Ajali zinazosababishwa na magari binafsi zimezidi kuongezeka katika kipindi cha miezi sita ya 2019 na sasa inazidi ajali za bodaboda

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
AJALI zinazosababishwa na magari binafsi zimezidi kuongezeka kwa kasi katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo wa mwaka huu na sasa inazidi hata vifo vya ajali zitokanazo na pikipiki maarufu kama bodaboda ambazo ndizo zilikuwa zikiongoza kwa kusababisha vifo.

Takwimu za Jeshi la Polisi katika kipindi cha miezi sita Januari hadi Juni 2019 zinaonesha kuwa magari binafsi ndiyo yamekuwa vinara wa kusabisha ajali zinazosababisha vifo na hata majeruhi.

Wadau wa usalama barabarani wanaonya kuwa hali inaweza kuwa mbaya zaidi kama hatua za haraka hazitachukuliwa, kwani kwa mujibu wa takwimu rasmi za Jeshi la Polisi (Januari mpaka Juni 2019), magari binafsi yamesababisha ajali 528, vifo 222 na majeruhi 453, kwa wastani; kila siku magari binafsi husababisha ajali tatu, kifo cha mtu mmoja mpaka wawili na majeruhi wawili.

Kwa miezi sita ya mwanzo ya mwaka huu pikipiki zimesababisha ajali 334, vifo 176, majeruhi 319, kwa wastani pikipiki zinahusika katika ajali mbili kila siku na kusababisha kifo cha mtu mmoja tu, na mmoja mpaka wawili.

Takwimu zingine zinaonesha mabasi ya abiria yakipata ajali 103, na kusababisha vifo 61 na majeruhi 195 katika kipindi hicho.

Pia ripoti hiyo inaonesha malori yalihusika katika ajali 167, na kusababisha vifo vya watu 130 na majeruhi 142, wakati daladala zilipata ajali 143, na kusababisha vifo 89 na majeruhi 268.

Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Deus Sokoni alisema wanachukua hatua mbalimbali kudhibiti ajali za magari binafsi ikiwemo kufungia leseni za madereva wanaosababisha ajali kwa uzembe, na kujihusisha na ulevi, mwendokasi na makosa mengineyo.

Alisema pia wanatarajia kufanyika kwa mabadiliko ya kisheria ambayo yatasaidia kudhibiti magari binafsi katika masuala mbalimbali ikiwemo mwendokasi, ulevi pamoja na ufungaji wa mikanda.

Utafiti wa WHO unasema kufunga mkanda wa usalama humsaidia abiria wa mbele kujikinga na madhara ya ajali kwa asilimia 40 mpaka 50, na asilimia 50-75 kwa abiria waliokaa viti vya nyuma.

Ripoti ya Usalama Barabarani ya Shirika la Afya Dunia (WHO) iliyotolewa mwaka 2018, inabainisha kuwa Sheria za Tanzania zina upungufu katika kudhibiti usalama barabarani ikiwamo kuruhusu kiwango kikubwa cha ulevi kwa madereva bila kujali uzoefu wa dereva katika kazi husika.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi nchini, zaidi ya ajali 2,250 zimerekodiwa kuwa zilitokana na ulevi kati ya mwaka 2006 mpaka 2017 huku magari binafsi yakitajwa kuhusika zaidi kwenye ajali hizo.


Chanzo: Habarileo
 
Ripoti ya Usalama Barabarani ya Shirika la Afya Dunia (WHO) iliyotolewa mwaka 2018, inabainisha kuwa Sheria za Tanzania zina upungufu katika kudhibiti usalama barabarani ikiwamo kuruhusu kiwango kikubwa cha ulevi kwa madereva bila kujali uzoefu wa dereva katika kazi husika.
 
Takwimu za Jeshi la Polisi katika kipindi cha miezi sita Januari hadi Juni 2019 zinaonesha kuwa magari binafsi ndiyo yamekuwa vinara wa kusabisha ajali zinazosababisha vifo na hata majeruhi.


Magari yananunuliwa kwa wingi sana na wengi wa wanaonunua hujifunza kuendesha kwa muda mfupi sana na kuingia nayo barabarani, nina majirani kadhaa wamewanunulia wake zao magari na kutokana na kujifunza kwa muda mfupi sana wamepata nayo ajali mbaya
 
Katika taaluma ya udereva/udereva wa kujihami unabainisha vyanzo vikuu vitatu vya ajali za vyombo vya moto
.binadamu( pia viumbe hai kwa ujumla
.miundo mbinu/mazingira km vile ubovu wa barabara, alama za tahadhari,alama za dharua na onyo pia
.chombo( ubovu wa chombo chenye either kabla ama kikiwa katika mchakato wa kutembea mean kipo katika motion then brake imefail au tyre imepasuka ghafla

So yote ya yote suala la ajali ni mtambuka sana japo tumekandia kisababishi kimoja tu cha binadamu(dereva) na tumemwacha binadamu mwingne awe hana hati kama(watembea kwa miguu,waendesha baiskel na wanyama wengne wengi wenye wigo wa kumfanya dereva atetereke mpk atoke nje ya njia )
Note
Madereva wanapitia mengi sana maana kuna njia zingine zito,hazipitiki kwa ujua na harakaharaka, zinahitaji utulivu wa moyo, nafsi na mwili wakuu
 
Japo
Gari na dereva vyaweza kuwa visababishi lakini MIUNDO MBINU huenda ikachukua % nyingi
Jiulize hivi kuna eneo Mbeya kila wakati ajali zinatokea eneo hilo
Je Dereva au Gari huanza kumiss behave hapo tu

Barabara zimebonyea kupita maelezo
Hazina curve hata kwenye kona ni flat kama sebule
Je kanuni za ki fizikia zinafuatwa?
 
Automatic unaendesha na mguu wa kulia tu ukiachia mafuta unakanyaga breki..
Hairuhusiwi kutumia wa kushoto kukanyaga breki na wa kulia mafuta mda wowote majanga
sio kweli nina Miaka 9 sijawahi pata ajali inayohusu hiyo scenario yako!!..Na kuna kipindi napiga safari dsm-mbeya au dsm-shinyanga!.
 
Sasa manual clutch utakanyaga na nini?? Kama auto unatumia miguu yote ukiendesha manual unafanyaje??
sio kweli nina Miaka 9 sijawahi pata ajali inayohusu hiyo scenario yako!!..Na kuna kipindi napiga safari dsm-mbeya au dsm-shinyanga!.
 
Magari yananunuliwa kwa wingi sana na wengi wa wanaonunua hujifunza kuendesha kwa muda mfupi sana na kuingia nayo barabarani, nina majirani kadhaa wamewanunulia wake zao magari na kutokana na kujifunza kwa muda mfupi sana wamepata nayo ajali mbaya
Automatic transmission gear error! Manually gear mtu ulikua unajifunza si chini ya miezi mitatu nowadays driving school wiki mbili mpaka mwezi mtu anakua tayari kuingia barabarani, hii ni hatari.Yote kwa yote ni Kumwomba Mungu Atuepushe na Ajai. Amen
 
Automatic unaendesha na mguu wa kulia tu ukiachia mafuta unakanyaga breki..
Hairuhusiwi kutumia wa kushoto kukanyaga breki na wa kulia mafuta mda wowote majanga
Kutumia miguu miwili it's more comfortable, Ila inahitaji ufundi na uzoefu. Usiigeeeeee
 
Kutumia miguu miwili it's more comfortable, Ila inahitaji ufundi na uzoefu. Usiigeeeeee
Hii haipo sawa , kutumia miguu miwili auto ni uvivu. Ukitakiwa kufanya maamuzi ya gafra ni rahisi kuchanganya. Mguu wa kulia unatakiwa ufanye yote kwa ama mafuta au breki.
 
Back
Top Bottom