USSR
JF-Expert Member
- Jul 15, 2015
- 9,895
- 22,659
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Chipuputa, Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara (jina limehifadhiwa), ameripoti shuleni akiwa na mtoto mchanga.
Uongozi wa shule umesema, mtoto huyo alijifungua baada ya kuhitimu darasa la saba mwezi Oktoba mwaka jana.
USSR
---
MWANAFUNZI wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Chipuputa, Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara (jina limehifadhiwa kwa kuwa ni mtoto), ameripoti shuleni akiwa na mtoto mchanga.
Uongozi wa shule umeeleza kuwa mtoto huyo alijifungua baada ya kuhitimu darasa la saba mwezi Oktoba mwaka jana.
Wilayani hapa jana, Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Osmondi Nkanovya alibainisha kuwapo shida hiyo alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu maendeleo ya kuripoti kwa wanafunzi waliochaguliwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu.
Mwalimu Nkanovya alisema shule hiyo kwa mwaka huu wa 2023 ilipangiwa kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 194. Kati yao, wavulana ni 93 na wasichana ni 101.
Alisema Shule ya Sekondari Chipuputa imekuwa na mwenendo mzuri wa wanafunzi kuripoti shuleni kwa mwaka huu, akibainisha kuwa hadi jana, walikuwa wameripoti ni 186. Kati yao, wavulana ni 88 na wasichana 98.
Mkuu wa shule alisema kuwa kati ya wanafunzi hao, mmoja aliripoti shuleni akiwa na mtoto mchanga.
"Inaonekana wazi kwamba hata wakati anafanya mtihani wa darasa la saba, wamanafunzi huyo aliufanya akiwa na ujauzito," mwalimu huyo alisema.
Kiongozi huyo wa shule alisema mwanafunzi huyo baada ya kuripoti shuleni na mtoto mchanga, alipokewa kisha kuelezwa kuwa kwa mwaka huu hatoweza kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza, hivyo anatakiwa kwenda kumlea mtoto wake na anarejee shuleni mwakani kujiunga na kidato cha kwanza kwa ajili ya kuendelea na masomo yake.
Mwalimu huyo alisema wameshuhudia mwamko mzuri kwa wanafunzi kuripoti shuleni kwa wakati, kukiwa na wanafunzi wanane pekee (akiwamo mwenye mtoto) ambao hawajaripoti shuleni kati ya wanafunzi 194 waliopangwa kuripoti kwenye shule hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu, Mariamu Chaurembo alisema serikali wilayani humo inaendelea kuwafuatilia wazazi na walezi ambao watoto wao hawajaripoti shuleni na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Alisema wapo baadhi ya watoto ambao walipaswa kujiunga na kidato cha kwanza na tayari wamepata ujauzito, hivyo kushindwa kuripoti shuleni na serikali wilayani hapa inaendelea kufuatilia takwimu halisi za wanafunzi ambao wamepata ujauzito ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.
Uongozi wa shule umesema, mtoto huyo alijifungua baada ya kuhitimu darasa la saba mwezi Oktoba mwaka jana.
USSR
---
MWANAFUNZI wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Chipuputa, Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara (jina limehifadhiwa kwa kuwa ni mtoto), ameripoti shuleni akiwa na mtoto mchanga.
Uongozi wa shule umeeleza kuwa mtoto huyo alijifungua baada ya kuhitimu darasa la saba mwezi Oktoba mwaka jana.
Wilayani hapa jana, Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Osmondi Nkanovya alibainisha kuwapo shida hiyo alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu maendeleo ya kuripoti kwa wanafunzi waliochaguliwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu.
Mwalimu Nkanovya alisema shule hiyo kwa mwaka huu wa 2023 ilipangiwa kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 194. Kati yao, wavulana ni 93 na wasichana ni 101.
Alisema Shule ya Sekondari Chipuputa imekuwa na mwenendo mzuri wa wanafunzi kuripoti shuleni kwa mwaka huu, akibainisha kuwa hadi jana, walikuwa wameripoti ni 186. Kati yao, wavulana ni 88 na wasichana 98.
Mkuu wa shule alisema kuwa kati ya wanafunzi hao, mmoja aliripoti shuleni akiwa na mtoto mchanga.
"Inaonekana wazi kwamba hata wakati anafanya mtihani wa darasa la saba, wamanafunzi huyo aliufanya akiwa na ujauzito," mwalimu huyo alisema.
Kiongozi huyo wa shule alisema mwanafunzi huyo baada ya kuripoti shuleni na mtoto mchanga, alipokewa kisha kuelezwa kuwa kwa mwaka huu hatoweza kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza, hivyo anatakiwa kwenda kumlea mtoto wake na anarejee shuleni mwakani kujiunga na kidato cha kwanza kwa ajili ya kuendelea na masomo yake.
Mwalimu huyo alisema wameshuhudia mwamko mzuri kwa wanafunzi kuripoti shuleni kwa wakati, kukiwa na wanafunzi wanane pekee (akiwamo mwenye mtoto) ambao hawajaripoti shuleni kati ya wanafunzi 194 waliopangwa kuripoti kwenye shule hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu, Mariamu Chaurembo alisema serikali wilayani humo inaendelea kuwafuatilia wazazi na walezi ambao watoto wao hawajaripoti shuleni na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Alisema wapo baadhi ya watoto ambao walipaswa kujiunga na kidato cha kwanza na tayari wamepata ujauzito, hivyo kushindwa kuripoti shuleni na serikali wilayani hapa inaendelea kufuatilia takwimu halisi za wanafunzi ambao wamepata ujauzito ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.