Akamatwa kwa kujifanya Katibu Mkuu Kiongozi wa Ikulu na kutapeli Ofisi za Serikali

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu Dar es salaam linamshikilia Seif Abdallah Mohamed, mkazi wa Tuangoma Kigamboni jijini Dar es salaam, kwa tuhuma za kujifanya Katibu Mkuu Kiongozi wa Ikulu na kuendesha vitendo vya utapeli katika ofisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Operesheni ya Jeshi la Polisi Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabas, amesema Seif mwenye umri wa miaka 35 alitiwa mbaroni baada ya kumpigia simu kiongozi wa ngazi za juu kwa nia ya kutekeleza vitendo hivyo vya utapeli.

Kamanda Sabas anasema Seif anatuhumiwa kuwa alikuwa akitumia majina zaidi ya manne katika vitendo hivyo vya utapeli ikiwemo kujitambulisha kama mkuu wa nidhamu na maadili wa chama cha mapinduzi (CCM).

Chanzo: Channel Ten
 
Kuna watu wanatisha sana duniani.

Bado level za Rais na Waziri Mkuu na Makamu wa Rais. Lakini zingine washapita kujitambulisha kitambo sana kwamba wao akina nani.
 
Utapeli wa Namna hii kwa Nyazifa kubwa hivyo tena unatapeli Idara za Serikali huwa hauniingii Akilini kabisaaa!!!
 
Ndo hivyo tena mkuu. Hivi hakushangazi hata madaktari feki katika Hospitali kubwa kuhudumu hata mwaka mzima.
Utapeli wa Namna hii kwa Nyazifa kubwa hivyo tena unatapeli Idara za Serikali huwa hauniingii Akilini kabisaaa!!!
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu Dar es salaam linamshikilia Seif Abdallah Mohamed, mkazi wa Tuangoma Kigamboni jijini Dar es salaam, kwa tuhuma za kujifanya Katibu Mkuu Kiongozi wa Ikulu na kuendesha vitendo vya utapeli katika ofisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Operesheni ya Jeshi la Polisi Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabas, amesema Seif mwenye umri wa miaka 35 alitiwa mbaroni baada ya kumpigia simu kiongozi wa ngazi za juu kwa nia ya kutekeleza vitendo hivyo vya utapeli.

Kamanda Sabas anasema Seif anatuhumiwa kuwa alikuwa akitumia majina zaidi ya manne katika vitendo hivyo vya utapeli ikiwemo kujitambulisha kama mkuu wa nidhamu na maadili wa chama cha mapinduzi (CCM).

Naye huyu bwn mbona katumia uongo mkubwa mno
 
Ni ishara ya kwamba mosi ni ukosefu Wa ajira, mbili ni kwamba wapo watu ambao ndoto zao nilikuwa ni kuwa watu Fulani, ko kutokana na ndoto hizo kuzima wanajaribu kuzufufua kwa njia yoyote!!!
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu Dar es salaam linamshikilia Seif Abdallah Mohamed, mkazi wa Tuangoma Kigamboni jijini Dar es salaam, kwa tuhuma za kujifanya Katibu Mkuu Kiongozi wa Ikulu na kuendesha vitendo vya utapeli katika ofisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Operesheni ya Jeshi la Polisi Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabas, amesema Seif mwenye umri wa miaka 35 alitiwa mbaroni baada ya kumpigia simu kiongozi wa ngazi za juu kwa nia ya kutekeleza vitendo hivyo vya utapeli.

Kamanda Sabas anasema Seif anatuhumiwa kuwa alikuwa akitumia majina zaidi ya manne katika vitendo hivyo vya utapeli ikiwemo kujitambulisha kama mkuu wa nidhamu na maadili wa chama cha mapinduzi (CCM).
Ukiona hivyo ujue viongozi wa ngazi za juu si waadilifu...nao ni matapeli ndiyo maana matapeli wanawatumia...
 
Nilidhani utasema kuwa ukiona hivyo ujue kuna ambao walikuwa wanakula nao..!
Ukiona hivyo ujue viongozi wa ngazi za juu si waadilifu...nao ni matapeli ndiyo maana matapeli wanawatumia...
 
Back
Top Bottom