Ajinyonga kwa kutotajwa na Padri kwenye misa ya Shukrani

Mkazi Mmoja wa Mkoani Iringa ameamua Kujiwahisha Kaburini kwa 'Kujiua' baada ya Kukasirishwa na Kitendo cha Padre wa Kanisa Katoliki kuamua 'Kumfagilia' tu Mkewe na 'Kumtenga' Yeye ( Mume ) pale walipoenda katika Misa ya Shukran hapo Kanisani baada ya Kumuuguza Mtoto wao kwa muda mrefu na hatimaye Kuponyeshwa na Mwenyezi Mungu.

Chanzo: Nipashe ya Radio One leo.

Sasa huyu Mhehe 'aliyejiua' kwa Kipopoma ( Kipumbavu ) hivi kama kumbe alitaka na anapenda 'Kufagiliwa' si angenitafuta tu GENTAMYCINE ili anipe Jina lake na nimtumie Mwanamuziki JB Mpiana na Bendi yake ya Wenge BCBG ili Wamtaje ( Wamfagilie ) sana katika Album yao iliyoko Jikoni sasa tayari Kupakuliwa kwa Wapenda Muziki?

Ila na Wewe Padre lazima Polisi Kwanza ikuhoji kwani haiingii Akili huyo Mtoto ana Wazazi wake Wawili halafu Wewe ukaamua 'Kumfagilia' tu Mkewe Marehemu na Yeye ( Marehemu Mume ) ukamuacha. Hivi hapa akina GENTAMYCINE tukihisi kuwa huenda kulikuwa na lililojificha kati yako na Mkewe tutakuwa tunakosea?
 
Inaelekea nyumbani kuna mengi yalikua yanaendelea yaliyosababisha baba kukosa kujiamini. Communication is a key to any active relationship.
Yumkini walisigana kuhusu shukurani, akina mama ndio wako active sana mambo ya kidini. Sasa kama baba aliweka kamgomo kwa hisia anazozijua yeye-kea ahadi ya kuja kufanya uchunguzi wa kina kujiridhisha ni shukurani kavu au kuna jingine nyuma ya pazia! kisha 'padre' naye akapitiwa na hilo lililoitwa kosa, tayari mashaka yakageuka ukweli.

Mwisho wa insha
 
Sasa hapo walio mtibu huyo mtoto ambao ni madokta na manesi hawapewa shukrani. Unajinyonga kwenye sabsbu isiyo halisia.
 
RFA mmepotosha,. Moravian hawana padri alafu kuhusu kujinyonga Kwa Huyo jamaa (Kwa asilimia kubwa alikuwa anaandamwa na pepo la kifo.apumzike Kwa amani

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli kanisa la moravian halina mapadri bali lina wachungaji, lakini vyombo vya habari vimemnukuu RPC wa Mkoa wa Njombe, yeye ndiye aliyetamka kuwa Padri wa kanisa la Moravian. Ukisikiliza vipande vya sauti unamsikia RPC akitamka Padri wa kanisa la Moravian. Kosa la waandishi ilikuwa ni kutomhoji RPC kama Moravian siku hizi wana mapadri!!
 
Mkazi Mmoja wa Mkoani Iringa ameamua Kujiwahisha Kaburini kwa 'Kujiua' baada ya Kukasirishwa na Kitendo cha Padre wa Kanisa Katoliki kuamua 'Kumfagilia' tu Mkewe na 'Kumtenga' Yeye ( Mume ) pale walipoenda katika Misa ya Shukran hapo Kanisani baada ya Kumuuguza Mtoto wao kwa muda mrefu na hatimaye Kuponyeshwa na Mwenyezi Mungu.

Chanzo: Nipashe ya Radio One leo.

Sasa huyu Mhehe 'aliyejiua' kwa Kipopoma ( Kipumbavu ) hivi kama kumbe alitaka na anapenda 'Kufagiliwa' si angenitafuta tu GENTAMYCINE ili anipe Jina lake na nimtumie Mwanamuziki JB Mpiana na Bendi yake ya Wenge BCBG ili Wamtaje ( Wamfagilie ) sana katika Album yao iliyoko Jikoni sasa tayari Kupakuliwa kwa Wapenda Muziki?

Ila na Wewe Padre lazima Polisi Kwanza ikuhoji kwani haiingii Akili huyo Mtoto ana Wazazi wake Wawili halafu Wewe ukaamua 'Kumfagilia' tu Mkewe Marehemu na Yeye ( Marehemu Mume ) ukamuacha. Hivi hapa akina GENTAMYCINE tukihisi kuwa huenda kulikuwa na lililojificha kati yako na Mkewe tutakuwa tunakosea?
Inawezekana huyo mke wa marehemu alikuwa chakula ya huyo Mchungaji
 
Mwanaume mmoja kutoka wilayani Ludewa amekatisha uhai wake kwa kujinyonga sababu ikiwa ni kutotajwa na padri katika misa ya Shukrani.

Bwana huyo na mke wake walikuwa wakitoa Shukrani katika Kanisa la Moravian kwa mtoto wao kupona lakini kwa sababu zisizofahamika Padri aliyeongoza misa hio alimtaja mama wa mtoto pekee na kumuacha yeye baba bila kutajwa hali iliyoleta sintofahamu.

............................
Habari Kamili;

MKAZI wa mtaa wa Kanisani B uliopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe anaefahamika kwa jina la Raban Razalo (48) amefariki kwa kujinyonga na waya kwa madai ya kutoridhishwa na kitendo cha Padri wa kanisa la Moravian kushindwa kumtaja jina wakati wa misa ya sadaka ya shukrani iliyofanywa na mkewe baada ya mtoto wao wa miaka 10 kupona majeraha ya kuvunjika mguu.

Kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Njombe, Hamis Issa amesema taarifa zilizobainiwa na jeshi hilo ni kwamba mtoto wa familia hiyo mwenye umri wa miaka 10 alivunjika mguu na kupelekea familia kuzunguka katika hospitali tofauti kupata matibu na kisha kupona jambo ambalo limemsukuma mama kwenda kanisani kutoa sadaka ya shukrani ambayo imekuwa chanzo cha kuondoa maisha ya baba wa familia.

“Walivyoenda kutoa sadaka ya shukrani,Padri wa kanisa hilo amemtaja mama wa mtoto peke yake, baba imemletea sintofahamu na matokeo yake baba ameamua kujinyonga kwa kutumia waya wa TTCL.

Kamanda Issa ametoa wito kwa viongozi wa dini kuangalia umuhimu wa familia kwa kuwa inaundwa na baba na mama.

“Viongoizi wa dini angalieni umuhimu wa familia,familia ni baba na mama,ukimtaja mmoja matokeo yake ndipo unapopata sintofahamu na maamuzi yasiyo kuwa na tija”amesema kamanda Issa.

Aidha ametoa rai kwa wanafamilia kutochukua maamuzi kwa jambo ambalo wamekwazika huku akisikitika kwa familia hiyo kumuuguza mtoto mpaka kupona na baadaye mzazi anafariki.


Chanzo: RFA

Padre atakuwa anapiga mzigo huo
 
Uchunguzi uanze na huo waya wa TTCL aliupatia wapi maana Kuna uhujumu uchumi hapo, rip Marehemu ngoja wenzio tuendelee kula ugali one day tutakutana
 
Iringa kuna shida kubwa! Roho ya kujinyonga imetawala sana huko tena kwa vitu vidogo.
 
Back
Top Bottom