kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,732
Ndugu wana JF nimesikia kupitia Channel 10 kuwa TRA wameamua kuifilisi akaunti ya TFF na sababu za msingi za wao kufanya hivyo ni TFF kushindwa kulipia gharama za makocha wa timu ya Taifa Kuanzia MAXIMO NA POUSELN, Nimepata shaka sana kwani katika kumbukumbu zangu hii ilikuwa ni ahadi za Rais Kikwete kuwa serikali italeta Makocha wa kigeni ili kuinua kiwango cha Soka hapa Bongo na italipia gharama zote za makocha hao.
My Take.
1. Kama ilikuwa ni ahadi ya Serikali na ikatekeleza ahadi ya kuleta makocha hao hivi nani alikuwa anawalipa na walikuwa wanalipwa Tsh. ngapi na je fedha walizokuwa wakilipwa zilitoka wapi?
2. Wakati wa ujio wa makocha hao TFF walipewa taarifa kuwa wanatakiwa kuwalipia gharama hao makocha, maana tukiangalia kwa Maximo kwa sasa hayupo na hakuna anacholidai taifa hili.
3. Hii pia inanipa wasiwasi na Ahadi za Rais inawezekana haweki kumbukumbu zake wakati anapoongea na inawezekana leo hii akiulizwa juu ya ahadi hii anaweza kukana kuwa hakuitoa.
** Kutokana ka kufilisiwa huko inasemekana inawezekana Round ya pili ya ligi kuu ikachelewa kuanza kwani fedha walizochukua ni zile Nauli za Timu zilizotolewa na wadhamini wa Ligi KUU.
My Take.
1. Kama ilikuwa ni ahadi ya Serikali na ikatekeleza ahadi ya kuleta makocha hao hivi nani alikuwa anawalipa na walikuwa wanalipwa Tsh. ngapi na je fedha walizokuwa wakilipwa zilitoka wapi?
2. Wakati wa ujio wa makocha hao TFF walipewa taarifa kuwa wanatakiwa kuwalipia gharama hao makocha, maana tukiangalia kwa Maximo kwa sasa hayupo na hakuna anacholidai taifa hili.
3. Hii pia inanipa wasiwasi na Ahadi za Rais inawezekana haweki kumbukumbu zake wakati anapoongea na inawezekana leo hii akiulizwa juu ya ahadi hii anaweza kukana kuwa hakuitoa.
** Kutokana ka kufilisiwa huko inasemekana inawezekana Round ya pili ya ligi kuu ikachelewa kuanza kwani fedha walizochukua ni zile Nauli za Timu zilizotolewa na wadhamini wa Ligi KUU.