kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,222
- 1,670
Naibu waziri wa Kazi na Ajira mh Milton Makongoro Mahanga' amesema leo katika kipindi cha TUONGEE, kuwa watu wenyekipato ndiyo wanafanya tatizo la watoto wa mitaani kuwa sugu, kwa kuwapa vijisenti ombaomba mitaani, na kuwavutia wale walioko mikoani kuja mijini kuongeza idadi ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi. Amesema ni bora watu wanaojiona wana pesa za kuwapa ombaomba WAENDE MAKANISANI NA MISKITINI wakatoe sadaka na zaka, kwani taasisi za dini zina utaratibu mzuri wa kuwasaidia wenyeshida ili kupunguza tatizo kuwa kubwa katika jamii yetu. Amesema wazazi wenye watoto ombaomba wanabweteka wakisubiri watoto wao walete walivyopata kwa njia ya kuomba. Na akazidi kukemea wale weendesha magari kwamba waache kuwapa hizo shilingi mia, kwa tabia hii inafanya serikali ishindwe kuhimili wingi wao, kwavile wanatoka makwao wanajua kuwa wakifika mjini watapa fedha. Pia aliulizwa kwa nini nchi ya Kenya wameweza kufanikisha tatizo la kuondoa watoto wa mitaa? Akajibu kama watanzania wataacha kutoa hizi shilingi mia zao, basi tatizo linaweza kupungua au kuisha kabisa. Amesama kuwa watu wasio kuwa na elimu ndiyo wanao zaa sana, na kushindwa kuwatunza watoto. Amesema serikali ya tanzania haijafikia hatua ya kuwapangia idadi ya watoto wa kuzaliwa katika familia' kama nchi kama China inavyofanya. KWAHIYO WANA JF PUNGUZENI IDADI YA KUZAA WATOTO, MWISHO WAWILI TU.