Aka fifte za hali tete....Kwa mshua, Inakuwaje mzazi?

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,385
..leo imebidi nikucheki kwa njia ya Zee manake nimekuwa nikitafuta kweli njia ya kugumiana na wewe lakini watu wananibania, nikaona sio mbaya katika miaka hii Fifte ya Independensi, nikuandikie leta. Japo ni sistim ya kilongtaimu sana,

Aka fifte za Uhuru, jana tulikuwa tunacheki runinga na wanangu, tumekuskia tumekuona na tumekubali spichi yako, ilikuwa poa sana, tulismaili kama wewe unavyosmaili kila mara lakini sasa mtu mzima, huwa unachukua muda wako kufikiria kuhusu hii laifu yetu ya kitaa ama watu wako wa karibu wanakudanganya kwamba ishu freshi tu?

Huku kwetu kimenuka ndugu yangu, watu wanapiga buku na mkwanja wa kukopa wakifikiria labda wakirudi kutoka maskonga kitaeleweka, wakirudi huku ajira zenyewe zinakuwa za kushtukiana, kama mtu hakushtukii anakupotezea, unakaa na mikaratasi yako ambayo umeisotea miaka kadhaa, wenzako wanaendelea kupeta.

Hapo ndipo mayanki wanapoanza kutafuta njia nyingine mbadala ya kuendesha laifu yao, sasa kuna taipu mbili hapa mshua, kuna wale wa kitaa ambao walikosa hata mkwanja wa kukopa, hawa ndio wanakuwa wakabaji, ile amani tunayojivunia inakuwa huko kwenu tu huku kwetu gozigozi mtindo mmoja.

Hatuna raha mshua, tukitoka kutafuta tunakabwa, tunanyang'anywa hata kile kidogo tulichonacho mwanangu, sasa hapa sisi tutakuwa tunajivunia amani gani, ndo' maana watu wanadata mpaka wanafikia kipindi wanasema bora wangezaliwa madogi mbele kuliko wanadamu bongo.
Wanashindwa hata kushtukia kwamba dogi ni dogi tu na ubinadamu una raha yake!

Misosi sasa, kila siku bei juu mwanangu, sasa hivi mpaka shuga kuweka kwente matii, imekuwa anasa, watu wanapiga chai bila mashuga wala nini, ishu za uji wa chumvi ndio zimetawala kitaani, na laifu inaendelea.

Manake imejini yuaself Mista prezident, kipato cha mtanzania ni chini ya dola moja, halafu shuga yenyewe kwa Mangi ni buku mbili, ...sema mwenyewe, unashika nini unaacha nini hapo?
Sema mwenyewe kama sio gozi gizo?

Haya, ukiachana na kesi hiyo, hivi hawa mandata a.k.a mapolisi wanafundishwa nini kule depo?
Mbona wamekuwa watu wa kutunyanyasa sana badala ya kuwa washkaji zao? Mbona wanakuwa wakitukamata wanapenda sana tuwakatie kitu kidogo kuliko kusimamia sheria kitaa kikanyooka?

Si mmewaongezea mikwanja juzi juzi tu hawa jamaa?
Sio siri nina mengi sana ya kukwambia mshua ila siimbi sasa, kama Izzo angalau umepata picha angalau kwa uchache,nila kuna ishu za maticha, manesi, na wamachinga, ishu ziko kibao mshua .

Wasaalam
 
Mwendawazimu sio lazima uvue nguo, kweli maisha kiboko, nadhani addresee wa msg hii ni yale mavuta unga a.k.a mateja walokubuhu na sio JK. Mtu unaweza kuwa na nguo zako kumbe kichaa kabisa. Mmhh aisee duh hii kali jamani kaaaa yaani looohh....

..leo imebidi nikucheki kwa njia ya Zee manake nimekuwa nikitafuta kweli njia ya kugumiana na wewe lakini watu wananibania, nikaona sio mbaya katika miaka hii Fifte ya Independensi, nikuandikie leta. Japo ni sistim ya kilongtaimu sana,
Aka fifte za Uhuru, jana tulikuwa tunacheki runinga na wanangu, tumekuskia tumekuona na tumekubali spichi yako, ilikuwa poa sana, tulismaili kama wewe unavyosmaili kila mara lakini sasa mtu mzima, huwa unachukua muda wako kufikiria kuhusu hii laifu yetu ya kitaa ama watu wako wa karibu wanakudanganya kwamba ishu freshi tu?
Huku kwetu kimenuka ndugu yangu, watu wanapiga buku na mkwanja wa kukopa wakifikiria labda wakirudi kutoka maskonga kitaeleweka, wakirudi huku ajira zenyewe zinakuwa za kushtukiana, kama mtu hakushtukii anakupotezea, unakaa na mikaratasi yako ambayo umeisotea miaka kadhaa, wenzako wanaendelea kupeta.
Hapo ndipo mayanki wanapoanza kutafuta njia nyingine mbadala ya kuendesha laifu yao, sasa kuna taipu mbili hapa mshua, kuna wale wa kitaa ambao walikosa hata mkwanja wa kukopa, hawa ndio wanakuwa wakabaji, ile amani tunayojivunia inakuwa huko kwenu tu huku kwetu gozigozi mtindo mmoja.
Hatuna raha mshua, tukitoka kutafuta tunakabwa, tunanyang'anywa hata kile kidogo tulichonacho mwanangu, sasa hapa sisi tutakuwa tunajivunia amani gani, ndo' maana watu wanadata mpaka wanafikia kipindi wanasema bora wangezaliwa madogi mbele kuliko wanadamu bongo.
Wanashindwa hata kushtukia kwamba dogi ni dogi tu na ubinadamu una raha yake!
Misosi sasa, kila siku bei juu mwanangu, sasa hivi mpaka shuga kuweka kwente matii, imekuwa anasa, watu wanapiga chai bila mashuga wala nini, ishu za uji wa chumvi ndio zimetawala kitaani, na laifu inaendelea.
Manake imejini yuaself Mista prezident, kipato cha mtanzania ni chini ya dola moja, halafu shuga yenyewe kwa Mangi ni buku mbili, ...sema mwenyewe, unashika nini unaacha nini hapo?
Sema mwenyewe kama sio gozi gizo?
Haya, ukiachana na kesi hiyo, hivi hawa mandata a.k.a mapolisi wanafundishwa nini kule depo?
Mbona wamekuwa watu wa kutunyanyasa sana badala ya kuwa washkaji zao? Mbona wanakuwa wakitukamata wanapenda sana tuwakatie kitu kidogo kuliko kusimamia sheria kitaa kikanyooka?
Si mmewaongezea mikwanja juzi juzi tu hawa jamaa?
Sio siri nina mengi sana ya kukwambia mshua ila siimbi sasa, kama Izzo angalau umepata picha angalau kwa uchache,nila kuna ishu za maticha, manesi, na wamachinga, ishu ziko kibao mshua .
Wasaalam
 
uko sawa kabisa,
maneno na avatar yako viko sawa,
wewe ongea tu na mshua mkuu wangu.
 
Mwana hii taito imenizingua kichizi mpaka kuikongotea unameaning nini, mpaka nilipochungulia ndani nikakusoma,kweli mkulu life ni chabangaa alfu ulela kamanda wangu,yaani ni full hard life. Usipime mwana sasa hivi tunaishi kimagumashi tu popote unapoona panafaa unapiga pini ung'oke na chochote, hamna michongo nowdays tunalisongesha kwa tantalila. Ebwanaeee saint ivuga bongo ishakuwa noumar bora tulisongeshe mbele mwana. Pamoko mtu wangu.pinaa!
 
Mwendawazimu sio lazima uvue nguo, kweli maisha kiboko, nadhani addresee wa msg hii ni yale mavuta unga a.k.a mateja walokubuhu na sio JK. Mtu unaweza kuwa na nguo zako kumbe kichaa kabisa. Mmhh aisee duh hii kali jamani kaaaa yaani looohh....

hahaa ..kachala wangu kausha basi ..wewe kamata meseji theni piga lapa au sio?
 
Mwana hii taito imenizingua kichizi mpaka kuikongotea unameaning nini, mpaka nilipochungulia ndani nikakusoma,kweli mkulu life ni chabangaa alfu ulela kamanda wangu,yaani ni full hard life. Usipime mwana sasa hivi tunaishi kimagumashi tu popote unapoona panafaa unapiga pini ung'oke na chochote, hamna michongo nowdays tunalisongesha kwa tantalila. Ebwanaeee saint ivuga bongo ishakuwa noumar bora tulisongeshe mbele mwana. Pamoko mtu wangu.pinaa!

kachala wangu mbele ndio usipime...huko ndio kimewaka ile mbayaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom