Ajira 5000 za Hayati Magufuli zimepotea, ajira 6,000 za Rais Samia hazieleweki. Sasa hivi tunazungumzia ajira 12,000 bajeti ijayo

Komando tamimy

Senior Member
Nov 18, 2020
108
121
Kulikuwana ajira 5000 ambazo tulizoaahidiwa na Hayati Magufuli aliyekuwa Rais wetu mpendwa muda ukayoyoma na zikapotea bila majibu ya kueleweka mara wamesharipoti in PM voice bungeni nayo ikapita.

Kipenzi chetu Mungu akamchukua kazi ya Mungu haina makosa (RIP Rais Magufuli)

Tukaja mama yetu muongoza dira akasema anataka walimu 6,000 waajiriwe haraka as replacement kwa waliostaafu na waliokufa, hamna kilichofanyika sijui tatizo nini sijui hawaelewi maagizo ya mkuu wao.

Wenye dhamana wamebaki wanazurura hawaelewi nini wafanye.

Wizara ya TAMISEMI imekuwa kubwa, nashauri ingegawanywa hata zikawa 2 vinginevyo Waziri anafanya mark time.

Tena zimekuja nyingine ajira 12000 za bajeti mbona hatuelewi sasa tushike lipi tuache lipi!? Au ndio kuwaaambia waalimu wanywe maji kwanza sukari ipo chini?

Jana tena amesikika waziri akisema ajira 10000 za waalimu hivi karibuni. serikali zetu za kiafrika kwanini hazina muunganiko?! Kila waziri anaongea anavyojisikia?

Serikali ikijikite katika kutekeleza ahadi zake kwa vijana wengi wamebaki njiapanda.
 
Labda wanaripoti kimya kimya.

Si unajua Tayari walishaomba kwa hio sasa ni kuchakata na kupeleka watu vituoni.

Ngoja mwaka huu wamalize wengine ndio labda kutakuwa na dirisha lingine la maombi.
 
Kuna yule jamaa anayejulikana kwa cheo cha PM, ndani ya mwezi mmoja tu! Tena pasipo hata na chembe ya aibu, aliwadanganya watu wazima wenzake mara mbili!

Alitudanganya kuhusu ajira hewa elfu 5! Na pia kuhusu afya ya yule mpita njia. Uongo uongo uongo! Wanasiasa ni viumbe waongo, vigeugeu na wanafiki sana. Siyo wa kuwaamini kwa 100%.
 
Kuna yule jamaa anayejulikana kwa cheo cha PM, ndani ya mwezi mmoja tu! Tena pasipo hata na chembe ya aibu, aliwadanganya watu wazima wenzake mara mbili!

Alitudanganya kuhusu ajira hewa elfu 5! Na pia kuhusu afya ya yule mpita njia. Uongo uongo uongo! Wanasiasa ni viumbe waongo, vigeugeu na wanafiki sana. Siyo wa kuwaamini kwa 100%.
Utendaji kazi wa sasa ni wa slow slow sana compared na kipindi kile Hayati JPM alipotoa maagizo ya ajira tarehe 04/09/2020 na iliwachukua siku 3 tu na wakaruhusu watu waapply lkn Mh.Rais SSM aliwaagiza tarehe 06/04 wafanye haraka ajira za replacement lakini mpaka leo hawaeleweki kama watachukua majina ya kwenye database au wataruhusu application upya.Wao kila siku kwenye vyombo vya habari.
 
wanasiasa wameshagundua nchi hii raia wake wako na matatizo ya ubongo, kwa hiyo wanaweza kudanganya lolote na watu wakasifia. Leo madudu ya CAG hayana kiki tena watu wameshahamishwa kwenye reli. ELIMU ELIMU ELIMU.
umeongea kweli, watanzania ni watu wakusahau, habari za report YA CAG ishasahaulika haraka sana
 
Utendaji kazi wa sasa ni wa slow slow sana compared na kipindi kile Hayati JPM alipotoa maagizo ya ajira tarehe 04/09/2020 na iliwachukua siku 3 tu na wakaruhusu watu waapply lkn Mh.Rais SSM aliwaagiza tarehe 06/04 wafanye haraka ajira za replacement lakini mpaka leo hawaeleweki kama watachukua majina ya kwenye database au wataruhusu application upya.Wao kila siku kwenye vyombo vya habari.
Mchakato mbona umeshaanza kimya kimya na kwa umakini mkubwa! Wewe subiri tu usikie watakao fanikiwa kupata check number.
 
Utendaji kazi wa sasa ni wa slow slow sana compared na kipindi kile Hayati JPM alipotoa maagizo ya ajira tarehe 04/09/2020 na iliwachukua siku 3 tu na wakaruhusu watu waapply lkn Mh.Rais SSM aliwaagiza tarehe 06/04 wafanye haraka ajira za replacement lakini mpaka leo hawaeleweki kama watachukua majina ya kwenye database au wataruhusu application upya.Wao kila siku kwenye vyombo vya habari.
Wanaajiri walimu wanaojitolea.
 
Wanaojitolewa watapata cheq no kimya kimya hahaha hizi ajira bana,
Mtu anaandikwa amejitolea hata chaki hajawahi kuishika.
Hao mamluki hawakosekani. Ila kama vigezo vitafuatwa, litakuwa ni jambo jena sana kuwapa kipaumbele hawa wazalendo waliojitolea kwa muda sasa huko mashuleni, halafu nafasi zinazobaki ndipo mgombanie nyinyi ambao mlikuwa kitaa mkipambana na ishu nyingine!

Ingawa sikatai, wote mnastahili kuajiriwa. Maana na uhitaji nao ni mkubwa. Sema tu Serikali yenyewe nayo haina hela za kuwaajiri wahitimu wote kwa mpigo, baada ya kufanya uzembe alipoingia Hayati.
 
Tena nmegundua hata huyu mama ni mwanasiasa kwel kwel,eti anasema yote alyoyasema atayatekeleza,hapo ndo nkagundua kuwa hakuna lolote
 
Hao mamluki hawakosekani. Ila kama vigezo vitafuatwa, litakuwa ni jambo jena sana kuwapa kipaumbele hawa wazalendo waliojitolea kwa muda sasa huko mashuleni, halafu nafasi zinazobaki ndipo mgombanie nyinyi ambao mlikuwa kitaa mkipambana na ishu nyingine!

Ingawa sikatai, wote mnastahili kuajiriwa. Maana na uhitaji nao ni mkubwa. Sema tu Serikali yenyewe nayo haina hela za kuwaajiri wahitimu wote kwa mpigo, baada ya kufanya uzembe alipoingia Hayati.
Aisee mkuu niombe radhi.
 
Na mtoa uzi hii you MUST show RESPECT,sio mama Samia ni President Samia,na wewe sio msemaji wa watanzania wote ...eti kipenzi chetu JMP ...no no mimi hakuwa kipenzi changu please usinisemee nitaongea mwenyewe.
 
Na mtoa uzi hii you MUST show RESPECT,sio mama Samia ni President Samia,na wewe sio msemaji wa watanzania wote ...eti kipenzi chetu JMP ...no no mimi hakuwa kipenzi changu please usinisemee nitaongea mwenyewe.
Anzisha uzi wako kaka
 
wanasiasa wameshagundua nchi hii raia wake wako na matatizo ya ubongo, kwa hiyo wanaweza kudanganya lolote na watu wakasifia. Leo madudu ya CAG hayana kiki tena watu wameshahamishwa kwenye reli. ELIMU ELIMU ELIMU.
Shida na matatizo yamekuwa sehemu ya maisha yetu. Watajadili mambo ya kutumbuana tu huku kila mtu akipambana kutafuta pesa ya mboga.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom