Ajenda ya kupinga ufisadi: Ni ya CHADEMA kama Chama au ilikuwa ya Dr Slaa. Pekee?

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
WanaJF,

Ningeomba wana CHADEMA msaidie Watanzania kuelewa kuhusu ajenda ya kupinga ufisadi ndani ya chama chenu kupitia uzi huu.

Kwa maana Watanzania wote wamekifahamu chama chenu (CHADEMA) kwa ajenda hii ya kupinga ufisadi na sio kwa jambo lingine lolote lile. Ni ajenda ya ufisadi ndio iliipa CHADEMA nguvu na nikiri tu, ajenda hiyo ndio ilikuwa ikiitoa CCM jasho kwa wakati ule kabla Lowassa na genge lake hawajatoka rasmi CCM.

Na kumbukumbu zinaonyesha kuwa ajenda ya ufisadi ilikuwa ikisimamiwa kikamilifu na Dkt Slaa kipindi akiwa katibu mkuu wa CHADEMA. Ni mara chache sana kuona viongozi wengine waandamizi wakikemea ufisadi kama ambavyo alikuwa akikemea Dkt Slaa.

Sasa tangu Dkt Slaa atoke rasmi ndani ya CHADEMA, mimi na Watanzania wengi hatujasikia kabisa CHADEMA ikikemea ufisadi au hata kumpongeza rais aliyepo madarakani ambae tangu ameingia amekuwa akiwasaka mafisadi kwa nguvu zake zote.

Je, ajenda ya ufisadi imepotelea wapi huko CHADEMA? Je, ajenda ya ufisadi ilikuwa ni ya chama ama ya Dkt Slaa pekee!? Kama ni ya chama, iweje tangu Dkt Slaa atoke CHADEMA, chama kimekuwa bubu kuhusu ufisadi!? Je, CHADEMA itabaki hai pasipo kukemea ufisadi kama ilivyokuwa huko zamani?
 
Wataipingaje ilihali walikaribisha kirusi? Watie boriti kwanza ndipo watafute vibanzi
 
Bunge lijalo tunaanza na mapapa wa ufisadi kule bandarini Saada mkuya na mwigulu....hawa ndio wezi wa makontena yetu .....subirini muone
 
Bunge lijalo tunaanza na mapapa wa ufisadi kule bandarini Saada mkuya na mwigulu....hawa ndio wezi wa makontena yetu .....subirini muone

wee zama za Saada na Mwigulu zilishapita. sasa hivi tuna serikali mpya! bado unaota nini
 
wee zama za Saada na Mwigulu zilishapita. sasa hivi tuna serikali mpya! bado unaota nini

Mafisadi hao wapo bado wanatakiwa wawe segerea Mwigulu na saada ndo ...mapapa wa ufisadi......
 
Kampeni zimeisha....sasa tuna taka hawa mapapa waliokuwa wanajiita wazalebdo kumbe ndo walaji wakubwa ....Mwigulu na Saada mapapa wa ufisadi.....

Wamefisadi nini hao unao wataja? Maana naona umeshupalia kweli. Lowassa ni fisadi wa RICHMOND na tunajua ushirika wake na hadi leo taifa linaendelea kupata hasara kwa ufisadi wa Lowassa. Hemu tueleze huo ufisadi wa hao unao wataja ni upi na walishiriki vipi kuufanya huo ufisadi?
 
Wamefisadi nini hao unao wataja? Maana naona umeshupalia kweli. Lowassa ni fisadi wa RICHMOND na tunajua ushirika wake na hadi leo taifa linaendelea kupata hasara kwa ufisadi wa Lowassa. Hemu tueleze huo ufisadi wa hao unao wataja ni upi na walishiriki vipi kuufanya huo ufisadi?

Wamefisadi Bandari kontena zaidi ya 2000 ,,walizopiga sio mchezo nawashangaa kama richmond....lowasa yake makufuli kwa nn hampeleki segerea....ila ma ccm bi wez sana ......tena kwenye kushtakiwa mwakyembe na sita wasisahaulike.mabilion wamepiga kule TRL...pia....
 
WanaJF,

Ningeomba wana CHADEMA msaidie Watanzania kuelewa kuhusu ajenda ya kupinga ufisadi ndani ya chama chenu kupitia uzi huu.

Kwa maana Watanzania wote wamekifahamu chama chenu (CHADEMA) kwa ajenda hii ya kupinga ufisadi na sio kwa jambo lingine lolote lile. Ni ajenda ya ufisadi ndio iliipa CHADEMA nguvu na nikiri tu, ajenda hiyo ndio ilikuwa ikiitoa CCM jasho kwa wakati ule kabla Lowassa na genge lake hawajatoka rasmi CCM.

Na kumbukumbu zinaonyesha kuwa ajenda ya ufisadi ilikuwa ikisimamiwa kikamilifu na Dkt Slaa kipindi akiwa katibu mkuu wa CHADEMA. Ni mara chache sana kuona viongozi wengine waandamizi wakikemea ufisadi kama ambavyo alikuwa akikemea Dkt Slaa.

Sasa tangu Dkt Slaa atoke rasmi ndani ya CHADEMA, mimi na Watanzania wengi hatujasikia kabisa CHADEMA ikikemea ufisadi au hata kumpongeza rais aliyepo madarakani ambae tangu ameingia amekuwa akiwasaka mafisadi kwa nguvu zake zote.

Je, ajenda ya ufisadi imepotelea wapi huko CHADEMA? Je, ajenda ya ufisadi ilikuwa ni ya chama ama ya Dkt Slaa pekee!? Kama ni ya chama, iweje tangu Dkt Slaa atoke CHADEMA, chama kimekuwa bubu kuhusu ufisadi!? Je, CHADEMA itabaki hai pasipo kukemea ufisadi kama ilivyokuwa huko zamani?
Mleta uzi uko sawa kuleta huu uzi, na ni wazi ufisadi ilikuwa ni ajenda ya Dr. Slaa.
Chadema kumbe wao hawana ajenda, ile ni ya Slaa. Wao ni kudandia matukio, sasa watasubiri kifo cha mwanachadema mwingine wapake rangi tena.
 
MAGUFULI KATIKA KAMPENI ALIONGELEA KUPIGA VITA UFISADI; LOWASA KATIKA KAMPENI HAKUWAHI KUONGELEA UFISADI; CHADEMA AJENDA YA UFISADI ILIKUFA KIFO CHA MENDE SIKU WALIPOMKARIBISHA LOWASA!!!!:lock1::lock1::lock1::lock1:
 
Wamefisadi Bandari kontena zaidi ya 2000 ,,walizopiga sio mchezo nawashangaa kama richmond....lowasa yake makufuli kwa nn hampeleki segerea....ila ma ccm bi wez sana ......tena kwenye kushtakiwa mwakyembe na sita wasisahaulike.mabilion wamepiga kule TRL...pia....

Kajifunze kwanza kuandika...ukiweza kuandika vizuri ndio urudi kumwaga pumba zako JF. Maana hueleweki unataka kusema nini!
 
Wamefisadi nini hao unao wataja? Maana naona umeshupalia kweli. Lowassa ni fisadi wa RICHMOND na tunajua ushirika wake na hadi leo taifa linaendelea kupata hasara kwa ufisadi wa Lowassa. Hemu tueleze huo ufisadi wa hao unao wataja ni upi na walishiriki vipi kuufanya huo ufisadi?

Mahakama zipo...kwanini usiende kumfungulia kesi??
 
Mambo ya slaa na ajenda yameshapita!!! Kuna jamaa anahurumia nchi na wananchi wanyonge. Ndio habari kuu. Watu wawajibike. Kurudi kwa slaa na ajenda yake hakuna nafasi kwa sasa. Kabda 2020
 
Swali lako halina msingi.Lowasa si lolote ndani ya chama.Swala la ufisadi bado limo huko ccm.eg.Uliza kuhusu umeme wa upepo Saada na wenzake kwanini hadi sasa wananchi wamekataa kuachia maeneo yao.Lowasa bado ni zao bovu la ccm.Hivyo chama hakina agenda moja.Hivyo acha unafki.Tutawaumbua walio wengi zaidi subiri.
 
Back
Top Bottom