Ajiunga CCM adai NCCR imejaa Ukabila, Usiri, na Ubinafsi!

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Ajiunga CCM na kuibua siri nzito NCCR




na Mwandishi Wetu



MKURUGENZI wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi taifa, Bhakome Mugeta, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku akitoa tuhuma nzito za usiri wa upatikanaji wa magari na fedha zilizotumika kwenye kampeni za uchaguzi uliopita, wakati chama hicho hakikuwa na ruzuku.

Bhakome alisema hakuna kiongozi yeyote zaidi ya Mwenyekiti James Mbatia, anayejua jinsi magari hayo zaidi ya sita aina ya Land Cruiser, yalivyopatikana wakati chama hakikuwa na fedha.

“Moja ya sababu iliyonifanya mimi nitoke NCCR-Mageuzi ni usiri, unauliza magari hayo na fedha za kampeni tumepata wapi, hupati majibu, usiri huu wa nini?” alihoji, Bhakome.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi hiyo na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, Bhakome alisema ameamua kujiunga nacho kutokana na kuridhishwa na jinsi CCM inavyokubali kukosolewa na kuchukua hatua.

“Leo naipenda CCM, kimekuwa chama bora, kinakubali kukosolewa, kujisahihisha na kuchukua hatua,” alisema Bhakome.

Alisema hali hiyo ni tofauti na kambi ya upinzani na kutolea mfano wa chama chake cha NCCR-Mageuzi kwamba kimekuwa cha kikabila, usiri, ubinafsi na sasa kimekuwa miliki ya koo.

“Wewe unanijua, nimekuwa mageuzi kwa muda mrefu sana, lakini nimefika mahala nimechoka, chama hakikui, kimebaki kukumbatia ukabila, usiri, ubinafsi na sasa kimekuwa chama cha ukoo, hakuna kukosoana,” alisema Bhakome.

Bhakome amekuwa ndani ya chama hicho tangu kilipoanzishwa na wakati wa mgogoro kati ya kambi ya aliyekuwa mwenyekiti wake wakati ule, Augustine Mrema na Katibu Mkuu, Mabere Marando, alikuwa upande wa Marando na ndio waliochangia kwa kiasi kikubwa kumbwaga Mrema, aliyeamua kukimbilia Tanzania Labour Party (TLP).

Wanachama wengine waliorejea CCM jana kutoka upinzani ni Naibu Katibu Mkuu wa UPDP, Haji Mbelwa.

Wengine ni Katibu wa CHADEMA, Wilaya ya Korogwe, Musa Sanyo na Katibu wa chama hicho, Bakari Rajab, Wilaya ya Handeni.

Makamba alisema hayo ni matunda ya CCM kukubali kujikosoa, kukosolewa na kuchukua hatua. Alisema CCM isihukumiwe kwa makosa ya watu wachache.

Wakati huo huo, CCM Mkoa wa Dar es Salaam jana ilifanya maandamano ya kuunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, aliyoitoa mwishoni mwa wiki, mjini Dodoma.
 
Wanakubali kujikosoa, kukosolewa na kuchukua hatua, eh? If this were the case then CCM would have been one damn clean party.
Hivi akina Kabourou wameishia wapi?
 
Ama kweli, mtu hatakufa kwa njaa!


"Moja ya sababu iliyonifanya mimi nitoke NCCR-Mageuzi ni usiri, unauliza magari hayo na fedha za kampeni tumepata wapi, hupati majibu, usiri huu wa nini?" alihoji, Bhakome.

"Wewe unanijua, nimekuwa mageuzi kwa muda mrefu sana, lakini nimefika mahala nimechoka, chama hakikui, kimebaki kukumbatia ukabila, usiri, ubinafsi na sasa kimekuwa chama cha ukoo, hakuna kukosoana," alisema Bhakome.



Kwa nini usitumie lugha nyepesi bw. Bhakome; Jua ni kali upinzani sio?!
...Ulidhani ni lelemama!
:)







.
 
Sasa asubiri huko CCM aone kama ataambiwa kitu. Hivi yeye haoni hata kitendawili cha EPA? Au hiyo sio siri?

Angesema tu kwamba familia imezidi kulala njaa, inabidi ajinusuru hata kama italeta fedheha.
 
Bhakome alisema hakuna kiongozi yeyote zaidi ya Mwenyekiti James Mbatia, anayejua jinsi magari hayo zaidi ya sita aina ya Land Cruiser, yalivyopatikana wakati chama hakikuwa na fedha.

"Moja ya sababu iliyonifanya mimi nitoke NCCR-Mageuzi ni usiri, unauliza magari hayo na fedha za kampeni tumepata wapi, hupati majibu, usiri huu wa nini?" alihoji, Bhakome.

Haya maneno ya huyu mzee yanahitaji kujadiliwa kwani huenda ukaja kusikia yaleyale ya Mtikila na milioni 3 ,sasa hapa huenda pakawa pagumu zaidi.....
 
makahaba wa itikadi hawa! Ni hatari kuliko nuclear warheads. Let them enjoy big reception by makamba but soon ccm will despatch them into political oblivion. Bhakome ukabila ameuona leo ? Kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi ,kwa kuondoka kwako chama kitapumua na kitapata muda wa kusimamia na kutekeleza sera za kuwakomboa watanzania .
Turncoats and political sellouts are dangerous to our society
 
vyama vya upinzani havina siri yeyote ni danganya toto tu na CCM wanaliwa kwa mtindo huo
 
Chamsingi Mbatia akanushe kuwa zile vx sita ni uzushi, then tuconclude ya bhakombe. Otherwise tutaamini NCCR umangimeza upo au wako kwenye rosta ya RA.

Siasa za kutumia njaa za watu ndio zimetawala nchini, hata hii ya "mpaka kieleweke" ni kutaka kutumia njaa za watu.

Ukweli hakuna atakayeondoa umasikini wa mwenzie, watu wanajengewa shule na kupewa elimu bure bado wanatia nanga walimu.
 
MK,

Hivi ni lini wapinzani walishawahi kumchukua Mtu kutoska CCM,Hasa Katika Nafasi ya uongozi kama Katibu Mkuu.Hii maada kwanini isifungwe sababu inabomoa Upinzani?au kwa kuwa inawahusu NCCR?
Kiundani ukiangalia lichoongea utajua kuwa kuna mambo na sababu ya yeye kuhama zinafanana na matztizo yaliyoko CHADEMA na siyo NCCR..

Alisema hali hiyo ni tofauti na kambi ya upinzani na kutolea mfano wa chama chake cha NCCR-Mageuzi kwamba kimekuwa cha kikabila, usiri, ubinafsi na sasa kimekuwa miliki ya koo.
 
MK,

Hivi ni lini wapinzani walishawahi kumchukua Mtu kutoska CCM,Hasa Katika Nafasi ya uongozi kama Katibu Mkuu.Hii maada kwanini isifungwe sababu inabomoa Upinzani?au kwa kuwa inawahusu NCCR?
Kiundani ukiangalia lichoongea utajua kuwa kuna mambo na sababu ya yeye kuhama zinafanana na matztizo yaliyoko CHADEMA na siyo NCCR..

Kumbe jambo likiwa linakihusu CHADEMA hata kama linabomoa CHADEMA ni ruksa ,ila kama linahusu chama kingine hilo ndio linabomoa Upinzani?

Naamini kuwa kwenye jukwaa hili kila chama kinajadilika ama kwa mazuri ama kwa mabaya yake sasa kusema kuwa mada ifungwe naona kama sikuelewi vile .....

Nafikiri kuwa jambo jema zaidi ni kukosoana na huko ndiko kunaweza kusaidia kujenga kuliko kusema tuu kuwa mada ifungwe kwa vile tuu haiwahusu CCM ama CHADEMA.
 
Ajiunga CCM na kuibua siri nzito NCCR




na Mwandishi Wetu



MKURUGENZI wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi taifa, Bhakome Mugeta, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku akitoa tuhuma nzito za usiri wa upatikanaji wa magari na fedha zilizotumika kwenye kampeni za uchaguzi uliopita, wakati chama hicho hakikuwa na ruzuku.

Bhakome alisema hakuna kiongozi yeyote zaidi ya Mwenyekiti James Mbatia, anayejua jinsi magari hayo zaidi ya sita aina ya Land Cruiser, yalivyopatikana wakati chama hakikuwa na fedha.

“Moja ya sababu iliyonifanya mimi nitoke NCCR-Mageuzi ni usiri, unauliza magari hayo na fedha za kampeni tumepata wapi, hupati majibu, usiri huu wa nini?” alihoji, Bhakome.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi hiyo na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, Bhakome alisema ameamua kujiunga nacho kutokana na kuridhishwa na jinsi CCM inavyokubali kukosolewa na kuchukua hatua.

“Leo naipenda CCM, kimekuwa chama bora, kinakubali kukosolewa, kujisahihisha na kuchukua hatua,” alisema Bhakome.

Alisema hali hiyo ni tofauti na kambi ya upinzani na kutolea mfano wa chama chake cha NCCR-Mageuzi kwamba kimekuwa cha kikabila, usiri, ubinafsi na sasa kimekuwa miliki ya koo.

“Wewe unanijua, nimekuwa mageuzi kwa muda mrefu sana, lakini nimefika mahala nimechoka, chama hakikui, kimebaki kukumbatia ukabila, usiri, ubinafsi na sasa kimekuwa chama cha ukoo, hakuna kukosoana,” alisema Bhakome.

Bhakome amekuwa ndani ya chama hicho tangu kilipoanzishwa na wakati wa mgogoro kati ya kambi ya aliyekuwa mwenyekiti wake wakati ule, Augustine Mrema na Katibu Mkuu, Mabere Marando, alikuwa upande wa Marando na ndio waliochangia kwa kiasi kikubwa kumbwaga Mrema, aliyeamua kukimbilia Tanzania Labour Party (TLP).

Wanachama wengine waliorejea CCM jana kutoka upinzani ni Naibu Katibu Mkuu wa UPDP, Haji Mbelwa.

Wengine ni Katibu wa CHADEMA, Wilaya ya Korogwe, Musa Sanyo na Katibu wa chama hicho, Bakari Rajab, Wilaya ya Handeni.

Makamba alisema hayo ni matunda ya CCM kukubali kujikosoa, kukosolewa na kuchukua hatua. Alisema CCM isihukumiwe kwa makosa ya watu wachache.

Wakati huo huo, CCM Mkoa wa Dar es Salaam jana ilifanya maandamano ya kuunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, aliyoitoa mwishoni mwa wiki, mjini Dodoma.

Hivi huyu ni Bhakome yupi ? Maana kama ni huyu Mzee basi hana lolote ni mnafiki sana .Ninamtambua kwa majungu na Bhakome na Tambwe wakisimama mbele yangu hawataweza kusema .I will come back nieleze upuuzi wake , huyu mkabila mkubwa .Mtu yeyote mbaguzi na mkabila akiishiwa hoja ataleta ukabila wake .Njaa yake ndiyo inamfanya ana fedheheka ila CCM nao wameamka hawawataki watu aina yake .Kilimbah na wenzake wamewahi lakini walio bakia hakuna kitu kabisa .Pole zao maana wanacheza ngoma ya Makamba another failure ndani ya CCM .
 
Hivi huyu ni Bhakome yupi ? Maana kama ni huyu Mzee basi hana lolote ni mnafiki sana .Ninamtambua kwa majungu na Bhakome na Tambwe wakisimama mbele yangu hawataweza kusema .I will come back nieleze upuuzi wake , huyu mkabila mkubwa .Mtu yeyote mbaguzi na mkabila akiishiwa hoja ataleta ukabila wake .Njaa yake ndiyo inamfanya ana fedheheka ila CCM nao wameamka hawawataki watu aina yake .Kilimbah na wenzake wamewahi lakini walio bakia hakuna kitu kabisa .Pole zao maana wanacheza ngoma ya Makamba another failure ndani ya CCM .

Kaka ukisema ana majungu kipindi hiki wakati amehama NCCR hujafanya kitu tutakulaumu wewe! kumbe ulikuwa unajua kuwa ndani ya NCCR kuna mamluki?

KWA KIFUPI VYAMA VYOTE VYA UPINZANI MNAVYOJARIBU KUVITETEA HAPA HAVINA MPANGO WOWOTE NA MAPAMBANO YA UFISADI VYAMA KAMA NCCR, CUF,TLP they are pieces of scrap! mnatpoteza muda wenu kujaribu kuvitetea mtapoteza muda hawana na hawatakuwa na mpango wa kupigania hali bora za wananchi Tanzania.they need money(ruzuku) na hoja zote ambazo huyo bwana anazungumza, waache wakaangane wenyewe!!!
 
Anasahau kwamba CCM imejaa mafisadi, waroho wa utajiri wa haraka haraka walioweka maslahi yao mbele badala ya Taifa na wahuni wanaojifanya viongozi. Watu watasema chochote kile ili kuhalalisha kuhamia kwao CCM, kumbe wanaruka haja ndogo na kukanyaga haja kubwa!!!
 
MSIMSHANGAE BHAKOME KUHAMA WAKATI MBATIA MWENYEWE KAHAMA SIKU NYINGI
Jamani mnamshangaa Bhakome kuhamia CCM! Mbona Mbatia kahamia CCM siku nyingi? Mbatia anachokifanya pale ni usanii tu wa press-conference kibao! Wewe umeona wapi chama kikaendeshwa kwa press conference? Hiyo ndo staili ya Mbatia: usiku ana kula CCM, mchana press conference!
 
Back
Top Bottom