Ajira mpya hakuna, halafu hela mnakula wenyewe, Good God will pay you

Wanaukumbi.

Serikali tuliiamini na tukavumilia mateso ya mtaani tukijipa matumaini makubwa kuwa mnaijenga nchi baadae mambo yatakuwa mazuri, kumbe fedha zinatumiwa hovyo, mlikuwa na uwezo wa kuajiri kila mwaka na kuongeza mishahara ila mliamua kubana ili hizo hela za umma na kufanya ufisadi kama ripoti ya CAG, inavyosema.

CAG anaonesha namna mabeberu wetu walivyokuwa wanaitafuna hii nchi, huku wamejificha kwenye kimvuli cha uzalendo.

Ripoti hii ya CAG imetuonyesha kuwa:
  • Tunahitaji taasisi imara na siyo fikra za mtu mmoja anayejidai imara
  • Tunahitaji wanasiasa visionary wanaojali maslahi ya muda mrefu ya Watanzania na vyama imara vya siasa.
Barikiwa sana mkuu, kuna watu kila wakati wamekuwa wakiongelea ujenzi wa Taasisi imara badala ya kuwa na watu imara ambao ni probable dead bodies. Lakini watu wa chama kile wanaodhani wanajua kila kitu isipokuwa kufufua wafu wamekuwa wakikashifu fikra kama hizi zako kwa kusema unaweza kuwa na taasisi imara aliye juu akawa wa ovyo mipango yote ikakwama. Tunawambia itakwama vipi na wakati taasisi za kumsukuma zina nguvu?
 
Usije yaamini maccm hata siku moja,mwendazake alikuwa anajigamba kudhibiti rushwa kumbe wanalinda ufisadi wa wenye vyeo

Bora hata hizo ajira 6000 za walimu alizosema mama zijazwe na zile za dangote 4000 zitafika 10,000 wanyonge wapatepo kiduchu ila hao jamaa wanatia hasira sana
 
Jamaa alikuwa na Mambo ya hovyo hovyo..ubabe wa kijima..Kama mfuasi wake sabaya..ujuha uongozi wa kishamba..mauwaji..na kuficha wizi kwa kutumia maneno ya uzalendo na mabeberu..
Lakini sisi wa chato tunamjua vizuri kwamba jamaa anapenda Sana kujilimbikizia Mali toka zamani..
Akiwa waziri alikuwa analazimisha wafanyakazi wa wilayani wapange kwenye nyumba zake..Tena nyumba nyingi ambazo ilisemekana zilipatikana kifisadi..
Pia alipindisha ujenzi wa lami uliokuwa uanzie mwanza..ukaanzia porini ili lami ipite kwao chato..kikwete akamsaidia akampa pesa lami nyingine ianzie mwanza kupitia Geita..jamaa alikuwa mtu mbaya Sana
Akiwa mbunge na waziri alikuwa hataki mpinzani hata ndani ya ccm ..wapinzani wote aliwafanyia hujuma..wengine alwahonga wajitoe kwenye kura za maoni..wengi aliwatisha..wengie aliwaroga..
Ndio maana Kila mara alipita bila kupingwa..udikteta toka akiwa mbunge
 
Dah Hii nchi yetu viongoz ni wabinafs sana wanatuzuga kwa matamko wao wanaenjoy kugawana tu mapesa Vijana hawaajiriw waloajiriw hawapandishw mishahara huku wao wenyew wakijigawia mapesa
This is not fair
 
Back
Top Bottom