Ajira kwa ujumla wake zitatoka lini

Kifurukutu

JF-Expert Member
Aug 29, 2013
4,502
6,403
Ni takribani miaka miwili sasa tangu ajira kutoka kada zote kusitishwa huku mtaani wasomi wakiongezeka wasijue nini cha kufanya maana wengi kimbilio lao ni ajira za serkali

Ni muda sasa ukimya umetamalaki yaani asitokee ata mtu kuhoji ni lini ajira zitatoka rasmi

Mpaka sasa makontena ya wasomi ni yapo mawili huku mtaani wasijue nini kinaendelea, na hivi mda mfupi ujao kontena la tatu linakaribia!
Wasomi wote hawa wataenda wapi pasi na ajira na kazi za uhakika?

Ni muda muafaka sasa watawala wetu waweke siasa pembeni, watukumbuke walimu wa sanaa, na kada zingine zote na ajira zitoke kama ilivyokuwa enzi za Jk!
 
Tusiwahi kuhukumu kila jambo ni siasa mda mwingine tuwe wavumilivu, watanzania hatujawah kupitia hali kama hii ndio maana wengi wanashangaa but mkulu yupo sahihi na kama ipo sehm anamakosa basi tujue yy pia ni bin adam kama sie tulionyuma yake
 
soon wasomi tutaanza kuihama nchi kutafuta green pasture hatutaki siasa kwenye elimu na maisha yetu.
 
Pesa za mafisadi zote tumechukua, wanaolia njaa no waliozoea ujanjaujanja, pesa za wakwepa kodi zote sasa zipo. Tanzania ya viwanda ajira za nini wenzenu tunasubiri neema tu ya magawio, watu wenyewe 45 million. Za fisadi mmoja tu zinatosha kila mwezi seuze za kodi na viwanda!
 
Back
Top Bottom