Akamatwa Live Gesti na Denti wake!

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,316
33,125
fimanizi20101.jpg


Mwalimu wa Shule ya Sekondari Muhanga, iliyopo Tabata Kinyerezi, Dar, Lucas Yusuph a.k.a Ticha Leizer, juzi alijikuta akipata aibu ya mwaka baada ya kukutwa ndani ya gesti akiwa na mwanafunzi wake wa kidato cha tatu (Jina linahifadhiwa).

Ijumaa Wikienda a.k.a the Biggest IQ Paper ndilo pekee lenye kuthubutu kuwa la kwanza kulianika tukio hilo ambalo lilichukua nafasi Ijumaa iliyopita (Aprili 9, 2010) ndani ya kuta za Mori Guest, Sinza, Dar na kusindikizwa na timbwili zito.​


.....jamani nilikuwa namfundisha hesabu za square...square..!!


fimanizi2010.jpg

...ishakuwa soo, nimeingia choo cha kike...

fimanizi20102.jpg

....zana za kujihami alikuwa nazo
...dah viatu havivaliki!

“Kuhusu hili la Mwalimu Leizer, huyu binti yetu amekuwa akimlalamikia kwa muda mrefu akieleza kuwa, amekuwa akimsumbua akimtaka kimapenzi. Licha ya kumkatalia mwalimu huyu amekuwa akimlazimisha na leo amemwambia wakutane katika gesti ya Mori, eti kuna mambo anataka kumwambia, tunaomba mtusaidie ili tuweze kumnasa fataki huyu.”

Kufuatia maelezo hayo, waandishi wetu kwa kushirikiana na wazazi wa binti huyo pamoja Polisi wa Kituo cha Alimaua A, Tandale waliweka mtego ambapo Ijumaa majira ya saa 11 jioni walifanikiwa kumnasa Ticha huyo ‘live’ akiwa na mwanafunzi wake ndani ya chumba namba 1 cha gesti hiyo.

Baada ya fumanizi hilo, mwalimu huyo alijitetea kuwa hakuwa na lengo baya na denti wake na kudai kuwa, walikutana pale ili amfundishe mwanafunzi wake somo la Hisababti.​

Hata hivyo, Ticha huyo alipobanwa kuhusu kondomu zilizokuwa kitandani, alishindwa kutoa majibu ya kueleweka.

Vijana wa Mwema ambao wakati huo walikuwa eneo la tukio, walimchukua mwalimu huyo pamoja na mwanafunzi wake hadi Kituo cha Polisi cha Alimaua kwa ajili ya mahojiano.

Ticha Leizer wakati akijieleza, aliruka kimanga kwa kudai kwamba yeye siyo mwalimu na kuongeza kuwa hata binti huyo aliyekuwa naye gesti hakujua ni denti.

fimanizi20102.jpg
....zana za kujihami alikuwa nazo

Hata hivyo, utetezi wake huo mbele ya polisi ulionekana kuwa feki kwani zilifanyika jitihada za kupata namba ya simu ya mwalimu mkuu wa shule hiyo aliyefahamika kwa jina moja la Mwakatobe ambaye alikiri kwamba Leizer ni mwalimua wake wa somo la Historia.

Mwakatobe alisema kuwa Leizer ni mwalimu mgeni shuleni kwake ambaye hajapitia Chuo cha Ualimu, bali ni mhitimu wa Kidato cha Sita (Form Six Leaver).

...umeumbuka mzee mzima..
Licha ya maelezo hayo ya Mkuu wa shule, bado Leizer aliendelea na msimamo wake kuwa si mwalimu katika shule hiyo hivyo kulazimisha shitaka hilo kuhamishiwa Kituo cha Polisi cha Mabatini kilichopo Kijitonyama kwa hatua nyingine.​

Baada ya kufika kituoni hapo, maelezo ya pande zote mbili yalichukuliwa upya na baadaye mwalimu huyo kufunguliwa jalada la kesi lenye namba KJM/RB/2227/2010 SHAMBULIO LA AIBU kisha mwalimu huyo kuwekwa ‘lokapu’.​

Gazeti hili linakemea vikali tabia ya walimu kuwatongoza wanafunzi wao na linaomba taasisi husika kuhakikisha walimu kama hao wanashughulikiwa ipasavyo kwani wamekuwa ni chanzo cha baadhi ya wanafunzi wa kike kufeli katika masomo yao. MHARIRI.
 
matatizo hayo yapo kwa walimu lakini kwa suala la Liezer kweli yeye si mwalimu kwa taaluma ya ualimu kwa ni form six leaver asiye na mafunzo ya ualimu. hivyo hana maadili ya uali,u kabisa.kama akitpitia ualimu at least angekuwa na ufahamu madhara ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi wake kiamaadili ya ualimu na kwa sheria za nchi yetu.

Nashauri shule zetu zijitahidi sana kuajiri waalimu wenye taaluma ya ualimu na kufuata cheap labour.
 
Mwl. wa History kaenda kumfundisha namba! Of all venues, guest ndio palikuwa most suitable kwa hilo zoezi lao? At whose expense?
 
nadhani hii ni jokes !!! ilikua ni igizo tuu .... !!! Au imekaaje wakuu humu ndani ????
 
Hakuna kitu hapo!! hizi story za mchungaji Shigongo za kuuza tabloid kwa wakina mama wa uswazi tu!
 
duuuuuuuuuuuh haka kajamaah hatari kwelikweli,
TUWE WAANGALIFU NA WALIMU WAKWARE NA HIZI TUITION,TUITION UICHAGUE WEWE MZAZI MTOTO WAKO AKASOME WAPI SIO ' mwalimu yule mzuri anafundisha vizuriiiiiiiiiiii naomba niende'. UMEUMIA.
 
Hivi denti wa kidato cha tatu ana miaka mingapi vile? Na huyu mwalimu umri wake? Naona kama walielewana tu. Hao waandishi nao muflisi kabisa, hili ni fumanizi kivipi, nani mlalamikaji hapo? Kwani huyo mwanafunzi ni mke wa mtu? Au mke wa huyo mwalimu yuko wapi, mbona hatuambiwi kuwa ndie mlalamikaji, pengine hata hajaoa huyo mwalimu. Ujinga tu wa waandishi wetu. Mwalim mwenyewe anaonekana kabisa ni wale yeboyebo, kamaliza form six mwaka huu hata sura inaonesha bado mtoto. Hawa ni rika moja tu, hilo la ualimu na uanafunzi ni labels tu lakini kwa hali halisi ni rika moja, wanafanya kinachofanywa na watu wa rika hilo. Tuacheni hukmu za kijinga.
 
Nadhani watu aina hii ya fataki wanatakiwa kuchukuliwa hatua kali. vilevile inaelekea huyo mwanafunzi hajalelewa vizuri na wazazi wake kwani alipaswa kutoa taarifa kwa wazazi na pia mwalimu mkuu kuhusiana na huyo mkware. Tatizo lingine ninaloliona ni kutafuta cheap labour kwa kuokota watu wasiokuwa na sifa sitaiki ya kazi ya ualimu. Ukilichambua kwa haraka haraka utaona karibu kila mtu ana kosa.
Eeeeeee Mungu wanusuru mabinti zetu.
 
Mh hii kali binti body limetulia na linaita lakini na kamuinamia jamaa na inaonyesha kuwa wana mafeeling ya ukweli ukweli ila Teacher naye lol gest hii ndo zile za buku cheki kuta hizo hapo ukilala unao
 
Back
Top Bottom