na madarasa ya shule anazojenga na ilhali huku hazina na kodi anazokamuliwa Mtz zinaliwa na wajanja ambao kila kukicha wanabuni mbinu za kumuua mtz kusudi kama jana alipata mlo mmoja kwa siku kesho asipate hata uji. Kwa kweli inatia uchungu. Lakini tukumbuke kwamba ripoti ya EPA ni tone la maji tu kati ya mengi ambayo yamefanywa na hawa hawa wanaojiita wazalendo wa nchi hii.
 
Na kila ninaposema Kikwete anafanya kweli, watu hawanielewi
 
Na kila ninaposema Kikwete anafanya kweli, watu hawanielewi

Anafanya kweli gani??
Hakuna haja ya kumwogopa mhalifu, eti ukimtaja utaharibu ushahidi...Sasa kwani hao watu hawajijui kama kampuni zao zimetajwa tayari?? Tena katika ukimya huu ndo wataweza kuharibu ushahidi maana wamepewa a period of 6 months...
Kikwete anawachezea watanzania, kinachofanyika kwa sasa ni juhudi za udi na uvumba kuwanasua washikaji zake akina Kagoda Agriculture na wengine, wewe subiri tu utakuja kuona siku hiyo ripoti inasomwa...
 
Acheni habari za magazetini, kama kweli ilikuwa siri mbona imeshatoka?...
Nani mwenye account hizo ambaye kwa taarifa kama hii atakuwa bado amelala akizubiri report ya EPA ifikishwe bungeni..Hakuna siri Tanzania isipokuwa kuna kubebana..
Majina sii hoja, hoja na ushahidi ni kiasi gani cha fedha zipo huko na zimeokolewa... JK na serikali yako kama utafanya kweli fanya, hizi habari za kusubiri ziara ya Bush mara sijui nini hali kinachopotea ni zaidi ya msaada huo hatuwezi vumilia.
Chakula kinapoa mkubwa maswala ya kusubiri mgeni aondoke watu ndio kwanza wanashiba jikoni..na tonge likisha ingia tumboni kitakacho bakia ni lawama tupu...kinyesi hakiliki wala kuhesabika..
 
Wakuu hiii ngoma bado ni mbichi sana, time will tell, maana pia kuna wafadhili wetu ambao wanataka kujua waliojiuzulu na wanaotuhumiwa watishia kufanywa nini?
 
Field Marshall Es,
Unajua mimi nachoshindwa kuelewa ni kwamba pamoja na kuwa ngoma hii nzito lakini hawa watu tuliwafahamu toka Mkapa aondoke madarakani na wengine as soon as hizi scandal zimetokea.. tuliwataja kwa majina yao lakini JK akasema leteni Ushahidi.. akapewa bado hakuamini kwa madai kuwa ni tetesi na walikuwepo washabiki kibao..

Leo majina yameisha julikana na hadithi ni ile ile kama tulivyoweka madai yetu toka 2006 bado tunaambiwa tusubiri wakijenga habari kibao za kuepusha hasira za wananchi hali hakuna mashtaka yoyote yaliyokwisha wekwa kisheria..
Tutasubiri ikiwa mashtaka tayari lakini hizi habari za Upelelezi kuendelea wakati uchunguzi tayari umeisha kamilika ni kuwabeba baadhi ya watu..They are not stupid mkuu kuihama nchi sii swala zito waliweza miaka ya Nyerere na pili wengi wao hawana asili ya pale.
 
jamani nawammbieni kuwa sidhani kama kuna lolote la maana litakalofanyika dhidi ya watuhumiwa maana hili la Richmonduli limefanyika kusudi kurudisha heshima ya bunge kwa wananchi (ripoti ya redet). na vilevile Chama Chawala kinajaribu kutoa kafara (zaka) za kuteketezwa ili iwe harufu nzuri kwa ushindi ujao. Ila hizo hela hazitorudi na wahusika watapewa respect kama mlivyoanza kuona wanavyomiminiwa sifa ya kuamua kujiuzulu baada ya kutuhumiwa.

Sisi tunataka hela zetu zirudi ili mwalimu kasongo kule mvuti alipwe mshahara wake kwa time, na mjomba wangu malingumu apate pensheni yake kwa wakati. Sisemi kuhusu zahanati na huduma zake, sisemi kuhusu pembejeo na nishati. Nasema kuhusu hela kurudi na zifanye jambo la maana au la huu ni utapeli mchana kweupeeee
 
Na kila ninaposema Kikwete anafanya kweli, watu hawanielewi

Kikwete mwenyewe anahusika na ufisadi, kwa nini hawa Majira wasimtaje tu Mkapa na ma goons wake?

Kikwete hawezi kum prosecute Mkapa wala Lowassa kwa sababu na yeye ana issues kibao.

Vita dhidi ya rushwa Tanzania haiwezi kufanikiwa mpaka CCM ing'olewe.
 
Waanze kuwafilisi akina Lowasa, Rostam, Mramba, Chenge nk then tutajua wapo serious otherwise mazingaombwe tu...
 
Nasema huu ni mtihani mgumu sana kwa JK na sisi wadanganyika tunasubiri kusikia,hizi habari za magazeti tunazishukuru kwani ndiyo ambazo zinatufumbua macho. Kubwa hapa ni nani kahusika na jina lake litajwe adharani na tujue kachukuliwa hatua gani na mwaisho fedha zetu zirudi.
 
we zomba ww.naona umetumwa na chama cha mafisadi kuja kuwatetea huku.huwa wanakulipa sh. ngapi?
 
Sasa tunataka kuona hawa mafisadi wanatupwa gerezani. Waanze na lowassa na kundi lake. Halafu Sumaye na kundi lake. Oooh Gosh my god. Nitapiga mluzi chooni.
 
Nashindwa nianzie wapi tokana na hasira niliyokuwa nayo.

Ninachomuomba Rais na serikali yake ni kwamba wafanye kazi waliyopewa na watanzania na wala wasifanye vinginevyo.

Watanzania wengi wamepoteza kabisa matumaini na serikali, tokana na kukumbatia wezi na majangili wa uchumi wa nchi yetu.
Kauli ya Rais aliyosema eti tumwache Mkapa amestaafu tusimchunguze katika ufisadi aliofanya akiwa ikulu na hili la kuchelewesha kuwachukulia hatua wezi wa fedha toka BOT, na mafisadi wa Richmond linatupa uelewo sisi watanzania kwamba serikali inahusika na upuzi huu ama imeubariki upuzi huu. Hatuna imani na serikali yetu tena, mwaka 2010 tuipeleke serikali hii makaburini.

Nashindwa kuelewa mantiki aliyotumia Rais ya kuogopa kumchunguza KING OF ZAMUNDA AKA MKAPA kwa ufisadi alioufanya akiwa ikulu.

Wezi na mafisadi wakubwa wanajulikana hakuna sababu ya kudanganyana eti mpaka miezi sita ya uchunguzi
 
Kwanza pole kwa kazi uliyoifanya kukusanya taarifa ,lakini bado umetuacha njia panda hatuelewi ni kiasi gani cha fedha kimekwapuliwa katika akauti ya EPA na kila akauti ya kila fisadi ina kiasi gani cha fedha mafisadi hao ni akinani jaribu kuwa muwazi.ukifafanua haya yatasaidia watu wafanye maamuzi magumu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom