Ajira za TANROADS: Kuna Harufu ya Ubaguzi na Upendeleo

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Jul 1, 2008
10,564
7,973
Salam WanaJF,

Kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wadau wa sekta ya usafirishaji juu ya vitendo vya rushwa na ubabe vinavyofanywa na watendaji ama watumishi wa mizani zilizopo maeneo mbalimbali nchini kwa upande mmoja. Kwa upande wa pili kumekuwa na malalamiko toka kwa wafanyakazi wa mizani hizo hasa weighbridge operators na shift incharges kulalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na mameneja wa mizani hizo katika mikoa mbalimbali nchini.

Kutokana na hali hiyo nimelazimika kufanya kautafiti kadogo ili walau kujua ukweli wa tuhuma hizi. Kuna vitu vichache namalizia kabla sijaweka bayana findings zangu kuhusu malalamiko hayo. Muda si mrefu nitaweka hapa ripoti yangu hapa JF.

Nikirudi katika mada ya leo kama kichwa cha habari kinavyosomeka; hivi karibuni Mameneja wa Tanroads wa mikoa yenye mizani (weigh bridges) wamekuwa wakitoa matangazo ya ajira kwa nafasi za Shift Incharge na Weigh Bridge Operators. Matangazo ya hivi karibuni kabisa ya ajira hizo ni katika mikoa ya Mwanza, Pwani na Morogoro.

Mojawapo ya sifa za lazima kwa waombaji ni kama ifuatavyo:

1. Shift Incharge;
a) Awe na elimu ya shahada ya kwanza [bachelor] ama Stashahada ya juu [Advanced Diploma] katika fani yoyote toka taasisi ya elimu ya juu inayotambulika na
b) Awe na umri kati ya miaka 35 hadi 40

2. Weighbridge Operator;
a) Awe na elimu ya Fundi Mchundo[FTC] katika fani za Umeme [Electrical Eng.], Ujenzi [Civil Eng.] au Mitambo [Mechanical Eng.] na
b) Awe na umri usiozidi miaka 35.

Kimsingi sina tatizo kabisa na kigezo cha elimu, isipokuwa hapo kwenye umri. Nimekuwa nikijiuliza masawali kadhaa bila kupata majibu, nikaona ni vizuri niwashirikishe maGT hapa ili tusaidiane kulitazama suala hili kwa pamoja. Vijana wengi sasahivi wanahitimu shahada/ stashahada za juu wakiwa na umri kati ya miaka 22-25, na wapo vijana wengi sana wenye uwezo mkubwa wa kushika nafasi za majukumu makubwa hata kuliko hiyo nafasi ya shift incharge. Na kwa kuwa wenye umri wa miaka 35 hadi 40 ambao wana elimu ya kiwango cha shahada/stashada ya juu watakuwa ni watu wenye kazi zao mahali kwingineko, hivyo basi kunakuwa hakuna mantiki ya kuweka kigezo cha umri mkubwa kiasi hicho katika ajira kama hizi.

Kwa mtazamo wangu naona kama kuna ubaguzi kama si upendeleo wa dhahiri katika ajira hizi za Tanroads, sina uhakika kama watu wenye umri huo mkubwa kiasi hicho ndio pekee wanaweza kuhimili majukumu ya kazi ya shift incharge. Nadhani hapa kuna mazingira ya mameneja wa Tanroads mikoa ama wizara ya ujenzi ama Tanroads makao makuu kuajiri watu wao wanaowataka wao, na kwa kufanya hivyo wanakuwa wanakiuka katiba yetu ya JMT pamoja na kufanya upendeleo wa wazi kwa baadhi ya kundi fulani la watanzania kwa kuwabagua wengine.

Na kwakuwa kama taifa tunakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana, nilidhani Tanroads kama taasisi ya umma inawajibika kuisaidia serikali katika kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana badala ya kuweka vigezo ambavyo vinadhihirisha wazi kwamba wanataka kuendelea kufanya "recycling" ama kujuana.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa mawazo yenu na mitazamo yenu katika hili.

Copy kwa Asprin, Invisible, Ngongo, chama, Ritz, zomba, AshaDii, Dark City, Preta, WiseLady, Molemo, Nguruvi3, Mkandara, Mag3, Ben Saanane, fmpiganaji, Filipo, Crashwise, Mzee wa Rula, LiverpoolFC, Mungi, jogi, Rutashubanyuma, Nicholas, Daudi mchambuzi, Mtambuzi, Mchambuzi, nngu007, n00b na wengine.
 
Mwita maranya.

Naona siku hizi tumepotezana kabisa sana. Hatukutani kwenye mijadala.

Hakika mimi nafikiri kwa upande wa Incharge/ Supervosor wamezingatia Uzoefu zaidi. Kwani hiyo ni nafasi ya uongozi inahitaji mtu mwenye uzoefu wa muda mrefu si tu katika kazi bali pia hata kwenye sharia za kazi na mahusiano kazini.

Kwani kwa kukosa uzoefu ndio yatakuwa kama ya yule DC aliyesema digree ya kwenye Chupi ( ni kijana mdogo ambaye hajawahi kushika nafasi hata ya mkuu wa section/ supervisor lakin akapewa U DC. Hivyo hajui sharia za kazi na mahusiano kazini ikiwa pamoja na kujua mamlaka za nchi na sharia zake.

Uzoefu ni muhimu sana kwa post zote za Uongozi.

Nakushauri katika utafiti wako usisahau kuPitia human resource polices za nchi yenu especially SOS pasi na shaka watabainisha kila kitu humo.

mash'kuura.
 
Ahsante sana mkuu Mwita Maranya kwa uchambuzi wako,

Haya mambo mbona yalianza kitambo?

Kuna mahali ilitangazwa kazi na jamaa walikuwa na mtu tayari. Kwa hiyo, wao walikuwa anasema kwamba wanatimiza maandiko tu. Walichofanya ni kuandaa tangazo la kazi ambalo lilitumia vigezo vilivyotoka kwenye CV ya mlengwa....Kwa wale tuliokuwa karibu tuliishia kucheka tu kwani ulikuwa ni usanii tena wa kitoto.

Naomba uzidi kufuatilia ili uone kama hili tangazo litakuwa tofauti na hayo ya nyuma niliyoyataja!!
 
Last edited by a moderator:
Maranya,

Tukizungumza upande wa ajira ya mashirika mbali mbali iwe binafsi ama serkali sio tu TANROADS ambapo kuna harufu ya Ubaguzi na Upendeleo. Hili tatizo sasa hivi limekuwa mno kiasi kwamba ingekuwa ni legal hata ofisi zingefunguliwa za consultation za kushauri namna gani hasa ni njia bora ya kubagua na kupendelea. Inaweza onekana mzaha ila ndio ukweli…

Kama unakumbuka huko nyuma (hasa prior 2000) hili lilikuwa ni tatizo sugu nchini kwetu ikiwa ni moja ya kipengele kilichokuwa kikitazamwa kwa mfumo wa rushwa (Kulikuwa na Upendeleo hasa wa ndugu na jamaa katika nafasi mbali mbali ikiwa haijalishi mhusika ana vigezo ama lah!). Akaja Mkapa kwa kiasi Fulani akalipunguza sana, watu wengi walifukuzwa kazi, wengine waliambiwa waende wakajiendeleze ili kupisha wale ambao wana sifa hasa kuomba nafasi za kazi. Likawa briefly controlled na Serkali chini ya Mkapa wakati huo, ila sasa limerudi kwa kasi! Huna ndugu, jamaa ama pesa ya kukuweka katika nafasi Fulani then possibility ya wewe kupata kazi haraka ipo chini sana. Ingawa kuna wengine wanabahatika kwa njia ya ku apply hivo hivo anapata.

Nikija kwa hawa watu wa Tanroads, naona kama upande wa umri sio mbaya saana, sijui labda nalitazama tofauti. For instance hio ‘Weighbridge operator’ wamesema kuwa umri usiozidi 35, hivo ina maana wote walio chini ya mika 35 hata hao wa 22-25 (range ya 1[SUP]st[/SUP] degree undergraduates wengi); ina maana kwa anae qualifay na ana sifa hizo atapata hio nafasi. Hali katika ‘Shift Incharge’ wameweka limitation ya 35 – 40.. Hapa nakuunga mkono walau ingekuwa from 30. Na hii kazi inahitaji mtu alie na experience katika managemet ya field yoyote ambayo inahusisha delegation ambayo huja with age…

Kutoka nje ya mada kidogo… Naamini kuwa tatizo la ajira katika Tanzania yetu ya sasa halitaweza kutatuliwa kwa ajira, nadhani inatakiwa kwa nguvu zote zisukumwe katika kuhamasisha vijana wenyewe kujiajiri. Kuajiriwa kwa sasa imekua ni mtihani saana. Kwa njia ya kuajiri kwa mtazamo wangu serkali ingeweza kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijna wengi kama wangeongeza bidii za dhati katika ku formalize vya kutosha sector ya kilimo nchini.

Ninapo sema ku formalize nina maana kuwa sector hio ikuzwe hadi kusababishe kuwa na demand kubwa ya wachumi, wana sociologia, washauri, waalimu, wakandarasi, Waandisi n.k kwa wingi katika hio sector ya kilimo kama walivyofanya wenzetu Zimbabwe. Tuna ardhi kubwa, kuna uhitaji wa chakula mkubwa duniani na kundi la vijana ni kubwa sana nchini kuliko kundi lolote lile… A perfect combination.
 
Mkuu Mwita Maranya siku hizi mashirika ya umma karibu yote yanatumia mtindo huo wa hovyo kupitiliza.

Ukitia mguu AUWASA Mamlaka ya Maji jijini Arusha yuko afisa mwajiri mpare/mchagga yeye anahakikisha tatizo la ajira kijiji alichozaliwa na familia yake linamalizwa kama si kupunguzwa na uwepo wake AUWASSA.
 
Last edited by a moderator:
Kwa upande wangu sijui mantiki ya kuweka umri wa kati ya 35 hadi 40. Kwanini wasitumie kigezo cha uzoefu kazini hata kama wangesema mwenye uzoefu usiopungua miaka 10 kazini. Kwa hiyo wanataka mtu mwenye miaka 35 hata kama hana uzoefu wa mwaka hata mmoja maana yake nini? Kwamba mtu bora kwao ni yule wa kati 35 na 40 na sio chini ya hapo au zaidi ya hapo?
 
Salam WanaJF,

Kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wadau wa sekta ya usafirishaji juu ya vitendo vya rushwa na ubabe vinavyofanywa na watendaji ama watumishi wa mizani zilizopo maeneo mbalimbali nchini kwa upande mmoja. Kwa upande wa pili kumekuwa na malalamiko toka kwa wafanyakazi wa mizani hizo hasa weighbridge operators na shift incharges kulalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na mameneja wa mizani hizo katika mikoa mbalimbali nchini.

Kutokana na hali hiyo nimelazimika kufanya kautafiti kadogo ili walau kujua ukweli wa tuhuma hizi. Kuna vitu vichache namalizia kabla sijaweka bayana findings zangu kuhusu malalamiko hayo. Muda si mrefu nitaweka hapa ripoti yangu hapa JF.

Nikirudi katika mada ya leo kama kichwa cha habari kinavyosomeka; hivi karibuni Mameneja wa Tanroads wa mikoa yenye mizani (weigh bridges) wamekuwa wakitoa matangazo ya ajira kwa nafasi za Shift Incharge na Weigh Bridge Operators. Matangazo ya hivi karibuni kabisa ya ajira hizo ni katika mikoa ya Mwanza, Pwani na Morogoro.

Mojawapo ya sifa za lazima kwa waombaji ni kama ifuatavyo:

1. Shift Incharge;
a) Awe na elimu ya shahada ya kwanza [bachelor] ama Stashahada ya juu [Advanced Diploma] katika fani yoyote toka taasisi ya elimu ya juu inayotambulika na
b) Awe na umri kati ya miaka 35 hadi 40

2. Weighbridge Operator;
a) Awe na elimu ya Fundi Mchundo[FTC] katika fani za Umeme [Electrical Eng.], Ujenzi [Civil Eng.] au Mitambo [Mechanical Eng.] na
b) Awe na umri usiozidi miaka 35.

Kimsingi sina tatizo kabisa na kigezo cha elimu, isipokuwa hapo kwenye umri. Nimekuwa nikijiuliza masawali kadhaa bila kupata majibu, nikaona ni vizuri niwashirikishe maGT hapa ili tusaidiane kulitazama suala hili kwa pamoja. Vijana wengi sasahivi wanahitimu shahada/ stashahada za juu wakiwa na umri kati ya miaka 22-25, na wapo vijana wengi sana wenye uwezo mkubwa wa kushika nafasi za majukumu makubwa hata kuliko hiyo nafasi ya shift incharge. Na kwa kuwa wenye umri wa miaka 35 hadi 40 ambao wana elimu ya kiwango cha shahada/stashada ya juu watakuwa ni watu wenye kazi zao mahali kwingineko, hivyo basi kunakuwa hakuna mantiki ya kuweka kigezo cha umri mkubwa kiasi hicho katika ajira kama hizi.

Kwa mtazamo wangu naona kama kuna ubaguzi kama si upendeleo wa dhahiri katika ajira hizi za Tanroads, sina uhakika kama watu wenye umri huo mkubwa kiasi hicho ndio pekee wanaweza kuhimili majukumu ya kazi ya shift incharge. Nadhani hapa kuna mazingira ya mameneja wa Tanroads mikoa ama wizara ya ujenzi ama Tanroads makao makuu kuajiri watu wao wanaowataka wao, na kwa kufanya hivyo wanakuwa wanakiuka katiba yetu ya JMT pamoja na kufanya upendeleo wa wazi kwa baadhi ya kundi fulani la watanzania kwa kuwabagua wengine.

Na kwakuwa kama taifa tunakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana, nilidhani Tanroads kama taasisi ya umma inawajibika kuisaidia serikali katika kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana badala ya kuweka vigezo ambavyo vinadhihirisha wazi kwamba wanataka kuendelea kufanya "recycling" ama kujuana.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa mawazo yenu na mitazamo yenu katika hili.

Copy kwa Asprin, Invisible, Ngongo, chama, Ritz, zomba, AshaDii, Dark City, Preta, WiseLady, Molemo, Nguruvi3, Mkandara, Mag3, Ben Saanane, fmpiganaji, Filipo, Crashwise, Mzee wa Rula, LiverpoolFC, Mungi, jogi, Rutashubanyuma, Nicholas, Daudi mchambuzi, Mtambuzi, Mchambuzi, nngu007, n00b na wengine.
Hata hii habari uliotoa ina harufu ya ubaguzi mkubwa. Binafsi siwezi nikachangia kabisa kwa kuwa umewalenga rafiki zako unaowajua na umewakopi kwa kuonyesha msisitizo. Hali hii ni mbaya sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu. Napinga kwa sauti kuu huu ubaguzi ulioufanya. Kama umeufanya kwa makusudi basi mungu akuhukumu kwa dhambi ya ubaguzi, na kama ni bila kufahamu basi mungu akusamehe kwa kuwa hujui ulitendalo.
 
Hata hii habari uliotoa ina harufu ya ubaguzi mkubwa. Binafsi siwezi nikachangia kabisa kwa kuwa umewalenga rafiki zako unaowajua na umewakopi kwa kuonyesha msisitizo. Hali hii ni mbaya sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu. Napinga kwa sauti kuu huu ubaguzi ulioufanya. Kama umeufanya kwa makusudi basi mungu akuhukumu kwa dhambi ya ubaguzi, na kama ni bila kufahamu basi mungu akusamehe kwa kuwa hujui ulitendalo.

Copy 10 kwa kiroba,
ha haa ha...
 
Last edited by a moderator:
Maranya,

Tukizungumza upande wa ajira ya mashirika mbali mbali iwe binafsi ama serkali sio tu TANROADS ambapo kuna harufu ya Ubaguzi na Upendeleo. Hili tatizo sasa hivi limekuwa mno kiasi kwamba ingekuwa ni legal hata ofisi zingefunguliwa za consultation za kushauri namna gani hasa ni njia bora ya kubagua na kupendelea. Inaweza onekana mzaha ila ndio ukweli…

Kama unakumbuka huko nyuma (hasa prior 2000) hili lilikuwa ni tatizo sugu nchini kwetu ikiwa ni moja ya kipengele kilichokuwa kikitazamwa kwa mfumo wa rushwa (Kulikuwa na Upendeleo hasa wa ndugu na jamaa katika nafasi mbali mbali ikiwa haijalishi mhusika ana vigezo ama lah!). Akaja Mkapa kwa kiasi Fulani akalipunguza sana, watu wengi walifukuzwa kazi, wengine waliambiwa waende wakajiendeleze ili kupisha wale ambao wana sifa hasa kuomba nafasi za kazi. Likawa briefly controlled na Serkali chini ya Mkapa wakati huo, ila sasa limerudi kwa kasi! Huna ndugu, jamaa ama pesa ya kukuweka katika nafasi Fulani then possibility ya wewe kupata kazi haraka ipo chini sana. Ingawa kuna wengine wanabahatika kwa njia ya ku apply hivo hivo anapata.

Nikija kwa hawa watu wa Tanroads, naona kama upande wa umri sio mbaya saana, sijui labda nalitazama tofauti. For instance hio ‘Weighbridge operator’ wamesema kuwa umri usiozidi 35, hivo ina maana wote walio chini ya mika 35 hata hao wa 22-25 (range ya 1[SUP]st[/SUP] degree undergraduates wengi); ina maana kwa anae qualifay na ana sifa hizo atapata hio nafasi. Hali katika ‘Shift Incharge’ wameweka limitation ya 35 – 40.. Hapa nakuunga mkono walau ingekuwa from 30. Na hii kazi inahitaji mtu alie na experience katika managemet ya field yoyote ambayo inahusisha delegation ambayo huja with age…

Kutoka nje ya mada kidogo… Naamini kuwa tatizo la ajira katika Tanzania yetu ya sasa halitaweza kutatuliwa kwa ajira, nadhani inatakiwa kwa nguvu zote zisukumwe katika kuhamasisha vijana wenyewe kujiajiri. Kuajiriwa kwa sasa imekua ni mtihani saana. Kwa njia ya kuajiri kwa mtazamo wangu serkali ingeweza kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijna wengi kama wangeongeza bidii za dhati katika ku formalize vya kutosha sector ya kilimo nchini.

Ninapo sema ku formalize nina maana kuwa sector hio ikuzwe hadi kusababishe kuwa na demand kubwa ya wachumi, wana sociologia, washauri, waalimu, wakandarasi, Waandisi n.k kwa wingi katika hio sector ya kilimo kama walivyofanya wenzetu Zimbabwe. Tuna ardhi kubwa, kuna uhitaji wa chakula mkubwa duniani na kundi la vijana ni kubwa sana nchini kuliko kundi lolote lile… A perfect combination.


Kwa kweli umezungumza mambo mazito sana, na nitakuwa mchoyo wa fadhwila kama sijatia japo neno moja la kukupongeza.

Lakin SUALA KUBWA kwa sasa huko Tanzania ni KUBADILISHA MFUMO WENU WA ILMU. yaani mfumo tuliosomea sisi (wa Zamani) wa KUSOMESHWA KWA LENGO LA KUAJIRIWA ambapo sisi sote tulipokuwa tunamaliza form 4, form 6 au Chuo kikuu wote tulipata ajira Serikalini au kwenye mashirika tanzu ya umma.

Ila kwa sasa kutokana na Serikali yenu kushindwa kutoa ajira kwa vijana wake. Inabidi SERA ZA ILMU KUBADILIKA NA kujikita KUWAFUNDISHA VIJANA KUJIAJIRI kama wanavyofanya jirani zenu kenya na Uganda.

Ukiwa katika nchi hizo Vijana wanafundishwa somo la Ujasiriamali, Uchumi na Uzalendo tokea wakiwa primary school na ni lazima kwa kila mwanafunzi kusoma somo hilo ima uwe unachukua sayansi, Arts au Biashara.

Ni vizuri na Tanzania mbadilike ili muweze kwenda na wakati ikiwa pamoja na kuwaandaa vijana kupambana na maisha kwa njia ya kujiajiri.



Nakupa pongezi Ashadii kwa upembuzi na mchango wako katika uzi huu.
 
Maranya,

Tukizungumza upande wa ajira ya mashirika mbali mbali iwe binafsi ama serkali sio tu TANROADS ambapo kuna harufu ya Ubaguzi na Upendeleo. Hili tatizo sasa hivi limekuwa mno kiasi kwamba ingekuwa ni legal hata ofisi zingefunguliwa za consultation za kushauri namna gani hasa ni njia bora ya kubagua na kupendelea. Inaweza onekana mzaha ila ndio ukweli…

Kama unakumbuka huko nyuma (hasa prior 2000) hili lilikuwa ni tatizo sugu nchini kwetu ikiwa ni moja ya kipengele kilichokuwa kikitazamwa kwa mfumo wa rushwa (Kulikuwa na Upendeleo hasa wa ndugu na jamaa katika nafasi mbali mbali ikiwa haijalishi mhusika ana vigezo ama lah!). Akaja Mkapa kwa kiasi Fulani akalipunguza sana, watu wengi walifukuzwa kazi, wengine waliambiwa waende wakajiendeleze ili kupisha wale ambao wana sifa hasa kuomba nafasi za kazi. Likawa briefly controlled na Serkali chini ya Mkapa wakati huo, ila sasa limerudi kwa kasi! Huna ndugu, jamaa ama pesa ya kukuweka katika nafasi Fulani then possibility ya wewe kupata kazi haraka ipo chini sana. Ingawa kuna wengine wanabahatika kwa njia ya ku apply hivo hivo anapata.

Nikija kwa hawa watu wa Tanroads, naona kama upande wa umri sio mbaya saana, sijui labda nalitazama tofauti. For instance hio ‘Weighbridge operator' wamesema kuwa umri usiozidi 35, hivo ina maana wote walio chini ya mika 35 hata hao wa 22-25 (range ya 1[SUP]st[/SUP] degree undergraduates wengi); ina maana kwa anae qualifay na ana sifa hizo atapata hio nafasi. Hali katika ‘Shift Incharge' wameweka limitation ya 35 – 40.. Hapa nakuunga mkono walau ingekuwa from 30. Na hii kazi inahitaji mtu alie na experience katika managemet ya field yoyote ambayo inahusisha delegation ambayo huja with age…

Kutoka nje ya mada kidogo… Naamini kuwa tatizo la ajira katika Tanzania yetu ya sasa halitaweza kutatuliwa kwa ajira, nadhani inatakiwa kwa nguvu zote zisukumwe katika kuhamasisha vijana wenyewe kujiajiri. Kuajiriwa kwa sasa imekua ni mtihani saana. Kwa njia ya kuajiri kwa mtazamo wangu serkali ingeweza kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijna wengi kama wangeongeza bidii za dhati katika ku formalize vya kutosha sector ya kilimo nchini.

Ninapo sema ku formalize nina maana kuwa sector hio ikuzwe hadi kusababishe kuwa na demand kubwa ya wachumi, wana sociologia, washauri, waalimu, wakandarasi, Waandisi n.k kwa wingi katika hio sector ya kilimo kama walivyofanya wenzetu Zimbabwe. Tuna ardhi kubwa, kuna uhitaji wa chakula mkubwa duniani na kundi la vijana ni kubwa sana nchini kuliko kundi lolote lile… A perfect combination.

Dah,una nigusa sana.
Wengi tuna tamani kujiajiri sana,lakini sio kwamba tumekuwa wavivu la hasha.

By the way AshaDii natafuta kazi pia,nipe mchongo basi.
Huu wa Tanroads mh,hamna changu hapo.
 
Last edited by a moderator:
Mwita maranya.

Naona siku hizi tumepotezana kabisa sana. Hatukutani kwenye mijadala.

Hakika mimi nafikiri kwa upande wa Incharge/ Supervosor wamezingatia Uzoefu zaidi. Kwani hiyo ni nafasi ya uongozi inahitaji mtu mwenye uzoefu wa muda mrefu si tu katika kazi bali pia hata kwenye sharia za kazi na mahusiano kazini.

Kwani kwa kukosa uzoefu ndio yatakuwa kama ya yule DC aliyesema digree ya kwenye Chupi ( ni kijana mdogo ambaye hajawahi kushika nafasi hata ya mkuu wa section/ supervisor lakin akapewa U DC. Hivyo hajui sharia za kazi na mahusiano kazini ikiwa pamoja na kujua mamlaka za nchi na sharia zake.

Uzoefu ni muhimu sana kwa post zote za Uongozi.

Nakushauri katika utafiti wako usisahau kuPitia human resource polices za nchi yenu especially SOS pasi na shaka watabainisha kila kitu humo.

mash'kuura.

Ndugu yangu Barubaru bado tuko pamoja hapa JF basi tu inatokea kwamba hatukutani mara kwa mara kama zamani, nahisi umebadilisha muda wa kuvisit JF.

Hata hivyo ninakubaliana kwa sehemu kubwa na maelezo yako kwakuwa una uzoefu wa kutosha na ajira za serikali yetu ya JMT.

Ni kweli kwamba shift incharge/supervisor wamezingatia kupata watu wenye uzoefu, lakini kama ungekuwa unafahamu structure ya weigh bridge ungegundua kwamba hakuna ulazima wa kuweka kigezo cha umri mkubwa sana kiasi hicho. Kwa uzoefu wangu na hawa watu wa mizani mara nyingi maoperator ambao wamefanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja hadi miaka miwili ndio wamekuwa wakiwapromote kuwa shift incharges na wanaperform vizuri sana.

Kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba mizani nyingi zinakuwa na shift mbili kwa siku, except mzani wa kibaha ambao una shift tatu kwa siku. Kila shift inakuwa na incharge wake(shift incharge) lakini papo hapo kunakuwa na overall incharge na juu yake kuna weighbridge supervisor, kwahiyo hawa mashift incharge wanafanya kazi kwa karibu sana na maoverall incharge na weighbridge supervisor.

Kwa utafiti nilioufanya katika baadhi ya mizani, wengi wa hawa mashift incharge na overall incharge ni watu wenye elimu za FTC, Ordinary Diploma na wachache wenye shahada. Na hata ma weigh bridge supervisors wako mchanganyiko, wenye FTC na Shahada/stashahada.

Angalizo lako nitalifanyia kazi, si vibaya kama unaifahamu hiyo human resource policy hasa hiyo SOS ili kunisaidia kukamilisha kazi yangu.
 
Last edited by a moderator:
Ahsante sana mkuu Mwita Maranya kwa uchambuzi wako,

Haya mambo mbona yalianza kitambo?

Kuna mahali ilitangazwa kazi na jamaa walikuwa na mtu tayari. Kwa hiyo, wao walikuwa anasema kwamba wanatimiza maandiko tu. Walichofanya ni kuandaa tangazo la kazi ambalo lilitumia vigezo vilivyotoka kwenye CV ya mlengwa....Kwa wale tuliokuwa karibu tuliishia kucheka tu kwani ulikuwa ni usanii tena wa kitoto.

Naomba uzidi kufuatilia ili uone kama hili tangazo litakuwa tofauti na hayo ya nyuma niliyoyataja!!

Ni kweli mkuu haya mambo yalikuwepo sana miaka ya nyuma hadi miaka ya 90 huku ndipo yalianza kuonekana kupungua sana. Sikutarajia kwamba hali hii inarudi kwa kasi ya ajabu kiasi hiki.

Na kweli hili la kutangaza nafasi ya kazi wakati mtu keshaajiriwa lipo sana. Wanafanya hivi kama formality tu ili kuwazuga watanzania kumbe wanakuwa wameshaajiri mtu wao.

Hii tabia inakera sana na inabidi kwa pamoja tuikemee ili kila mtanzania mwenye sifa na uwezo aweze kuajirika katika serikali yake ama katika mashirika yetu ya umma. Imefika mahali watu wanajua kwamba taasisi fulani ama wizara fulani ni kwa ajili ya watu fulani ama kabila fulani, hii ni hatari sana kwa ustawi wa nchi yetu.
 
Mkuu mimi nadhani ingekuwa vizuri tukafahamu umri wa mtu aliyetangaza hizo nafasi, na je ni akili yake mwenyewe, ama kwa maelekezo.
Halafu tambua kwamba hizo nafasi mpaka itangazwe tayari imeshapata watu wa kuziba, isipokuwa wanafanya hivyo kuondoa lawama!
 
Hata hii habari uliotoa ina harufu ya ubaguzi mkubwa. Binafsi siwezi nikachangia kabisa kwa kuwa umewalenga rafiki zako unaowajua na umewakopi kwa kuonyesha msisitizo. Hali hii ni mbaya sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu. Napinga kwa sauti kuu huu ubaguzi ulioufanya. Kama umeufanya kwa makusudi basi mungu akuhukumu kwa dhambi ya ubaguzi, na kama ni bila kufahamu basi mungu akusamehe kwa kuwa hujui ulitendalo.

We nawe, ndo mana jina lako ni kiroba..LOL
Keshasema na wengine, sasa ulitaka ataje wana JF wote....!

Na kiroba anaalikwa kuchangia mada hii.... haya changia sasa maana nimekutaja kwa jina lako
 
Last edited by a moderator:
Kwa upande wangu sijui mantiki ya kuweka umri wa kati ya 35 hadi 40. Kwanini wasitumie kigezo cha uzoefu kazini hata kama wangesema mwenye uzoefu usiopungua miaka 10 kazini. Kwa hiyo wanataka mtu mwenye miaka 35 hata kama hana uzoefu wa mwaka hata mmoja maana yake nini? Kwamba mtu bora kwao ni yule wa kati 35 na 40 na sio chini ya hapo au zaidi ya hapo?

SG8,

Kama unavyoelewa sasa hivi kuna uchakachuzi mkubwa sana, CV za watu ni fake (kuna mtu ana CV ipo very impressive ila ukweli pekee wa hio CV ni Jina lake na elimu ya Secondary). Kupunguza zoezi la form zitakazo pokelewa moja ya strategy huwa wanaweka range ya umri ambayo wanaamini kuwa mtu wa umri huwa kweli anayo experience (hasa kwa nafasi za kazi ambazo experience ni muhimu).

Walau huo ndio mtazamo wangu.
 
Hata hii habari uliotoa ina harufu ya ubaguzi mkubwa. Binafsi siwezi nikachangia kabisa kwa kuwa umewalenga rafiki zako unaowajua na umewakopi kwa kuonyesha msisitizo. Hali hii ni mbaya sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu. Napinga kwa sauti kuu huu ubaguzi ulioufanya. Kama umeufanya kwa makusudi basi mungu akuhukumu kwa dhambi ya ubaguzi, na kama ni bila kufahamu basi mungu akusamehe kwa kuwa hujui ulitendalo.


Kiroba kwanza nisamehe kukujibu kwa niaba, nimeona vigumu kupita bila kulizungumzia pia... kama una mchango ambao unaona kabisa tutafaidika tafadhali tunaomba... Naamini kuwa Maranya kafanya hivi kama njia ya kutushtua kuwa kuna topic kaweka hapa na angependa michango yetu (kama tunayo ama kama nafasi inaruhusu); Jamvi hili kubwa sana, huwezi ona topic zote, hio ni moja ya technique ya kujulisha topic umerusha na wahitaji mawazo ya wadau...
 
Ninakubaliana na maelezo yake mia kwa mia AshaDii.

Labda nichangie kidogo juu ya hii observation yako.

Kutoka nje ya mada kidogo… Naamini kuwa tatizo la ajira katika Tanzania yetu ya sasa halitaweza kutatuliwa kwa ajira, nadhani inatakiwa kwa nguvu zote zisukumwe katika kuhamasisha vijana wenyewe kujiajiri. Kuajiriwa kwa sasa imekua ni mtihani saana. Kwa njia ya kuajiri kwa mtazamo wangu serkali ingeweza kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijna wengi kama wangeongeza bidii za dhati katika ku formalize vya kutosha sector ya kilimo nchini.

Ninapo sema ku formalize nina maana kuwa sector hio ikuzwe hadi kusababishe kuwa na demand kubwa ya wachumi, wana sociologia, washauri, waalimu, wakandarasi, Waandisi n.k kwa wingi katika hio sector ya kilimo kama walivyofanya wenzetu Zimbabwe. Tuna ardhi kubwa, kuna uhitaji wa chakula mkubwa duniani na kundi la vijana ni kubwa sana nchini kuliko kundi lolote lile… A perfect combination

Vijana wengi bado hawana elimu ya kujiajiri na serikali bado haijaweka mazingira bora kwa vijana kujiajiri. Mitaala ya elimu yetu inatujenga kutegemea ajira za kuajiriwa zaidi kuliko kujiajiri.Na hata huko kwenye kilimo bado serikali haijawekeza vya kutosha ili kuyafanya mazingira ya kilimo yawe rafiki kwa vijana na kuwavutia ili wengine waelekeze nguvu zao huko. Hapa ninaizungumzia serikali kwakuwa ndiyo inawajibika kuwaandaa wananchi wake kielimu na baadae kuwawekea mazingira bora ya kujiajiri na kuajiriwa.

Fikiria ardhi kubwa tuliyonayo nchini, tena yenye rutuba lakini serikali imeshindwa kuwekeza vya kutosha katika kuweka miundombinu muhimu kwa kilimo kama irrigation schemes, nani atapoteza muda wake kujikita katika kilimo cha kutegemea kudra za mwenyezi Mungu atuletee mvua? wakati tuna mabonde mengi ambayo tungeweza kuweka miundombinu tu na vijana wenyewe wakakimbilia huko. Jambo la pili katika kilimo ni masoko, sasahivi kila mmoja ni shahidi namna wakulima wetu wa mikoa ya kusini wanavyopata shida ya kupata masoko, wanazalisha kwa shida sana bila msaada wa serikali lakini ikifika wakati wa kuuza wanazuiwa wasipeleke mazao yao nje ya nchi ambako kuna bei nzuri na kulazimishwa waiuzie serikali au wafanyabiashara wajanja wajanja wa hapa mjini ambao mwisho wa siku mazao hayo hayo waliyonunua kwa wakulima wa ndani ambao serikali imewazuia kuypeleka nje, wafanyabiashara wao wanaruhusiwa kuyapeleka kokote wanakoona kuna bei nzuri, sasa katika hali kama hiyo ni kijana gani mwenye shahada yake atapoteza muda kujikita katika kilimo?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mimi nadhani ingekuwa vizuri tukafahamu umri wa mtu aliyetangaza hizo nafasi, na je ni akili yake mwenyewe, ama kwa maelekezo.
Halafu tambua kwamba hizo nafasi mpaka itangazwe tayari imeshapata watu wa kuziba, isipokuwa wanafanya hivyo kuondoa lawama!

Ndugu yangu Mungi meneja wa Tanroads mkoa wa Pwani ni engineer Sarakikya, kama nakumbuka vizuri huyu mtu alipata kuwa meneja tanroads Arusha ama Kilimanjaro kabla ya kuhamishiwa Pwani, sina uhakika na umri wake labda kama kuna mtu anamfahamu kwa undani anaweza kutusaidia. Lakini pia nimeona matangazo ya namna hii kwa mikoa ya Mwanza na Morogoro, hapa ndipo napata feeling kwamba huenda haya ni maelekezo ya Tanroads makao makuu ama wizara ya ujenzi.
 
Last edited by a moderator:
Hata hii habari uliotoa ina harufu ya ubaguzi mkubwa. Binafsi siwezi nikachangia kabisa kwa kuwa umewalenga rafiki zako unaowajua na umewakopi kwa kuonyesha msisitizo. Hali hii ni mbaya sana kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu. Napinga kwa sauti kuu huu ubaguzi ulioufanya. Kama umeufanya kwa makusudi basi mungu akuhukumu kwa dhambi ya ubaguzi, na kama ni bila kufahamu basi mungu akusamehe kwa kuwa hujui ulitendalo.

mdau umetoa la MOYONI,NA LIMETOKA,NAMI TABIA HII SIIPENDI
 
Back
Top Bottom