Ajira za TANROADS: Kuna Harufu ya Ubaguzi na Upendeleo

Mkuu Mwita Maranya siku hizi mashirika ya umma karibu yote yanatumia mtindo huo wa hovyo kupitiliza.

Ukitia mguu AUWASA Mamlaka ya Maji jijini Arusha yuko afisa mwajiri mpare/mchagga yeye anahakikisha tatizo la ajira kijiji alichozaliwa na familia yake linamalizwa kama si kupunguzwa na uwepo wake AUWASSA.

Sasa mkuu ni kwanini tuendelee kufumbia macho vitendo kama hivi vinavyofanywa na wahuni wachache kwa manufaa yao na familia zao? mashirika ya umma na idara/wizara za serikali lazima ziwe na utaratibu unaowawezesha watanzania wote kuajirika bila vikwazo.

Nadhani katika hili tuna jukumu la kufanya nadhani tunalazimika sasa kuwamulika wale wote wanaotumia ofisi za umma kwa manufaa yao binafsi kwa kuwabagua wengine na kuwapendelea ndugu, jamaa na marafiki zao.
 
Hata hii habari uliotoa ina harufu ya ubaguzi mkubwa. Binafsi siwezi nikachangia kabisa kwa kuwa umewalenga rafiki zako unaowajua na umewakopi kwa kuonyesha msisitizo. Hali hii ni mbaya sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu. Napinga kwa sauti kuu huu ubaguzi ulioufanya. Kama umeufanya kwa makusudi basi mungu akuhukumu kwa dhambi ya ubaguzi, na kama ni bila kufahamu basi mungu akusamehe kwa kuwa hujui ulitendalo.

Ndugu zangu kiroba na Bajabiri acheni jazba, tunaomba mawazo yenu katika hili, si jambo rahisi kama mnavyotaka kuliweka kwamba ningeweza kuwataja wanaJF wote katika uzi huu, na ndio maana utaona nimesema na wanaJF wengine na hapo ndipo mnapopatikana. Kama mmejisikia vibaya naomba kuwatoa wasiwasi kwamba ninathamini sana mawazo ya kila mwanaJF na ninyi wawili ni miongoni mwa watu ambao ninathamini mawazo yenu.

Kwakuwa haya mambo tunayajadili kwa ajili ya faida ya wadogo zetu, ndugu zetu na taifa letu tuache haya mambo madogo madogo na tujikite kwenye hoja ya msingi.
 
Last edited by a moderator:
Ila kwa sasa kutokana na Serikali yenu kushindwa kutoa ajira kwa vijana wake. Inabidi SERA ZA ILMU KUBADILIKA NA kujikita KUWAFUNDISHA VIJANA KUJIAJIRI kama wanavyofanya jirani zenu kenya na Uganda.

Ukiwa katika nchi hizo Vijana wanafundishwa somo la Ujasiriamali, Uchumi na Uzalendo tokea wakiwa primary school na ni lazima kwa kila mwanafunzi kusoma somo hilo ima uwe unachukua sayansi, Arts au Biashara.

Ni vizuri na Tanzania mbadilike ili muweze kwenda na wakati ikiwa pamoja na kuwaandaa vijana kupambana na maisha kwa njia ya kujiajiri.

Nakupa pongezi Ashadii kwa upembuzi na mchango wako katika uzi huu.


Mkuu Barubaru,

Nakubaliana kabisa na unalosema... Haswa kwa wakati huu ambapo vyuo vya elimu ya juu vimeongezeka kwa kasi hivyo wahitimu kuongezeka kila mwaka pia (kama ni kiwango halisia ama chini ya kiwango that is another matter..).

Kikubwa naweza sema ni kuwa mimi kwa sasa nimeona kuwa kujiajiri kumeenda kukikuwa sasa kwa vijana wanaomaliza elimu ya vyuo ukilinganisha na hapo kati. Ingawa inakuwa taratibu lakini ni wazi kuwa kuna wale ambao wanathubutu kuanzisha vitega uchumi vyao. Na sababu wengi sana wanataka akimaliza chuo awe na kazi za maofisini unakuta kuna baadhi ambao wameanzisha taasisi za sandukuni (brief case office) hasa maeneo ya mijini ikilenga sio kile ambacho kipo katika karatasi bali end result ambayo mara nyingi ni kutoka (ki pesa na ki maisha).

Hili tatizo la ukosefu wa ajira ni kubwa ukiliangalia kwa upana (weka pembeni usugu wake); inayopelekea hatari ya kukuza matatizo mengine ambayo yanabomoa kabisa maadili na taratibu kubadilisha tamaduni za Mtanzania ambae ni mtu wa kuaminika, upendo na ukarimu. Tutakuwa kama wa Nigeria mda sio mrefu...

BTW Barubaru, I am humbled by your acknowledgement... Pamoja saaana.
 
Ndugu yangu Barubaru bado tuko pamoja hapa JF basi tu inatokea kwamba hatukutani mara kwa mara kama zamani, nahisi umebadilisha muda wa kuvisit JF.

Hata hivyo ninakubaliana kwa sehemu kubwa na maelezo yako kwakuwa una uzoefu wa kutosha na ajira za serikali yetu ya JMT.

Ni kweli kwamba shift incharge/supervisor wamezingatia kupata watu wenye uzoefu, lakini kama ungekuwa unafahamu structure ya weigh bridge ungegundua kwamba hakuna ulazima wa kuweka kigezo cha umri mkubwa sana kiasi hicho. Kwa uzoefu wangu na hawa watu wa mizani mara nyingi maoperator ambao wamefanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja hadi miaka miwili ndio wamekuwa wakiwapromote kuwa shift incharges na wanaperform vizuri sana.

Kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba mizani nyingi zinakuwa na shift mbili kwa siku, except mzani wa kibaha ambao una shift tatu kwa siku. Kila shift inakuwa na incharge wake(shift incharge) lakini papo hapo kunakuwa na overall incharge na juu yake kuna weighbridge supervisor, kwahiyo hawa mashift incharge wanafanya kazi kwa karibu sana na maoverall incharge na weighbridge supervisor.

Kwa utafiti nilioufanya katika baadhi ya mizani, wengi wa hawa mashift incharge na overall incharge ni watu wenye elimu za FTC, Ordinary Diploma na wachache wenye shahada. Na hata ma weigh bridge supervisors wako mchanganyiko, wenye FTC na Shahada/stashahada.

Angalizo lako nitalifanyia kazi, si vibaya kama unaifahamu hiyo human resource policy hasa hiyo SOS ili kunisaidia kukamilisha kazi yangu.

Mwita maranya.

Kwa kuwa umeamua kufanya utafiti wa AJIRA TANROADS , ni vizuri uwe na reference ili kualalisha utafiti wake.

Kwa hilo nakushauri pitia HR ofisi za Tanroads na ulizia Human Resource manual (HRM)ambayo ndio mwongozo wa kazi na ndanimwe kuna SOS na ndio siku zote inayotumika kutoa vigezo, stahiki, haki , wajibu na weledi wa kila kazi na pia katika kutangaza ajira sehemu yoyote ya kazi.


Na hii napatikana kwa Afsa mwajiri yoyote au Afisi yake kwani ndio mwongozo wa kazi zake za kila siku.
 
Mwita Maranya,

Harufu ya ubaguzi na upendeleo wa ajira katika nchi yetu limeishakuwa jambo la kawaida sio TANROAD tu karibia wizara zote bila kushikwa mkono huwezi kupata ajira.

Sasa ritz hapa ndipo tunatakiwa kuanzia, kwamba tuendelee kuwaachia walioko maofisini waendelee kufanya upendeleo na ubaguzi ama tunakate na kuchukua hatua za kurekebisha hali hiyo? nadhani kwa pamoja tuna wajibu wa kukemea kwa nguvu zote mambo hayo ili ofisi za umma zipate watu wenye uwezo na sifa badala ya kujaza makabila yetu, marafiki zetu na watoto wetu katika ofisi za umma.
 
SG8,

Kama unavyoelewa sasa hivi kuna uchakachuzi mkubwa sana, CV za watu ni fake (kuna mtu ana CV ipo very impressive ila ukweli pekee wa hio CV ni Jina lake na elimu ya Secondary). Kupunguza zoezi la form zitakazo pokelewa moja ya strategy huwa wanaweka range ya umri ambayo wanaamini kuwa mtu wa umri huwa kweli anayo experience (hasa kwa nafasi za kazi ambazo experience ni muhimu).

Walau huo ndio mtazamo wangu.
AshaDii,
Nimekuelewa lakin bado nina doubts! Vipi kuhu range hiyo ya miaka mitano..Kwani wangetuamia tu sera ya serikali inayosema ajira kwenye Public Service (kwa permanent and pensionable terms) maximum age ni 45 wangekosa watu wenye sifa hizo? I.e nina swali kwanini wasiseme 35-45? Na kama ni uzoefu mara nyingi inatakiwa iwe katika similar au related position na kwenye taasisi inayofanana au kukaribiana kwa kesi ya TANROADS maana yake kwenye Government Agencies zingine au taasisi nyingine za serikali. Mimi nahisi labda kuna mambo mawili
1. Wanataka ku recruit from within i.e kuna watu wenye sifa hizo ndani ya Tanroads pengine kuna watu walikuwa wanafanya kwa contracts au kwa kujitolea, au
2.Kuna watu wao waliondaliwa na wenye sifa kama hizo
 
Last edited by a moderator:
Dah,una nigusa sana.
Wengi tuna tamani kujiajiri sana,lakini sio kwamba tumekuwa wavivu la hasha.

By the way AshaDii natafuta kazi pia,nipe mchongo basi.
Huu wa Tanroads mh,hamna changu hapo.


Dah.. Tayari? Siku zinaenda kasi eeh? Lol. This will be best discussed via pm... Karibu Speaker. Pamoja saana.
 
Hili jambo yafaa liingizwe katika katiba mpya tunayoitarajia na waziri mwenye dhamana na masuala ya ajira atengeneze kanuni zitakazo ondoa mianya ya upendeleo.

Nilisema tangu mwanzo mashirika karibu yote yameshatembelewa na huyu mdudu undugunization,ukabilanization na udininization.Tembelea TRA,CRDB utakumbana na undugu na ukabila.Ukitia pua NSSF yuko mdudu udini anatawala utadhani nchi hii haina serekali.


Sasa mkuu ni kwanini tuendelee kufumbia macho vitendo kama hivi vinavyofanywa na wahuni wachache kwa manufaa yao na familia zao? mashirika ya umma na idara/wizara za serikali lazima ziwe na utaratibu unaowawezesha watanzania wote kuajirika bila vikwazo.

Nadhani katika hili tuna jukumu la kufanya nadhani tunalazimika sasa kuwamulika wale wote wanaotumia ofisi za umma kwa manufaa yao binafsi kwa kuwabagua wengine na kuwapendelea ndugu, jamaa na marafiki zao.
 
Ni bora kabisa Mwita maranya amelibainisha hili na kutaka tulijadili kwa kina ili kupata suluhu yake na sio kubaki watu wa kulalama.

Kwani Mwl JK Nyerere aliwahi kusema katika moja ya hotba zake akanena Wazanaki wanasema “ UBUBISUBISU OBUWERE EKIRO KIRIMBURA” akiwa na maana ya MFICHAFICHA MARADHI KILIO KITAMFICHUA.
Hongera sana Mwita M
 
AshaDii,
Nimekuelewa lakin bado nina doubts! Vipi kuhu range hiyo ya miaka mitano..Kwani wangetuamia tu sera ya serikali inayosema ajira kwenye Public Service (kwa permanent and pensionable terms) maximum age ni 45 wangekosa watu wenye sifa hizo? I.e nina swali kwanini wasiseme 35-45? Na kama ni uzoefu mara nyingi inatakiwa iwe katika similar au related position na kwenye taasisi inayofanana au kukaribiana kwa kesi ya TANROADS maana yake kwenye Government Agencies zingine au taasisi nyingine za serikali. Mimi nahisi labda kuna mambo mawili
1. Wanataka ku recruit from within i.e kuna watu wenye sifa hizo ndani ya Tanroads pengine kuna watu walikuwa wanafanya kwa contracts au kwa kujitolea, au
2.Kuna watu wao waliondaliwa na wenye sifa kama hizo


Maelezo yako pamoja na maswali yako SG8 ni ya msingi sana. Labda nikudokeze tu kwa kadri nilivyopita pita huko kwenye mizani, wafanyakazi wao wengi kwa sasa wanafanya kwa mikataba ya mwaka mmoja mmoja ambao unakuwa renewable subject to satisfactory performance. Kwa mujibu wa matangazo ya sasa watapewa mikataba ya miaka miwili ambayo pia itakuwa renewable. Na aina hii ya ajira kwa watu wa mizani imekuwa inawanufaisha zaidi waajiri(tanroads mikoa) kuliko kawaida, wakati wa kurenew mkataba na ajira mpya hapo watu hulazimika kuingia mifukoni ili wapate ajira, hili nitalielezea vizuri kwenye andiko ninaloliandaa.

Sijakuwa na figure kamili lakini kwa aina hii ya matangazo wanayoyatoa kuna watu wengi sana watapoteza ajira ambao tayari wanafanya kazi huko tanroads. Sasa inawezekana ni mbinu ya kuwakatisha tamaa walioko nje ili kuwalinda walioko tanroads tayari ama ni mbinu ya kuwaleta watu wao na kuwaondoa walioko ndani.

Kuna vijanawengi sana wamekuwa wakiajiriwa kwenye mizani kama weighbridge operators ambao wamesoma kozi ya Logistics and Transport management, sasa hao kwa vigezo hivi vya sasa ni moja kwa moja wameshapoteza kazi zao mara mikataba yao itakapofikia kikomo, hakuna matumaini ya kurenew mikataba kama sifa zilizotajwa zitazingatiwa.
 
Last edited by a moderator:
kuna kipindi haka katabia kalipotea lakini sasa naona kamerudi kwa kasi ya ajabu. Nakumbuka vijana wa france walianzisha timbwili la ajabu mpaka kikaeleweka, tatizo letu tz ni kukosa umoja, usaliti na woga usio na msingi. Vijana wangekuwa wamoja hili ni swala la wiki moja tu
 
Maelezo yako pamoja na maswali yako SG8 ni ya msingi sana. Labda nikudokeze tu kwa kadri nilivyopita pita huko kwenye mizani, wafanyakazi wao wengi kwa sasa wanafanya kwa mikataba ya mwaka mmoja mmoja ambao unakuwa renewable subject to satisfactory performance. Kwa mujibu wa matangazo ya sasa watapewa mikataba ya miaka miwili ambayo pia itakuwa renewable. Na aina hii ya ajira kwa watu wa mizani imekuwa inawanufaisha zaidi waajiri(tanroads mikoa) kuliko kawaida, wakati wa kurenew mkataba na ajira mpya hapo watu hulazimika kuingia mifukoni ili wapate ajira, hili nitalielezea vizuri kwenye andiko ninaloliandaa.

Sijakuwa na figure kamili lakini kwa aina hii ya matangazo wanayoyatoa kuna watu wengi sana watapoteza ajira ambao tayari wanafanya kazi huko tanroads. Sasa inawezekana ni mbinu ya kuwakatisha tamaa walioko nje ili kuwalinda walioko tanroads tayari ama ni mbinu ya kuwaleta watu wao na kuwaondoa walioko ndani.

Kuna vijanawengi sana wamekuwa wakiajiriwa kwenye mizani kama weighbridge operators ambao wamesoma kozi ya Logistics and Transport management, sasa hao kwa vigezo hivi vya sasa ni moja kwa moja wameshapoteza kazi zao mara mikataba yao itakapofikia kikomo, hakuna matumaini ya kurenew mikataba kama sifa zilizotajwa zitazingatiwa.
Ok kama watu wanafanya kwa mkataba wa muda tena wa mwaka mmoja kuna sababu ya kuweka kigezo cha umri? Mimi najiuliza sana, mtu mwenye miaka 41+ hawezi kufanya kazi kwa mkataba wa miaka miwili akarenew baada ya miaka miwili hata kwa miaka 10? Why below 40 kama huhitaji kumtumia huyu kwa muda mrefu? Kwa wale wanaoajiriwa kwa permanent terms ni lazima iwe below 45 ili wa qualify kuwa pensionable ambayo ni lazima iwe miezi 180 (miaka 15), je, hawa wanaweka limitations za umri wa juu kwa faida ya nani? WAMEANDAA WATU WAO!!! Nchi hii inakokwenda ipo siku vijana watavamia Ikulu kwa sababu ya kukosa ajira na fursa za kujiajiri
 
swala la ubaguz na upendeleo kwenye ajira limekuwa km mila na destur kwa sasa tz,vijana wanafundishwa ujasiriamal but nyenzo za kujiajir ndio tatizo na serikal haitoi support,hata ikitoka mikopo yaishia kwa wajanja wachache ambao ni wabinafc wasoweza kubun jambo ambalo litanufaisha na vijana wengine mayb kwakuwaajir.tz ya sasa huna ndugu kwenye system utasota sana na elinu au hata uwezo binafsi ulionao while vilaza wakipeta 2 kwenye position mbalimbal.hii ndo tz ful kubebana mbma mifam hai tunayo wakuu!
 
mwiTa, nipo kwenye tukutuku, nimeiona nakala yangu, vuta subira nitaweka kamchango kangu tukutuku ikisimama. Niombee kasinikwanyue kisigino.
 
mwiTa, nipo kwenye tukutuku, nimeiona nakala yangu, vuta subira nitaweka kamchango kangu tukutuku ikisimama. Niombee kasinikwanyue kisigino.


Mkuu nimekuwa nikikuombea muda wote naamini kisigino kimesalimika, sasa nasubiri tu kamchango kako.
 
Salam WanaJF,

Kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wadau wa sekta ya usafirishaji juu ya vitendo vya rushwa na ubabe vinavyofanywa na watendaji ama watumishi wa mizani zilizopo maeneo mbalimbali nchini kwa upande mmoja. Kwa upande wa pili kumekuwa na malalamiko toka kwa wafanyakazi wa mizani hizo hasa weighbridge operators na shift incharges kulalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na mameneja wa mizani hizo katika mikoa mbalimbali nchini.

Kutokana na hali hiyo nimelazimika kufanya kautafiti kadogo ili walau kujua ukweli wa tuhuma hizi. Kuna vitu vichache namalizia kabla sijaweka bayana findings zangu kuhusu malalamiko hayo. Muda si mrefu nitaweka hapa ripoti yangu hapa JF.

Nikirudi katika mada ya leo kama kichwa cha habari kinavyosomeka; hivi karibuni Mameneja wa Tanroads wa mikoa yenye mizani (weigh bridges) wamekuwa wakitoa matangazo ya ajira kwa nafasi za Shift Incharge na Weigh Bridge Operators. Matangazo ya hivi karibuni kabisa ya ajira hizo ni katika mikoa ya Mwanza, Pwani na Morogoro.

Mojawapo ya sifa za lazima kwa waombaji ni kama ifuatavyo:

1. Shift Incharge;
a) Awe na elimu ya shahada ya kwanza [bachelor] ama Stashahada ya juu [Advanced Diploma] katika fani yoyote toka taasisi ya elimu ya juu inayotambulika na
b) Awe na umri kati ya miaka 35 hadi 40

2. Weighbridge Operator;
a) Awe na elimu ya Fundi Mchundo[FTC] katika fani za Umeme [Electrical Eng.], Ujenzi [Civil Eng.] au Mitambo [Mechanical Eng.] na
b) Awe na umri usiozidi miaka 35.

Kimsingi sina tatizo kabisa na kigezo cha elimu, isipokuwa hapo kwenye umri. Nimekuwa nikijiuliza masawali kadhaa bila kupata majibu, nikaona ni vizuri niwashirikishe maGT hapa ili tusaidiane kulitazama suala hili kwa pamoja. Vijana wengi sasahivi wanahitimu shahada/ stashahada za juu wakiwa na umri kati ya miaka 22-25, na wapo vijana wengi sana wenye uwezo mkubwa wa kushika nafasi za majukumu makubwa hata kuliko hiyo nafasi ya shift incharge. Na kwa kuwa wenye umri wa miaka 35 hadi 40 ambao wana elimu ya kiwango cha shahada/stashada ya juu watakuwa ni watu wenye kazi zao mahali kwingineko, hivyo basi kunakuwa hakuna mantiki ya kuweka kigezo cha umri mkubwa kiasi hicho katika ajira kama hizi.

Kwa mtazamo wangu naona kama kuna ubaguzi kama si upendeleo wa dhahiri katika ajira hizi za Tanroads, sina uhakika kama watu wenye umri huo mkubwa kiasi hicho ndio pekee wanaweza kuhimili majukumu ya kazi ya shift incharge. Nadhani hapa kuna mazingira ya mameneja wa Tanroads mikoa ama wizara ya ujenzi ama Tanroads makao makuu kuajiri watu wao wanaowataka wao, na kwa kufanya hivyo wanakuwa wanakiuka katiba yetu ya JMT pamoja na kufanya upendeleo wa wazi kwa baadhi ya kundi fulani la watanzania kwa kuwabagua wengine.

Na kwakuwa kama taifa tunakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana, nilidhani Tanroads kama taasisi ya umma inawajibika kuisaidia serikali katika kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana badala ya kuweka vigezo ambavyo vinadhihirisha wazi kwamba wanataka kuendelea kufanya "recycling" ama kujuana.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa mawazo yenu na mitazamo yenu katika hili.

Copy kwa Asprin, Invisible, Ngongo, chama, Ritz, zomba, AshaDii, Dark City, Preta, WiseLady, Molemo, Nguruvi3, Mkandara, Mag3, Ben Saanane, fmpiganaji, Filipo, Crashwise, Mzee wa Rula, LiverpoolFC, Mungi, jogi, Rutashubanyuma, Nicholas, Daudi mchambuzi, Mtambuzi, Mchambuzi, nngu007, n00b na wengine.
Thank you comrade Mwita Maranya,

Hii tabia ya masharika ya umma kuendekeza nepotism ndiyo inayoua masharika yetu.Nepotism ni lazima izae utamaduni wa kulindana(culture of inmpunity). Watu hawaajiriwi based on merits.Tunazingatia kujuana n.k.Hii ni dalili ya Jamii isiyojua vipaumbele vyake.

Shirika kama TANESCO limekua katika mstarui wa mbele katika ufisadi na kadhia nyingi za aina hiyo.Ni aibu kubwa kwa shirika la umma lililopewa m,ajukumu makubwa kabisa kama injini ya kuchochea maendeleo yetu kama taifa kuwa mstari wa mbele katika kuonyesha tabia chafu kama hii.TANESCO ni taswira halisi ya kushindwa kwetu kama taifa.

Sasa tunahitaji kukabiliana na sura hii yenye madoa doa ya kujitakia kwa kufanya radical reform katika mfumo wetu.TANESCO na mashirika mengine yenye sura hiyo ya madoa doa yamepaliliwa na mfumo mbovu na sera zinazoendekeza fikra mgando katika utendaji na uendeshaji wa serikali na hivyo kuzidi kurudisha nyuma taifa letu.

Transparency katika mashirika ya umma inaonekana kama vile hakuna umuhimu.Mfumo wetu na sera za chama tawala zina-condone in one way or another kukosa uawzi katika uendeshaji wa mashirika ya umma jambo ambalo linachochea zaidi ufisadi na kulindana.

Corruption:This is the major and the grand master of Tanzania's and Tanzanian's problems. Sometimes We seem to have a legal framework in place but the grand killer by the name corruption will not allow anything work here in this country. If we can stamp corrruption by dealing decisively with corrupt Tanzanians in both public and private parastatals either by serious imprisonment or execution depending on the nature and degree of involvement that people wloud embrace the need for transparency and accountability in governance and resource management and its then every other problem will naturally fizzle away or be reduced to the bearest minimum

Pia na sisi wananchi hadi sasa tunachangia kwa kiasi kikubwa kuendeleza utamaduni huu mchafu.

TANZANIANS: This one is like the root cause of virtually all our problems. We as Tanzanians are uncouth, tribalistic, mannerless, corrupt, impatient, obsessed with power, oppressive, spiteful and hateful, persimmistic and lacadesical towards everything. We are too hopeful (on God) to fix all our glaring problems. Only a Tanzanian will be in Chruch on a Monday morning around 8.am - 2 pm praying for a job rather than walking the streets distributing C.Vs.

All this has led to a nationwide frustration which is why everyday, we keep coming out with new get rich quick schemes like armed robbery, Gold & Precious stones(like TANZANITE) trafficking, kidnapping, advance fee fraud, name it, we do it.
 
Mkuu Mwita Maranya,

Asante kwa kunishirikisha katika mada hii muhimu; Binafsi nadhani suala la UMRI huzingatiwa kwa sababu moja rahisi sana – kwamba Umri na Uzoefu Vinaenda Sambamba; Hili ni suala ambalo wadau wengine kama barubaru n.k, wamelizungumzia vizuri; Lakini hoja yako kuhusu mfumo wetu wa Elimu in relation to vigezo hivi vya ajira bado ina mashiko. Mimi nadhani mbali ya Umri na Uzoefu, kuna other factors at play, ingawa sijui ni factors vipi, sana sana nitaishia kutoa tu OPINIONS kuliko FACTS;

Baada ya kusema hayo, mimi nadhani suala muhimu pia la kutazama ni kwamba – Tanroads ni Sekta ya UMMA, hivyo watumishi wake wote ni watumishi wa UMMA ambao wanaajiriwa chini ya kanuni, taratibu, na sheria za ajira chni ya Sekta ya UMMA; Kwa mujibu wa vigezo hivyo, nje ya suala la Umri, yapo maeneo mengine muhimu kama manne kama ifuatayo:


  • Kwanza – Equal Opportunity Employment – bila ya kujali jinsia, kabila, dini, n.k;
  • Pili – ajira iendane na sifa walizonazo/ajira iwe based on MERIT of the individual;
  • Tatu – mchakato wa ajira uwe transparent/wa wazi;
  • Nne, mchakato utawaliwe na mazingira ya ushindani, na sio Upendelea;

Swali linalofuatia ni Je: Tanroads wanazingatia haya katika michakato yake ya ajira?
Nadhani masuala haya manne yakisimamiwa vizuri, tutaweza kupata suluhu kwa baadhi ya matatizo uliyoainisha;
 
Mkuu Mwita,
Wadau wengi wamesema mambo ya maana; tatizo kubwa la Tanroads inajiendesha sana kimtandao kwa manufaa ya wahusika fulani, suala la umri au jinsia si kigezo kwenye ajira; zipo kazi ambazo vijana wameonyesha uwezo mkubwa wa kuzimudu kiliko wazee na zipo ambazo wazee wazimudu kuliko vijana; hali kadhalika kwa wake kwa waume; ajira siku zote inazingatia elimu na uzoefu wa kazi husika; hili la umri limekwa maksudi tu kwa sababu kuna watu wao tayari wapo tayari kupewa hizo kazi; na nina uhakika hizo kazi zimeshatolewa kwa watu wao hilo tangazo ni kiini macho; hizi ajira zao zinavyolewa ndiyo sababu kubwa imeifanya Tanroads iwe mzigo mkubwa kwa serikali; kampuni haina ufanisi hata kidogo ni ulaji mtupu

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Mkuu Mwita Maranya
Kama mtakumbuka kuna viongozi waliotakiwa kuajiriwa kwa kufuata ushauri wa Pricewater coop, kiichoshangaza ni kuwa licha ya kulipwa milioni 80, kiongozi alipatikana nje ya utaratibu. Ilikuwa short cut from top to bottom.
Tatizo hili limekuwepo hata katika nafasi za uteuzi. Angalia safu ya wakuu wa Wilaya, wakurugenzi wa Halmashauri n.k.
Naweza kusema wazi aliyepalilia mbegu za hili jambo ni BWM.

Katika uandikaji wa modern CV/Resume umri hautakiwi kwasababu ya age discrimination.
Inaaminika kuwa nafasi za kazi zinazingatia mambo mengi kama elimu, ujuzi, uzooefu, hata usimamizi.

Nikiliangalia hilo tangazo la TANROAD, sijui HR alitumia vigezo gani kama Barubaru alivyosema.
Ninachokiona kama tatizo ni limitations za umri.
Sidhani kama mtu akiwa beyond 35, mfano 37,38,hawezi kufanya kazi kama bridge operator.

Kinachotia shaka zaidi ni umri wa 35-40, kwamba umri huo wa miaka 5 una umuhimu wa kipekee katika hiyo kazi.
Endapo walitaka kupata wazooefu basi wangeweza kusema, experience of not less than 10 Years.
Kwa graduate wa miaka 22-25 hilo lingemuondoa katika ushindani wakati huo huo likitoa fursa kwa wale wenye uzoefu haswa.

Kitendo cha kutumia umri tu kinaashiria kuwa kuna kundi lengwa, na sidhani kama kuna kigezo kingine.
Mfumo wetu wa ajira hauna uwazi na unajenga matabaka, ilianza taratibu na sasa inakuwa 'fashion'.

Waajiri wanatakiwa watoe ''equal opportunity'' kwa jamii.
Mchambuzi ametoa vigezo 1 hadi 4 ninavyokubaliana navyo kabisa.
 
Kigezo cha umri kweli ni kikwazo kwa vijana wengi.Wengi wa vijana wanaomaliza vyuo ni under 30.
Ila kwa suala la ubaguzi ni kila sehemug,kila sekta ni UBAGUZI TUU.
 
Back
Top Bottom