KERO Ajira za Watanzania katika Mradi wa EACOP ziangaliwe kwa karibu na Serikali

KERO Ajira za Watanzania katika Mradi wa EACOP ziangaliwe kwa karibu na Serikali

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mradi wa EACOP ulianza mwaka 2021 na sasa mwaka 2026 unakaribia kufikia mwisho. Hata hivyo, kuna wasiwasi mkubwa kuhusu utekelezaji wa mpango wa uhamishaji wa ujuzi na urithishaji wa nafasi (succession plan), hususan kwa wafanyakazi wa Kitanzania.


Kwa zaidi ya miaka minne, Watanzania wamefanya kazi na kupata uzoefu mkubwa katika maeneo mbalimbali kama HSE, Mazingira, HR, Uhandisi na taaluma nyingine muhimu. Pamoja na uzoefu huo, wengi wao wanaondolewa baada ya mikataba yao kuisha, huku baadhi ya wataalamu wa kigeni wakiendelea kubaki katika nafasi ambazo zinaweza kufanywa kwa ufanisi na Watanzania.

Suala hili linaibua maswali kuhusu utekelezaji wa sera za Local Content na uhamishaji wa ujuzi ambazo zilipaswa kuwa miongoni mwa faida kuu za mradi huu kwa taifa. Watanzania wamechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya mradi huu na wanastahili kupewa nafasi ya kuendeleza taaluma zao na kutumia uzoefu walioupata.

Tunaiomba Serikali, , , na kufuatilia kwa karibu suala hili ili kuhakikisha kuwa fursa za ajira, maendeleo ya taaluma na uhamishaji wa ujuzi vinawanufaisha Watanzania kama ilivyokusudiwa.

Local Content isibaki kwenye ripoti pekee; ionekane katika ajira, uongozi na fursa zinazotolewa kwa Watanzania ndani ya miradi mikubwa ya kimkakati. 🇹🇿
 
Mradi wa EACOP ulianza mwaka 2021 na sasa mwaka 2026 unakaribia kufikia mwisho. Hata hivyo, kuna wasiwasi mkubwa kuhusu utekelezaji wa mpango wa uhamishaji wa ujuzi na urithishaji wa nafasi (succession plan), hususan kwa wafanyakazi wa Kitanzania.


Kwa zaidi ya miaka minne, Watanzania wamefanya kazi na kupata uzoefu mkubwa katika maeneo mbalimbali kama HSE, Mazingira, HR, Uhandisi na taaluma nyingine muhimu. Pamoja na uzoefu huo, wengi wao wanaondolewa baada ya mikataba yao kuisha, huku baadhi ya wataalamu wa kigeni wakiendelea kubaki katika nafasi ambazo zinaweza kufanywa kwa ufanisi na Watanzania.


Suala hili linaibua maswali kuhusu utekelezaji wa sera za Local Content na uhamishaji wa ujuzi ambazo zilipaswa kuwa miongoni mwa faida kuu za mradi huu kwa taifa. Watanzania wamechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya mradi huu na wanastahili kupewa nafasi ya kuendeleza taaluma zao na kutumia uzoefu walioupata.


Tunaiomba Serikali, , , na kufuatilia kwa karibu suala hili ili kuhakikisha kuwa fursa za ajira, maendeleo ya taaluma na uhamishaji wa ujuzi vinawanufaisha Watanzania kama ilivyokusudiwa.


Local Content isibaki kwenye ripoti pekee; ionekane katika ajira, uongozi na fursa zinazotolewa kwa Watanzania ndani ya miradi mikubwa ya kimkakati. 🇹🇿
 
Kwa mambo ya ufundi, Welding specifically tumepigwa, Teknolojia inayotumika ni rahisi hata mtoto wa darasa la tano anaweza kuoperate Automatic welding machine, ila mafundi wa kibongo 50 waliobahatika kupelekwa kwenye mafunzo ya ufundi na mradi (chuo cha ufundi arusha) hawaruhusiwi hata kusogelea welding house(banda la kuchomea) Afisa wa EWURA anapita anauliza mnafanya kazi za kuchomelea?
Welder anaanzaje kujibu hapana; mbele ya mwajiri wake?
Mawelder wanaishia kufanya kazi kama vibarua na kazi ndogo ndogo za repair.

Wengine walipoona hvyo waliamua kuacha, Watu wa HR tena watanzania wanaamua kumstiri mchina kwa kufoji vyeti na kuingiza vijana ambao hawana taaluma hyo ili ukaguzi ukipita wanatolewa mawelder( wamchongo) ili EWURA warizike.

Kama ni kipato kweli wamepata ila kama kulikuwa na maono ya kuja kuwa na watu wa kutegemewa kwa miradi kama hii mbeleni, tumefeli 100%
 
Sasa kama mradi unakamilika maana kazi zinakwisha mfano civil works sasa utaendelea kubaki site kufanya nini mkuu.
 
Back
Top Bottom